< 2 Mosebok 36 >

1 Då arbetade Bezaleel och Aholiab, och alle vise män, de som Herren hade gifvit vishet och förstånd till att veta, huru de allahanda verk göra skulle, till den tjenst, som helgedomen tillhörde, efter allt det som Herren budit hade.
Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
2 Och Mose kallade Bezaleel och Aholiab, och alla visa män, dem Herren hade gifvit vishet i deras hjerta; nämliga alla de som välviljeliga tillbödo sig, och gingo dertill, till att arbeta på verket.
Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
3 Och de togo till sig af Mose alla häfningar, som Israels barn frambåro, till den tjenst, som helgedomen tillkrafde, att det skulle blifva gjordt; ty de båro hvar morgon deras viljoga hjelp till honom.
Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
4 Då kommo alle de vise, som arbetade på helgedomens verk, hvar och en af sitt verk, som de gjorde;
Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
5 Och sade till Mose: Folket bär allt för mycket till, mer än till denna tjenstenes verk behöfves, som Herren budit hafver att göra.
wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
6 Då böd Mose, att utropas skulle i lägren: Ingen gifve mer till helgedomens häfning. Så vände folket igen att frambära.
Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
7 Ty der var allaredo nog till allahanda verk, som görandes var, och ändå utöfver.
kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
8 Och så gjorde alle vise män ibland arbetarena på verket, tabernaklet, tio tapeter, af hvitt tvinnadt silke, gult silke, skarlakan, rosenrödt, Cherubim konsteliga.
Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
9 Längden af hvart tapetet var åtta och tjugu alnar, och bredden fyra alnar, och de voro all vid ena måtto.
Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
10 Och han häktade tillhopa ju fem tapeter, det ena vid det andra;
Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
11 Och gjorde gula lyckor på hvart tapetens stad, der de vordo tillhopafogde;
Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
12 Ju femtio lyckor på hvart tapetet, der det ena det andra med fattade;
Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
13 Och gjorde femtio gyldene häkte, och tillhopafogade det ena tapetet med det andra med häkten; så att det vardt ett tabernakel.
Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
14 Och han gjorde ellofva tapeter af getahår till öfvertäckelse öfver tabernaklet;
Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
15 Tretio alnar lång, och fyra alnar bred; all vid ena måtto;
Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
16 Och fogde fem af dem tillhopa på en del;
Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
17 Och sex tillhopa på den andra delen; och gjorde ju femtio lyckor på hvart tapetet vid stadet, dermed de vordo tillsammanknäppte;
Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
18 Och gjorde ju femtio kopparhäkte, der samma tapeter med tillhopafogdes;
Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
19 Och gjorde ett täckelse öfver detta täckelset af rödlett vädurskinn; och öfver det ännu ett täckelse af tackskinn;
Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
20 Och gjorde bräder till tabernaklet af furoträ, som stå skulle;
Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
21 Hvartdera tio alnar långt, och halfannor aln bredt;
Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
22 Och uppå hvartdera två nåckor, der de med vordo tillhopasatte; så gjorde han all bräden till tabernaklet,
zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
23 Att tjugu af dem stodo på södra sidone;
Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
24 Och gjorde fyratio silfverfötter derunder; under hvart brädet två fötter, till två sina nåckor.
na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
25 På den andra sidone af tabernaklet, som var nordantill, gjorde han ock tjugu bräder,
Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
26 Med fyratio silfverfötter; under hvart brädet två fötter.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
27 Men bak i tabernaklet på vestra sidone gjorde han sex bräder;
Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
28 Och tu annor på de tu hörnen af tabernaklet baktill;
na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
29 Så att hvartdera af de båda parade sig med sitt hörnebräde ifrå nedan uppåt, och kommo tillhopa ofvantill med en krampo;
Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
30 Så att bräden vordo åtta, och silfverfötterna sexton; under hvart två fötter.
Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
31 Och gjorde han skottstänger af furoträ; fem till bräden på den ena sidone af tabernaklet;
Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
32 Och fem på den andra sidone; och fem bak vestantill;
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
33 Och gjorde skottstångena, så att hon öfver bräden allt bortåt skjuten vardt, ifrå den ena ändan till den andra;
Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
34 Och öfverdrog bräden med guld. Men deras ringar gjorde han af guld till skottstängerna, och öfverdrog stängerna med guld;
Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
35 Och gjorde Cherubim på förlåten konsteliga af gult silke, skarlakan, rosenrödt, och hvitt tvinnadt silke;
Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
36 Och gjorde till den samma fyra stolpar af furoträ, och öfverdrog dem med guld, och deras knappar af guld, och göt dertill fyra silfverfötter;
Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
37 Och gjorde ett kläde uti tabernaklets dörr, stickadt af gult silke, skarlakan, rosenrödt, och hvitt tvinnadt silke;
Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
38 Och fem stolpar dertill med deras knappar, och öfverdrog deras knappar och gjordar med guld; och fem kopparfötter dertill.
Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.

< 2 Mosebok 36 >