< 1 Tarihler 15 >

1 Davut kendisine Davut Kenti'nde evler yaptı. Ardından Tanrı'nın Antlaşma Sandığı için bir yer hazırlayıp çadır kurdu.
Baada ya Daudi kujijengea nyumba zake katika Mji wa Daudi, akatengeneza sehemu kwa ajili ya Sanduku la Mungu, kisha akasimamisha hema kwa ajili yake.
2 Sonra, “Tanrı'nın Antlaşma Sandığı'nı yalnız Levililer taşıyacak” dedi, “Çünkü sandığı taşımak ve sonsuza dek kendisine hizmet etmek için RAB Levililer'i seçti.”
Kisha Daudi akasema, “Hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kulibeba Sanduku la Mungu isipokuwa Walawi peke yao, kwa sababu Bwana aliwachagua kulibeba Sanduku la Bwana na kuhudumu mbele zake milele.”
3 Davut RAB'bin Antlaşma Sandığı'nı hazırlamış olduğu yere getirmek için bütün İsrailliler'i Yeruşalim'de topladı.
Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Bwana na kulileta hadi kwenye sehemu aliyokuwa ametengeneza kwa ajili yake.
4 Sonra Harunoğulları'yla Levililer'i bir araya getirdi:
Kisha Daudi akawakusanya pamoja wazao wa Aroni na Walawi:
5 Kehatoğulları'ndan: Önder Uriel'le 120 yakını,
Kutoka wazao wa Kohathi, Urieli kiongozi na ndugu zake 120,
6 Merarioğulları'ndan: Önder Asaya'yla 220 yakını,
Kutoka wazao wa Merari, Asaya kiongozi na ndugu zake 220.
7 Gerşonoğulları'ndan: Önder Yoel'le 130 yakını,
Kutoka wazao wa Gershoni, Yoeli kiongozi na ndugu zake 130.
8 Elisafanoğulları'ndan: Önder Şemaya'yla 200 yakını,
Kutoka wazao wa Elisafani, Shemaya kiongozi na ndugu zake 200.
9 Hevronoğulları'ndan: Önder Eliel'le 80 yakını,
Kutoka wazao wa Hebroni, Elieli kiongozi na ndugu zake 80.
10 Uzzieloğulları'ndan: Önder Amminadav'la 112 yakını.
Kutoka wazao wa Uzieli, Aminadabu kiongozi na ndugu zake 112.
11 Bundan sonra Davut Kâhin Sadok'la Kâhin Aviyatar'ı, Levili Uriel'i, Asaya'yı, Yoel'i, Şemaya'yı, Eliel'i, Amminadav'ı yanına çağırdı.
Kisha Daudi akawaita makuhani Sadoki na Abiathari, pamoja na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli na Aminadabu.
12 Onlara şöyle dedi: “Siz Levili boyların başlarısınız. Levili kardeşlerinizle birlikte kendinizi kutsayın, sonra İsrail'in Tanrısı RAB'bin Antlaşma Sandığı'nı hazırlamış olduğum yere getirin.
Akawaambia, “Ninyi ndio viongozi wa jamaa za Walawi. Ninyi pamoja na Walawi wenzenu inawapasa mjitakase na kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli hadi mahali ambapo nimetengeneza kwa ajili yake.
13 Çünkü geçen sefer sandığı siz taşımadığınız ve biz de kurala uygun davranmadığımız için Tanrımız RAB bize öfkelendi.”
Ilikuwa ni kwa sababu hii, ninyi Walawi, hamkulipandisha Sanduku la Bwana mara ya kwanza, hata ikasababisha Bwana Mungu wetu kuwaka hasira dhidi yetu. Hatukumuuliza jinsi ya kufanya ili tupate kulileta jinsi alivyoagiza.”
14 Böylece kâhinlerle Levililer İsrail'in Tanrısı RAB'bin Antlaşma Sandığı'nı getirmek için kendilerini kutsadılar.
Kwa hiyo makuhani pamoja na Walawi wakajitakasa ili kulipandisha Sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
15 RAB'bin sözü uyarınca ve Musa'nın onlara buyurduğu gibi, Tanrı'nın Sandığı'nın sırıklarını omuzları üzerinde taşıdılar.
Nao Walawi wakalichukua Sanduku la Mungu mabegani mwao wakitumia mipiko, kama vile Mose alivyoamuru sawasawa na neno la Bwana.
16 Davut Levili önderlere, kardeşlerinden çenk, lir ve zil gibi çalgılar eşliğinde yüksek sesle sevinçli ezgiler okuyacak ezgiciler atamalarını söyledi.
Daudi akawaambia viongozi wa Walawi kuwaweka ndugu zao waimbaji ili waimbe nyimbo za shangwe, wakiwa na vyombo vya uimbaji: zeze, vinubi na matoazi.
17 Levililer de Yoel oğlu Heman'ı, akrabalarından Berekya oğlu Asaf'ı, akrabaları Merarioğulları'ndan Kuşaya oğlu Etan'ı atadılar.
Basi Walawi wakawaweka Hemani mwana wa Yoeli; kutoka miongoni mwa ndugu zake, Asafu mwana wa Berekia; kutoka miongoni mwa ndugu zao Wamerari, Ethani mwana wa Kushaiya;
18 Onlara yardımcı olarak da kapı nöbetçileri kardeşlerinden Zekeriya'yı, Yaaziel'i, Şemiramot'u, Yehiel'i, Unni'yi, Eliav'ı, Benaya'yı, Maaseya'yı, Mattitya'yı, Elifelehu'yu, Mikneya'yı, Ovet-Edom'u, Yeiel'i atadılar.
hawa ndio waliochaguliwa kuwa wasaidizi wao: Zekaria, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, Mikneya, pamoja na mabawabu Obed-Edomu na Yehieli.
19 Ezgicilerden Heman, Asaf, Etan tunç zil;
Waimbaji Hemani, Asafu na Ethani walichaguliwa kupiga matoazi ya shaba;
20 Zekeriya, Aziel, Şemiramot, Yehiel, Unni, Eliav, Maaseya, Benaya tiz perdeli çenk çalmak;
Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya na Benaya walikuwa wapiga zeze kufuatana na sauti ya alamothi,
21 Mattitya, Elifelehu, Mikneya, Ovet-Edom, Yeiel, Azazya sekiz telli lirle önderlik yapmak üzere seçildiler.
na Matithia, Elifelehu, Mikneya, Obed-Edomu, Yehieli na Azazia walikuwa wapiga vinubi, wakiongozwa kwa kufuata sauti ya sheminithi.
22 Levililer'in önderi Kenanya ise ezgilerden sorumluydu. Bu konuda yetenekliydi.
Kenania kiongozi wa Walawi alikuwa msimamizi wa uimbaji; huu ndio uliokuwa wajibu wake kwa sababu alikuwa stadi katika hilo.
23 Berekya ile Elkana Antlaşma Sandığı'nın bulunduğu yerin kapı nöbetçileriydi.
Berekia na Elikana walikuwa mabawabu kwa ajili ya Sanduku.
24 Şevanya, Yoşafat, Netanel, Amasay, Zekeriya, Benaya, Eliezer adındaki kâhinler Tanrı'nın Antlaşma Sandığı önünde borazan çalıyordu. Ovet-Edom ile Yehiya da Antlaşma Sandığı'nın bulunduğu yerin kapı nöbetçileriydi.
Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, makuhani, walikuwa wapiga tarumbeta mbele ya Sanduku la Mungu. Obed-Edomu na Yehiya waliwekwa pia kuwa mabawabu wa Sanduku.
25 Böylece Davut, İsrail ileri gelenleri ve binbaşılar RAB'bin Antlaşma Sandığı'nı Ovet-Edom'un evinden sevinçle getirmeye gittiler.
Basi Daudi pamoja na wazee wa Israeli na majemadari wa vikosi vya elfu wakaenda ili kulipandisha Sanduku la Agano la Bwana kutoka nyumba ya Obed-Edomu kwa shangwe.
26 Tanrı, RAB'bin Antlaşma Sandığı'nı taşıyan Levililer'e yardım ettiği için, yedi boğa ile yedi koç kurban ettiler.
Kwa sababu Mungu alikuwa amewasaidia Walawi waliokuwa wanalichukua Sanduku la Agano la Bwana, mafahali saba na kondoo dume saba walitolewa dhabihu.
27 Davut, sandığı taşıyan Levililer, ezgiciler ve ezgilerden sorumlu olan Kenanya ince ketenden cüppeler giyinmişlerdi. Davut ince keten efod da kuşanmıştı.
Basi Daudi alikuwa amevaa joho la kitani safi, kama walivyokuwa wamevaa Walawi wote waliokuwa wanalichukua lile Sanduku, waimbaji nao walivaa vivyo hivyo, pamoja na Kenania aliyekuwa anaongoza nyimbo za waimbaji. Daudi alivaa pia kisibau cha kitani safi.
28 Böylece İsrailliler sevinç naraları atarak, boru, borazan, zil, çenk ve lirler çalarak RAB'bin Antlaşma Sandığı'nı getiriyorlardı.
Hivyo Israeli wote wakalipandisha Sanduku la Agano la Bwana kwa shangwe, wakipiga pembe za kondoo dume, tarumbeta, matoazi, wakipiga zeze na vinubi.
29 RAB'bin Antlaşma Sandığı Davut Kenti'ne varınca, Saul'un kızı Mikal pencereden baktı. Oynayıp zıplayan Kral Davut'u görünce, onu içinden küçümsedi.
Sanduku la Agano la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akicheza na kusherehekea, akamdharau moyoni mwake.

< 1 Tarihler 15 >