< 1 Tarihler 17 >

1 Davut sarayına yerleştikten sonra Peygamber Natan'a, “Bak, ben sedir ağacından yapılmış bir sarayda oturuyorum. Oysa RAB'bin Antlaşma Sandığı bir çadırın altında duruyor!” dedi.
Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”
2 Natan, “Tasarladığın her şeyi yap, çünkü Tanrı seninledir” diye karşılık verdi.
Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.”
3 O gece Tanrı Natan'a şöyle seslendi:
Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:
4 “Git, kulum Davut'a şöyle de: ‘RAB diyor ki, oturmam için bana tapınak yapmayacaksın.
“Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo.
5 İsrail halkını Mısır'dan çıkardığım günden bu yana tapınakta oturmadım. Bir çadırdan öbür çadıra, orada burada konaklayarak dolaştım.
Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine.
6 İsrailliler'le birlikte dolaştığım yerlerin herhangi birinde, halkımı gütmesini buyurduğum İsrail önderlerinden birine, neden bana sedir ağacından bir konut yapmadınız diye hiç sordum mu?’
Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’
7 “Şimdi kulum Davut'a şöyle diyeceksin: ‘Her Şeye Egemen RAB diyor ki: Halkım İsrail'e önder olasın diye seni otlaklardan ve koyun gütmekten aldım.
“Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli.
8 Her nereye gittiysen seninleydim. Önünden bütün düşmanlarını yok ettim. Adını dünyadaki büyük adamların adı gibi büyük kılacağım.
Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
9 Halkım İsrail için bir yurt sağlayıp onları oraya yerleştireceğim. Bundan böyle kendi yurtlarında otursunlar, bir daha rahatsız edilmesinler. Kötü kişiler de halkım İsrail'e hâkimler atadığım günden bu yana yaptıkları gibi, bir daha onlara baskı yapmasınlar. Bütün düşmanlarının sana boyun eğmesini sağlayacağım. RAB'bin senin için bir soy yetiştirecek, bilesin.
Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote. “‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba:
11 “‘Sen ölüp atalarına kavuşunca, senden sonra oğullarından birini ortaya çıkarıp krallığını pekiştireceğim.
Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake.
12 Benim için tapınak kuracak olan odur. Ben de onun tahtını sonsuza dek sürdüreceğim.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele.
13 Ben ona baba olacağım, o da bana oğul olacak. Senden önceki kraldan esirgediğim sevgiyi hiçbir zaman esirgemeyeceğim.
Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia.
14 Onu sonsuza dek tapınağımın ve krallığımın üzerine atayacağım; tahtı sonsuza dek sürecektir.’”
Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’”
15 Böylece Natan bütün bu sözleri ve görümleri Davut'a aktardı.
Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
16 Bunun üzerine Kral Davut gelip RAB'bin önünde oturdu ve şöyle dedi: “Ya RAB Tanrı, ben kimim, ailem nedir ki, beni bu duruma getirdin?
Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
17 Ey Tanrı, sanki bu yetmezmiş gibi, kulunun soyunun geleceği hakkında da söz verdin. Benimle de büyük bir adammışım gibi ilgilendin, ya RAB Tanrı!
Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.
18 Kulunu onurlandırdın, ben sana başka ne diyebilirim ki! Çünkü sen kulunu tanıyorsun.
“Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako,
19 Ya RAB, kulunun hatırı için ve isteğin uyarınca bu büyüklüğü gösterdin ve bu büyük vaatleri bildirdin.
Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.
20 “Ya RAB, bir benzerin yok, senden başka tanrı da yok! Bunu kendi kulaklarımızla duyduk.
“Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe.
21 Halkın İsrail'e benzer tek bir ulus yok dünyada. Kendi halkın olsun diye onları kurtarmaya gittin. Büyük ve görkemli işler yapmakla ün saldın. Mısır'dan kurtardığın halkın önünden ulusları kovdun.
Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
22 Halkın İsrail'i sonsuza dek kendi halkın olarak seçtin ve sen de, ya RAB, onların Tanrısı oldun.
Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.
23 “Şimdi, ya RAB, kuluna ve onun soyuna ilişkin verdiğin sözü sonsuza dek tut, sözünü yerine getir.
“Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi,
24 Öyle ki, insanlar, ‘İsrail'i kayıran, Her Şeye Egemen RAB Tanrı İsrail'in Tanrısı'dır!’ diyerek adını sonsuza dek ansınlar, yüceltsinler ve kulun Davut'un soyu da önünde sürsün.
ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.
25 “Sen, ey Tanrım, ben kulun için bir soy çıkaracağını bana açıkladın. Bundan dolayı kulun önünde sana dua etme yürekliliğini buldu.
“Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya.
26 Ya RAB, sen Tanrı'sın! Kuluna bu iyi sözü verdin.
Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
27 Şimdi önünde sonsuza dek sürmesi için kulunun soyunu kutsamayı uygun gördün. Çünkü, ya RAB, onu kutsadığın için sonsuza dek kutlu kılınacak.”
Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”

< 1 Tarihler 17 >