< Ufunuo 1 >

1 Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
The Revelation of Jesus Christ that God gave him to show his bondmen what must happen quickly. And he signified it, having sent by his agent to his bondman John
2 naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
who testified the word of God and the testimony of Jesus Christ, as many things as he saw.
3 Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
Blessed is he who reads, and those who hear the words of the prophecy, and who keep the things written in it, for the time is near.
4 Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
John, to the seven congregations in Asia: Grace to you and peace from God, who is and who was and who is coming, and from the seven Spirits that are before his throne,
5 na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
and from Jesus Christ, the faithful witness, the firstborn of the dead, and the ruler of the kings of the earth. To him who loves us and washed us from our sins by his blood
6 akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
and made us a kingdom, priests to his God and Father, to him is the glory and the dominion into the ages of the ages. Truly. (aiōn g165)
7 Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
Behold, he comes with the clouds and every eye will see him, even the men who pierced him. And all the tribes of the earth will wail against him. Yea, Truly.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
I am the Alpha and the Omega, says the Lord, the God who is and who was and who is coming, the Almighty.
9 Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
I John, your brother and companion in the tribulation and kingdom and perseverance in Christ Jesus, happened to be on the isle that is called Patmos because of the word of God, and because of the testimony of Jesus Christ.
10 Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
I became in spirit on the Lord's day and I heard behind me a great voice like a trumpet
11 Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
saying, What thou see, write in a book and send to the seven congregations: to Ephesus, and to Smyrna, and to Pergamos, and to Thyatira, and to Sardis, and to Philadelphia, and to Laodicea.
12 Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
And I turned there to see the voice that spoke with me. And having turned I saw seven golden lampstands.
13 na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
And in the midst of the seven lampstands, resembling a son of man, he who was clothed down to the foot, and girded about with a golden belt at the breasts.
14 Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
And his head and hair were white as wool, white as snow, and his eyes as a flame of fire,
15 miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
and his feet resembling highly refined metal, as in a furnace having been fiery hot, and his voice as the sound of many waters,
16 Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
and having in his right hand seven stars, and a sharp two-edged sword coming out of his mouth. And the sight of him was as the sun shines in its strength.
17 Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
And when I saw him, I fell at his feet as dead. And he laid his right hand upon me, saying, Fear not, I am the first and the last,
18 Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
and he who lives. And I became dead, and behold, I am living into the ages of the ages. Truly. And I have the keys of death and of Hades. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
Therefore write the things that thou saw, and things that are, and things that are going to happen after these things.
20 Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.
The mystery of the seven stars that thou saw in my right hand, and the seven golden lampstands: the seven stars are agents of the seven congregations, and the seven lampstands that thou saw are the seven congregations.

< Ufunuo 1 >