< Job 37 >

1 Ja, vid sådant förskräckes mitt hjärta, bävande spritter det upp.
Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
2 Hören, hören huru hans röst ljuder vred, hören dånet som går ut ur hans mun.
Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
3 Han sänder det åstad, så långt himmelen når, och sina ljungeldar bort till jordens ändar.
Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
4 Efteråt ryter så dånet, när han dundrar med sin väldiga röst; och på ljungeldarna spar han ej, då hans röst låter höra sig.
Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
5 Ja, underbart dundrar Gud med sin röst, stora ting gör han, utöver vad vi förstå.
Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
6 Se, åt snön giver han bud: "Fall ned till jorden", så ock åt regnskuren, åt sitt regnflödes mäktiga skur.
Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
7 Därmed fjättrar han alla människors händer, så att envar som han har skapat kan lära därav.
Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
8 Då draga sig vilddjuren in i sina gömslen, och i sina kulor lägga de sig till ro.
Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
9 Från Stjärngemaket kommer då storm och köld genom nordanhimmelens stjärnor;
Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
10 med sin andedräkt sänder Gud frost, och de vida vattnen betvingas.
Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
11 Skyarna lastar han ock med väta och sprider omkring sina ljungeldsmoln.
Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
12 De måste sväva än hit, än dit, alltefter hans rådslut och de uppdrag de få, vadhelst han ålägger dem på jordens krets.
Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
13 Än är det som tuktoris, än med hjälp åt hans jord, än är det med nåd som han låter dem komma.
Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
14 Lyssna då härtill, du Job; stanna och betänk Guds under.
Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
15 Förstår du på vad sätt Gud styr deras gång och låter ljungeldarna lysa fram ur sina moln?
Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
16 Förstår du lagen för skyarnas jämvikt, den Allvises underbara verk?
Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
17 Förstår du huru kläderna bliva dig så heta, när han låter jorden domna under sunnanvinden?
Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
18 Kan du välva molnhimmelen så som han, så fast som en spegel av gjuten metall?
Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
19 Lär oss då vad vi skola säga till honom; för vårt mörkers skull hava vi intet att lägga fram.
Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
20 Ej må det bebådas honom att jag vill tala. Månne någon begär sitt eget fördärv?
Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
21 Men synes icke redan skenet? Strålande visar han sig ju mellan skyarna, där vinden har gått fram och sopat dem undan.
Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
22 I guldglans kommer han från norden. Ja, Gud är höljd i fruktansvärt majestät;
Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
23 den Allsmäktige kunna vi icke fatta, honom som är så stor i kraft, honom som ej kränker rätten, ej strängaste rättfärdighet.
Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
24 Fördenskull frukta människorna honom; men de självkloka -- dem alla aktar han ej på.
Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”

< Job 37 >