< Romarbrevet 9 >

1 Jag säger sanningen i Christo, och ljuger icke; som mitt samvete bär mig der vittne till i dem Helga Anda;
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 Att jag hafver ena stora sorg, och idkeliga pino i mitt hjerta.
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 Ty jag hafver sjelfver önskat mig bortkastad ifrå Christo, för mina bröders skull, som mig köttsliga skylde äro;
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 Hvilke äro af Israel, hvilkom barnaskapet tillhörer, och härligheten, och förbundet, och lagen, och Gudstjensten, och löften;
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 Hvilkas äro fäderna, der Christus af födder är, på köttsens vägnar; hvilken är Gud öfver all ting, lofvad evinnerliga. Amen. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Detta säger jag icke fördenskull, att Guds ord äro omintet vorden; ty de äro icke alle Israeliter, som äro af Israel;
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 Icke äro de heller alle söner, att de äro Abrahams säd; utan i Isaac skall dig kallas säden;
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 Det är: Icke äro de Guds barn, som äro barn efter köttet, utan de som äro barn efter löftet, de varda räknade för säd.
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 Ty detta är löftesordet: Jag skall komma i denna tiden; och Sara skall hafva en son.
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 Och icke allenast det; utan ock Rebecka vardt en gång hafvandes af Isaac, vårom fader.
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 Ty förr än barnen voro född, och hade hvarken godt eller ondt gjort (på det Guds uppsåt skulle blifva ståndandes efter utkorelsen, icke för gerningarnas skull, utan af kallarens nåde),
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 Vardt denne sagdt: Den större skall tjena dem mindre;
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 Såsom skrifvet är: Jacob älskade jag men Esau hatade jag.
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Hvad vilje vi då säga? Är Gud orättfärdig? Bort det.
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 Ty han säger till Mosen: Hvilkom jag är nådelig, honom är jag nådelig; och öfver hvilken jag förbarmar mig, öfver honom förbarmar jag mig.
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 Så står det nu icke till någors mans vilja eller lopp, utan till Guds barmhertighet.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 Ty Skriften säger till Pharao: Dertill hafver jag uppväckt dig, att jag skall bevisa mina magt på dig; och att mitt Namn skall varda förkunnadt i all land.
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 Så förbarmar han nu sig öfver hvem han vill, och hvem han vill, förhärdar han.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Så må du säga till mig: Hvad skyllar han då oss? Ho kan stå emot hans vilja?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 O menniska, ho äst du som vill träta med Gud? Icke säger det ting, som gjordt är, till sin mästare: Hvi hafver du gjort mig sådana?
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Hafver icke en pottomakare magt att göra af en klimp ett kar till heder, och det andra till vanheder?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 Derföre, då Gud ville låta se vredena, och kungöra sina magt, hafver han med stor tålsamhet lidit vredsens kar, som äro tillredd till fördömelse;
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 På det han skulle kungöra sina härlighets rikedom på barmhertighetenes kar, som han hafver tillredt till härlighet;
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 Hvilka han ock kallat hafver, nämliga oss, icke allenast af Judomen, utan ock af Hedningomen;
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 Såsom han ock säger genom Oseas: Det som icke var mitt folk, det skall jag kalla mitt folk; och den mig intet kär var, skall jag kalla min kära.
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 Och det skall ske, att der som hafver varit sagdt till dem: I ären icke mitt folk; der skola de varda kallade lefvandes Guds barn.
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 Men Esaias ropar för Israel: Om talet på Israels barn än vore som sanden i hafvet, så skola dock de igenlefde varda salige.
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 Ty han skall väl låta förderfva dem, och dock likväl stilla det förderfvet till rättfärdighet; ty Herren skall stilla förderfvet på jordene.
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 Och såsom Esaias sade tillförene: Hade icke Herren Zebaoth igenleft oss säd, då hade vi varit såsom Sodoma, och lika som Gomorra.
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 Hvad vilje vi då säga? Det säge vi: Hedningarna, som icke farit hafva efter rättfärdighetene, de hafva fått rättfärdigheten; den rättfärdighet menar jag, som af trone kommer.
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 Men Israel, som for efter rättfärdighetenes lag, kom icke till rättfärdighetenes lag.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 Hvarföre? Derföre att de icke sökte det af trone, utan såsom af lagsens gerningar; ty de stötte sig på förtörnelsestenen;
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 Såsom skrifvet är: Si, jag lägger i Zion en förtörnelsesten, och ena förargelseklippo: och hvar och en som tror på honom, skall icke komma på skam.
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Romarbrevet 9 >