< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
Por lo tanto, os exhorto, hermanos, por la misericordia de Dios, a que presentéis vuestros cuerpos en sacrificio vivo, santo, agradable a Dios, que es vuestro servicio espiritual.
2 Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu. (aiōn g165)
No os conforméis a este mundo, sino transformaos mediante la renovación de vuestra mente, para que podáis comprobar cuál es la buena, agradable y perfecta voluntad de Dios. (aiōn g165)
3 Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
Pues digo, por la gracia que me ha sido dada, a todos los que están entre vosotros, que no tengan más alto concepto de sí mismos que el que deben tener, sino que piensen razonablemente, según la medida de fe que Dios ha repartido a cada uno.
4 Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
Porque así como tenemos muchos miembros en un solo cuerpo, y no todos los miembros tienen la misma función,
5 Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
así nosotros, que somos muchos, somos un solo cuerpo en Cristo, y cada uno es miembro del otro,
6 Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
teniendo dones diferentes según la gracia que nos fue dada: si de profecía, profeticemos según la proporción de nuestra fe;
7 Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
o de servicio, entreguémonos al servicio; o el que enseña, a su enseñanza;
8 Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
o el que exhorta, a su exhortación; el que da, que lo haga con generosidad; el que gobierna, con diligencia; el que hace misericordia, con alegría.
9 Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
Que el amor sea sin hipocresía. Aborrece lo que es malo. Aferraos a lo que es bueno.
10 Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
En el amor a los hermanos, sed tiernos los unos con los otros; en la honra, preferíos los unos a los otros,
11 Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
no dejéis de ser diligentes, fervientes en el espíritu, sirviendo al Señor,
12 Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
alegrándoos en la esperanza, soportando en las tribulaciones, perseverando en la oración,
13 Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
contribuyendo a las necesidades de los santos, y dados a la hospitalidad.
14 Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
Bendice a los que te persiguen; bendice y no maldigas.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Alegraos con los que se alegran. Llorad con los que lloran.
16 Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
Tened los mismos sentimientos los unos hacia los otros. No sean altivos en su pensar, sino asociaros con los humildes. No seáis sabios en vuestras propias ideas.
17 Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
No paguéis a nadie mal por mal. Respetad lo que es honorable a los ojos de todos los hombres.
18 Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
Si es posible, en la medida en que dependa de vosotros, estad en paz con todos los hombres.
19 Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana.”
No busquéis la venganza vosotros mismos, amados, sino dad lugar a la ira de Dios. Porque está escrito: “La venganza me pertenece; yo pagaré, dice el Señor”.
20 Tena, Maandiko yasema: “Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Por eso “Si tu enemigo tiene hambre, aliméntalo. Si tiene sed, dale de beber; porque al hacerlo, amontonarás carbones de fuego sobre su cabeza”.
21 Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
No te dejes vencer por el mal, sino vence el mal con el bien.

< Warumi 12 >