< Warumi 14 >

1 Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
But the man who is weak in the faith, do not receive for arguments of opinions.
2 Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
One man has faith to eat all things, but he who is weak eats vegetables.
3 Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
The man who eats should not disdain the man who does not eat, and the man who does not eat should not criticize the man who eats, for God has received him.
4 Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
Who are thou who criticizes the servant of another? To his own lord he stands or falls. And he will be made to stand, for God is able to make him stand.
5 Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
One man prefers one day above another, another man prefers every day. Let each man be fully persuaded in his own mind.
6 Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
He who regards the day, regards it for the Lord. And he who does not regard the day, for the Lord he does not regard it. And he who eats, eats for the Lord, for he expresses thanks to God. And he who does not eat, for the Lord he does not eat, and expresses thanks to God.
7 Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
For none of us lives to himself, and no man dies to himself.
8 maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
For both if we live, we live for the Lord, and if we die, we die for the Lord. Both if we live and if we die, therefore, we are the Lord's.
9 Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
For because of this Christ both died and arose, and he became alive so that he might be Lord over both the dead and the living.
10 Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
But why do thou criticize thy brother? Or also why do thou disdain thy brother? For we will all stand before the judgment seat of Christ.
11 Maana Maandiko yanasema: “Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”
For it is written, I live, says the Lord, that every knee will bow to me, and every tongue will confess to God.
12 Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
So then each of us will give account about himself to God.
13 Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
Let us not therefore criticize each other any more, but judge ye this instead, not to place a stumbling block to the brother, or a snare.
14 Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
I know and am persuaded in the Lord Jesus, that nothing is profane by itself, except to him who regards anything to be profane. To that man it is profane.
15 Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
For if thy brother is distressed because of food, thou no longer walk according to love. Do not destroy with thy food that man for whom Christ died.
16 Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
Therefore do not let your good be maligned.
17 Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
For the kingdom of God is not eating and drinking, but righteousness and peace and joy in the Holy Spirit.
18 Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
For he who serves Christ in these things is acceptable to God, and approved by men.
19 Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
So then we should pursue the things of peace, and the things of constructiveness for each other.
20 Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
Do not tear down the work of God because of food. All things indeed are clean, but it is wrong to the man who eats through hindrance.
21 Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
It is good not to eat meats, nor to drink wine, nor in whatever thy brother stumbles against, or is caused to stumble, or becomes weak.
22 Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
The faith thou have, have in relation to thyself before God. Blessed is the man not condemning himself in what he allows.
23 Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.
But he who doubts is condemned if he eats, because it is not from faith, and everything that is not from faith is sin.

< Warumi 14 >