< 2 Tarihler 31 >

1 Bütün bunlar sona erince, oradaki İsrailliler Yahuda kentlerine giderek dikili taşları parçalayıp Aşera putlarını devirdiler. Yahuda, Benyamin, Efrayim ve Manaşşe bölgelerindeki puta tapılan yerlerin ve sunakların hepsini yıktılar. Sonra herkes kendi kentine, toprağına döndü.
Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
2 Hizkiya kâhinlerle Levililer'i görevlerine göre bölüklere ayırdı. Kimine yakmalık sunuları ve esenlik sunularını sunma, kimine hizmet etme, kimine de RAB'bin Konutu'nun kapılarında şükredip övgüler söyleme görevini verdi.
Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
3 Kral da RAB'bin Yasası uyarınca sabah akşam sunulmak üzere yakmalık sunular, Şabat günleri, Yeni Ay ve bayramlarda sunulacak yakmalık sunular için sürüsünden hayvanlar verdi.
Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
4 Yeruşalim'de yaşayan halka da kâhinlerle Levililer'in paylarına düşeni vermelerini buyurdu; öyle ki, RAB'bin Yasası'na kendilerini adayabilsinler.
Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
5 Kralın bu buyruğunu duyar duymaz İsrailliler ilk yetişen tahıl, yeni şarap, zeytinyağı, bal ve bütün tarla ürünlerinden bol bol verdiler. Bunun yanısıra her şeyin ondalığını da bol bol getirdiler.
Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
6 Yahuda kentlerinde yaşayan İsrailliler'le Yahudalılar da sığırlarının, davarlarının, Tanrıları RAB'be adamış oldukları kutsal armağanların ondalığını getirip bir araya yığdılar.
Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
7 Ondalıkların toplanması üçüncü aydan yedinci aya kadar sürdü.
Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
8 Hizkiya ile önderler gelip yığınları görünce, RAB'be övgüler sunup halkı İsrail'i kutsadılar.
Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
9 Hizkiya kâhinlerle Levililer'e yığınları sorunca,
Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
10 Sadok soyundan Başkâhin Azarya şu yanıtı verdi: “Halk RAB'bin Tapınağı'na bağış getirmeye başladıktan bu yana yiyip doyduk; üstelik artırdık da. Çünkü RAB halkını kutsadı. Bu büyük yığın da artakalandır.”
naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
11 Hizkiya RAB'bin Tapınağı'ndaki depoların hazırlanması için buyruk verdi. Depolar hazırlandı.
Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
12 Bağışlar, ondalıklar, adanan armağanlar sadakatle içeri getirildi. Bütün bu işlerin sorumlusu olarak Levili Konanya atandı; kardeşi Şimi de yardımcısı oldu.
Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
13 Kral Hizkiya ile Tanrı'nın Tapınağı'nın sorumlusu Azarya, Konanya ile kardeşi Şimi'nin yönetimindeki şu denetçileri atadılar: Yehiel, Azazya, Nahat, Asahel, Yerimot, Yozavat, Eliel, Yismakya, Mahat, Benaya.
Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
14 Tapınağın Doğu Kapısı'nın nöbetçisi Yimna'nın oğlu Levili Kore, Tanrı'ya gönülden verilen sunuların sorumlusuydu. RAB'be adanan bağışları ve kutsal yiyecekleri dağıtmak için bu göreve getirilmişti.
Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
15 Eden, Minyamin, Yeşua, Şemaya, Amarya ve Şekanya kâhinlerin yaşadıkları kentlerde bölükleri uyarınca büyük küçük bütün kardeşlerine bağışları dağıtma işinde Kore'ye sadakatle yardım ettiler.
Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
16 Ayrıca soyağacında adı kayıtlı üç ve daha yukarı yaştaki erkeklere, bölüklerine ve sorumluluklarına göre RAB'bin Tapınağı'na girip günün gerektirdiği değişik görevleri yapanların tümüne; bağlı oldukları boylara göre kütüğe kayıtlı kâhinlere, bölüklerine ve sorumluluklarına göre yirmi ve daha yukarı yaştaki Levililer'e; kâhinlerle Levililer'in soyağacında kayıtlı küçük çocuklara, kadınlara, oğullarla kızlara, yani topluluğa yiyecek dağıtıyorlardı. Çünkü kendilerini sadakatle Tanrı'ya adamışlardı.
Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
19 Kentlerinin çevresindeki kırlarda ya da herhangi bir kentte yaşayan Harun soyundan kâhinlere gelince, onlardan olan bütün erkeklere ve Levililer'in soyağacında kayıtlı herkese yiyecek dağıtmak için belirli kişiler atanmıştı.
Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
20 Hizkiya bütün Yahuda'da böyle davrandı; Tanrısı RAB'bin önünde iyi, doğru ve hakça olanı yaptı.
Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
21 Tanrı'nın Tapınağı'nda üstlendiği görevi bütün yüreğiyle yerine getirdi; Kutsal Yasa'ya, buyruklara uydu; Tanrısı'na yöneldi. Bu sayede başarılı oldu.
Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.

< 2 Tarihler 31 >