< Ufunuo 10 >

1 Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu, na upinde wa mvua kichwani mwake. Uso wake ulikuwa kama jua, na miguu yake ilikuwa kama moto.
And I saw a mighty agent coming down out of heaven, clothed with a cloud, and the rainbow was upon his head, and his face was like the sun, and his feet like pillars of fire,
2 Mikononi mwake alishika kitabu kidogo kimefunguliwa. Aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari, na wa kushoto juu ya nchi kavu,
and having in his hand an opened book. And he placed his right foot upon the sea, and the left upon the earth.
3 na kuita kwa sauti kubwa kama ya mngurumo wa simba. Alipopaaza sauti, ngurumo saba ziliitikia kwa kishindo.
And he cried out in a great voice as a lion roars. And when he cried out, the seven thunders uttered their voices.
4 Na hizo ngurumo saba ziliposema, mimi nikataka kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni: “Maneno ya ngurumo hizo saba ni siri; usiyaandike!”
And when the seven thunders uttered, I was going to write. And I heard a voice from heaven saying, Seal up what the seven thunders uttered, and do not write them.
5 Kisha yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu akainua mkono wake wa kulia juu mbinguni,
And the agent whom I saw standing upon the sea and upon the earth raised his right hand to heaven,
6 akaapa kwa jina la Mungu aishiye milele na milele, Mungu aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, bahari na vyote vilivyomo, dunia na vyote vilivyomo. Akasema, “Wakati wa kusubiri zaidi umekwisha! (aiōn g165)
and swore by him who lives into the ages of the ages, who created the heaven and the things in it, and the earth and the things in it, and the sea and the things in it, that time would be no more. (aiōn g165)
7 Lakini wakati ule malaika wa saba atakapotoa sauti yake, wakati atakapopiga tarumbeta yake, Mungu atakamilisha mpango wake wa siri kama alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
But in the days of the voice of the seventh agent, when he is going to sound, even the mystery of God is finished, as he declared the good news to his bondmen the prophets.
8 Kisha ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni pale awali ikasema nami tena: “Nenda ukakichukue kile kitabu kilichofunguliwa, kilicho mkononi mwa malaika asimamaye juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
And the voice that I heard from heaven was again speaking with me, and saying, Go, take the little book that has been opened in the hand of the agent who stands upon the sea and upon the earth.
9 Basi, nikamwendea huyo malaika, nikamwambia anipe hicho kitabu kidogo. Naye akaniambia, “Kichukue, ukile; kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali, lakini tumboni kitakuwa kichungu!”
And I went to the agent, telling him to give me the little book. And he says to me, Take and eat it. And it will make thy belly bitter, but it will be sweet as honey in thy mouth.
10 Basi, nikakichukua kitabu hicho kidogo kutoka mkononi mwa huyo malaika, nikakila; nacho kilikuwa kitamu kinywani mwangu kama asali, lakini nilipokimeza kikawa kichungu tumboni mwangu.
And I took the book out of the agent's hand, and ate it. And it was sweet as honey in my mouth, and when I had eaten it, my belly was made bitter.
11 Kisha nikaambiwa, “Inakubidi tena kutangaza ujumbe wa Mungu kuhusu watu wengi, mataifa, watu wa lugha nyingi na wafalme!”
And he says to me, Thou must prophesy again against many peoples, and against nations and tongues and kings.

< Ufunuo 10 >