< Ufunuo 8 >

1 Na Mwanakondoo alipouvunja mhuri wa saba, kukawa kimya mbinguni kwa muda wa nusu saa.
And when he opened the seventh seal, silence occurred in heaven, like half an hour.
2 Kisha nikawaona wale malaika saba wanaosimama mbele ya Mungu wamepewa tarumbeta saba.
And I saw the seven agents who stand before God, and seven trumpets were given to them.
3 Malaika mwingine akafika, akiwa anachukua chetezo cha dhahabu, akasimama mbele ya madhabahu ya kufukizia ubani. Naye akapewa ubani mwingi autoe sadaka pamoja na sala za watu wote wa Mungu, juu ya madhabahu ya dhahabu iliyo mbele ya kiti cha enzi.
And another agent came and stood at the altar, having a golden censer. And much incense was given to him, so that he would give with the prayers of all the sanctified upon the golden altar before the throne.
4 Moshi wa ubani ukapanda juu, pamoja na sala za watu wa Mungu, kutoka mikononi mwake huyo malaika aliyekuwa mbele ya Mungu.
And the vapor of the incense, with the prayers of the sanctified, ascended before God out of the agent's hand.
5 Kisha malaika akakichukua hicho chetezo, akakijaza moto wa madhabahuni akakitupa duniani. Kukawa na ngurumo, sauti, umeme na tetemeko la ardhi.
And the agent who took the censer, also filled it from the fire of the altar, and cast it to the earth. And there occurred thunders, and voices, and lightnings, and an earthquake.
6 Kisha wale malaika saba wenye tarumbeta saba wakajiweka tayari kupiga mbiu ya mgambo.
And the seven agents who have the seven trumpets prepared themselves so that they might sound.
7 Malaika wa kwanza akapiga tarumbeta yake. Mchanganyiko wa mvua ya mawe na moto, pamoja na damu, ukamwagwa juu ya nchi. Theluthi moja ya nchi ikaungua, theluthi moja ya miti ikaungua, na majani yote mabichi yakaungua.
And the first sounded, and there occurred hail and fire mingled with blood, and they were cast upon the earth. And the third part of the earth was burnt up, and the third part of the trees was burnt up, and all green grass was burnt up.
8 Malaika wa pili akapiga tarumbeta yake. Na kitu kama mlima mkubwa unaowaka moto ukatupwa baharini. Theluthi moja ya bahari ikawa damu,
And the second agent sounded, and something like a great burning mountain was cast into the sea. And the third part of the sea became blood,
9 theluthi moja ya viumbe vya baharini vikafa na theluthi moja ya meli zikaharibiwa.
and the third part of the creatures in the sea (those having lives) died, and the third part of the ships was destroyed.
10 Kisha malaika wa tatu akapiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa ikiwaka kama bonge la moto, ikaanguka kutoka mbinguni, na kutua juu ya theluthi moja ya mito na chemchemi za maji.
And the third agent sounded, and a great star fell from the heaven burning like a torch, and it fell upon the third part of the rivers, and upon the springs of the waters.
11 (Nyota hiyo inaitwa “Uchungu.”) Basi, theluthi moja ya maji yakawa machungu; watu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.
And the name of the star is called Wormwood oil. And the third part of the waters developed into wormwood oil, and many of the men died from the waters, because they were made bitter.
12 Kisha malaika wa nne akapiga tarumbeta yake. Ndipo theluthi moja ya jua, ya mwezi na ya nyota ikapata pigo; hata mwangaza ukapoteza theluthi moja ya mng'ao wake. Theluthi moja ya mchana ikakosa mwanga, hali kadhalika na theluthi moja ya usiku.
And the fourth agent sounded, and the third part of the sun was struck, and the third part of the moon, and the third part of the stars, so that the third part of them would be darkened. And the day did not shine the third part of it, and likewise the night.
13 Kisha nikatazama, nikasikia tai akiruka juu kabisa angani anasema kwa sauti kubwa, “Ole, ole, ole kwa wanaoishi duniani wakati malaika watatu waliobaki watakapopiga tarumbeta zao!”
And I looked, and I heard one eagle flying in mid-heaven, saying in a great voice, Woe, woe, woe, to those who dwell on the earth from the remaining sounds of the trumpet of the three agents who are going to sound.

< Ufunuo 8 >