< Ufunuo 3 >

1 “Kwa malaika wa kanisa la Sarde andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye na roho saba za Mungu na nyota saba. Nayajua mambo yako yote; najua unajulikana kuwa na uhai kumbe umekufa!
And to the agent of the congregation in Sardis write, These things says he who has the seven Spirits of God, and the seven stars: I know thy works, that thou have a name that thou live, and thou are dead.
2 Amka! Imarisha chochote chema kilichokubakia kabla nacho hakijatoweka kabisa. Maana, mpaka sasa, sijayaona matendo yako kuwa ni makamilifu mbele ya Mungu wangu.
Become thou watchful, and strengthen the remaining things that thou were going to throw away, for I have not found thy works made complete before my God.
3 Kumbuka, basi, yale uliyofundishwa na jinsi ulivyoyasikia, uyatii na ubadili nia yako mbaya. Usipokesha nitakujia ghafla kama mwizi, na wala hutaijua saa nitakapokujia.
Remember therefore how thou have received and heard, and be on guard, and repent. If therefore thou will not watch, I will come upon thee as a thief, and thou will, no, not know what hour I will come upon thee.
4 Lakini wako wachache huko Sarde ambao hawakuyachafua mavazi yao. Hao wanastahili kutembea pamoja nami wakiwa wamevaa mavazi meupe.
But thou have a few names in Sardis who did not defile their garments. And they will walk with me in white, because they are worthy.
5 “Wale wanaoshinda, watavikwa mavazi meupe kama hao. Nami sitayafuta majina yao kutoka katika kitabu cha uzima; tena nitawakiri kwamba ni wangu mbele ya Baba yangu na mbele ya malaika wake.
He who overcomes, this man will be clothed in white garments, and I will, no, not erase his name out of the book of life. And I will acknowledge his name before my Father, and before his agents.
6 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
He who has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ule ufunguo wa Daudi, na ambaye hufungua na hakuna mtu awezaye kufungua.
And to the agent of the congregation in Philadelphia write, These things says the Holy, the True, he who has the key of David, who opens, and none will shut it except he who opens, and none will open:
8 Nayajua mambo yako yote! Sasa, nimefungua mbele yako mlango ambao hakuna mtu awezaye kuufunga; najua kwamba ingawa huna nguvu sana, hata hivyo, umezishika amri zangu, umelitii neno langu wala hukulikana jina langu.
I know thy works. Behold, I have given before thee an opened door that none is able to shut it, because thou have little power, and thou keep my word, and did not deny my name.
9 Sikiliza! Nitawapeleka kwako watu wa kundi lake Shetani, watu ambao hujisema kuwa ni Wayahudi, kumbe ni wadanganyifu. Naam, nitawapeleka kwako na kuwafanya wapige magoti mbele yako wapate kujua kwamba kweli nakupenda wewe.
Behold, I give of the synagogue of Satan, those who say themselves to be Jews, and are not, but lie, behold, I will make them so that they will come and bow down before thy feet, and may know that I have loved thee.
10 Kwa kuwa wewe umezingatia agizo langu la kuwa na uvumilivu, nami pia nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima kuwajaribu wote wanaoishi duniani.
Because thou keep the word of my perseverance, I also will keep thee from the hour of trial that is going to come upon the whole inhabited world, to try those who dwell upon the earth.
11 Naja kwako upesi! Linda, basi, ulicho nacho sasa, ili usije ukanyang'anywa na mtu yeyote taji yako ya ushindi.
I come quickly, hold firm what thou have, so that none may take thy crown.
12 “Wale wanaoshinda nitawafanya wawe minara katika Hekalu la Mungu wangu, na hawatatoka humo kamwe. Pia nitaandika juu yao jina la Mungu wangu na jina la mji wa Mungu wangu, yaani Yerusalemu mpya, mji ambao utashuka kutoka juu mbinguni kwa Mungu wangu. Tena nitaandika juu yao jina langu jipya.
He who overcomes, I will make him a pillar in the temple of my God, and he will, no, not go out any more. And I will write upon him the name of my God, and the name of the city of my God, the new Jerusalem (it comes down out of the heaven from my God), and my new name.
13 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
He who has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikea andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aitwaye Amina. Yeye ni shahidi mwaminifu na wa kweli, ambaye ni chanzo cha viumbe vyote alivyoumba Mungu.
And to the agent of the congregation in Laodicea write, These things says the Truly, the faithful and true witness, the primacy of the creation of God:
15 Nayajua mambo yako yote! Najua kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungekuwa kimojawapo: baridi au moto.
I know thy works, that thou are neither cold nor hot. O that thou were cold or hot.
16 Basi, kwa kuwa hali yako ni vuguvugu, si baridi wala si moto, nitakutapika!
So because thou are lukewarm, and neither hot nor cold, I am going to spew thee out of my mouth.
17 Wewe unajisema, Mimi ni tajiri; ninajitosheleza, sina haja ya kitu chochote. Kumbe, hujui kwamba wewe ni mnyonge, unahitaji kuhurumiwa, maskini, kipofu tena uko uchi!
Because thou say, I am rich, and have become wealthy, and have need of nothing, and do not know that thou are wretched and miserable and poor and blind and naked.
18 Nakushauri ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto upate kuwa tajiri kweli. Tena afadhali ununue pia vazi jeupe, uvae na kufunika aibu ya uchi wako. Nunua pia mafuta ukapake machoni pako upate kuona.
I counsel thee to buy from me gold refined from fire, so that thou may become wealthy, and white garments, so that thou may clothe thyself, and the shame of thy nakedness may not be made known, and eye-salve, so that thou may anoint thine eyes, so that thou may see.
19 Mimi ndiye mwenye kumwonya na kumrudi yeyote ninayempenda. Kwa hiyo kaza moyo, achana na dhambi zako.
As many as I love, I rebuke and chasten. Be zealous therefore, and repent.
20 Sikiliza! Mimi nasimama mlangoni na kubisha hodi. Mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia nyumbani kwake na kula chakula pamoja naye, naye atakula pamoja nami.
Behold, I stand at the door and knock. If any man hears my voice and opens the door, I will come in to him, and will dine with him, and he with me.
21 “Wale wanaoshinda nitawaketisha pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi mwenyewe nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
He who overcomes, I will give him to sit with me in my throne, as I also overcame, and sat down with my Father in his throne.
22 “Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!”
He who has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.

< Ufunuo 3 >