< Ufunuo 15 >

1 Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
And I saw another sign in heaven, great and marvelous: seven agents having seven plagues, the last, because in them the wrath of God is ended.
2 Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
And I saw like a glassy sea mingled with fire, and those who were victorious over the beast and over its image and over the number of its name, standing on the glassy sea, having harps of God.
3 Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: “Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
And they sing the song of Moses the bondman of God, and the song of the Lamb, saying, Great and marvelous are thy works, Lord God Almighty, righteous and true are thy ways, thou King of the nations.
4 Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote.”
Who will, no, not fear thee, O Lord, and glorify thy name, because thou alone are holy? Because all the nations will come and worship before thee, because thy righteous deeds were made known.
5 Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
And after these things I looked, and the temple of the tabernacle of the testimony in heaven was opened.
6 Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
And the seven agents came forth from the temple having the seven plagues, who were clothed in pure bright linen, and golden belts girded around their breasts.
7 Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele. (aiōn g165)
And one of the four living creatures gave to the seven agents seven golden bowls containing the wrath of God who lives into the ages of the ages. (aiōn g165)
8 Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.
And the temple became full of vapor from the glory of God and from his power. And none was able to enter into the temple until the seven plagues of the seven agents were ended.

< Ufunuo 15 >