< 1 Timoteos 3 >

1 İşte güvenilir söz: Bir kimse gözetmen olmayı gönülden istiyorsa, iyi bir görev arzu etmiş olur.
Msemo huu ni wa kweli: mtu akitaka kuwa kiongozi katika kanisa, huyo anatamani kazi nzuri.
2 Ancak gözetmen ayıplanacak bir yanı olmayan, tek karılı, ölçülü, sağduyulu, saygın, konuksever, öğretmeye yetenekli biri olmalı.
Basi, kiongozi wa kanisa anapaswa awe mtu asiye na lawama; anapaswa awe na mke mmoja tu, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu; ni lazima awe mkarimu na anayeweza kufundisha;
3 Şarap düşkünü, zorba olmamalı; uysal, kavgadan ve para sevgisinden uzak olmalı.
asiwe mlevi au mtu wa matata, bali awe mpole, apendaye amani; asiwe mtu wa kupenda fedha;
4 Evini iyi yönetmeli, çocuklarına söz dinletmeli, her yönden saygılı olmalarını sağlamalı.
anapaswa awe mtu awezaye kuongoza vema nyumba yake, na kuwafanya watoto wake wawe watii kwa heshima yote.
5 Kendi evini yönetmesini bilmeyen, Tanrı'nın topluluğunu nasıl kayırabilir?
Maana kama mtu hawezi kuongoza vema nyumba yake, atawezaje kulitunza kanisa la Mungu?
6 Gözetmen yeni iman etmiş biri olmamalı. Yoksa gurura kapılıp İblis'in uğradığı yargıya uğrayabilir.
Mtu ambaye hajakomaa bado katika imani asifanywe kuwa kiongozi katika kanisa, asije akajaa majivuno na kuhukumiwa kama vile Ibilisi alivyohukumiwa.
7 Topluluğun dışındakiler tarafından da iyi bir insan olarak tanınmalıdır. Öyle ki, ayıplanacak duruma ve İblis'in tuzağına düşmesin.
Anapaswa awe mwenye sifa njema kati ya watu walio nje ya kanisa, ili asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa Ibilisi.
8 Aynı şekilde kilise görevlileri, özü sözü ayrı, şarap tutkunu, haksız kazanç peşinde koşan kişiler değil, ağırbaşlı kişiler olmalı.
Wasaidizi katika kanisa wanapaswa pia kuwa watu wenye tabia njema na wanyofu; wasiwe wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha;
9 Temiz vicdanla imanın sırrına sarılmalıdırlar.
wanapaswa kuzingatia kwa dhamiri njema ukweli wa ndani wa imani.
10 Bunlar da önce denensin; eleştirilecek bir yönleri yoksa görev alsınlar.
Ni lazima kwanza wathibitishwe, na wakionekana kuwa wanafaa, basi, watoe huduma yao.
11 Aynı şekilde kadınlar ağırbaşlı olmalı; iftiracı değil, ama ölçülü ve her bakımdan güvenilir olmalı.
Wake zao wanapaswa pia kuwa na tabia njema, wasiowasengenya watu, wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote.
12 Görevliler tek karılı, çocuklarını ve evlerini iyi yöneten kişiler olsun.
Msaidizi katika kanisa lazima awe na mke moja tu, na awezaye kuongoza vema watoto wake na nyumba yake.
13 Görevlerini iyi yapanlar, kendileri için iyi bir yer edinir, Mesih İsa'ya imanda büyük cesaret kazanırlar.
Maana wasaidizi wanaofanya kazi yao vizuri hujipatia msimamo mzuri, na wanaweza kusema bila hofu juu ya imani yao katika Kristo Yesu.
14 Yakında yanına gelmeyi umuyorum. Ama gecikirsem, gerçeğin direği ve dayanağı olan Tanrı'nın ev halkı arasında, yani yaşayan Tanrı'nın topluluğunda nasıl davranmak gerektiğini bilesin diye sana bunları yazıyorum.
Ninakuandikia barua hii nikiwa na matumaini ya kuja kwako hivi karibuni.
Lakini kama nikicheleweshwa, basi, barua hii itakufahamisha mwenendo tunaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, na ambalo ni nguzo na msingi wa ukweli.
16 Kuşkusuz Tanrı yolunun sırrı büyüktür. O, bedende göründü, Ruh'ça doğrulandı, Meleklerce görüldü, Uluslara tanıtıldı, Dünyada O'na iman edildi, Yücelik içinde yukarı alındı.
Hakuna mashaka yoyote juu ya ukuu wa siri ya dini yetu: Alionekana katika umbo la kibinadamu alithibitishwa na Roho kuwa ni mwadilifu, akaonekana na malaika. Alihubiriwa kati ya mataifa, aliaminiwa popote ulimwenguni, akachukuliwa juu mbinguni katika utukufu.

< 1 Timoteos 3 >