< Ufunuo 1 >

1 Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
Objawienie Jezusa Chrystusa, które dał mu Bóg, aby ukazać swoim sługom to, co ma się stać wkrótce, a [on to] ukazał i posłał przez swojego anioła swemu słudze Janowi;
2 naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
Który poświadczył słowo Boże i świadectwo Jezusa Chrystusa, i wszystko, co widział.
3 Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
Błogosławiony ten, kto czyta, i [ci], którzy słuchają słów tego proroctwa i zachowują to, co w nim jest napisane, bo czas jest bliski.
4 Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
Jan do siedmiu kościołów, które są w Azji. Łaska wam i pokój od tego, który jest i który był, i który ma przyjść, i od siedmiu Duchów, które są przed jego tronem;
5 na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
I od Jezusa Chrystusa, [który jest] wiernym świadkiem i pierworodnym z umarłych, i władcą królów ziemi. Temu, który nas umiłował i obmył nas z naszych grzechów swoją krwią;
6 akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
I uczynił nas królami i kapłanami dla Boga, swego Ojca, jemu chwała i moc na wieki wieków. Amen. (aiōn g165)
7 Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
Oto przychodzi z obłokami i ujrzy go wszelkie oko, także ci, którzy go przebili. I będą lamentować przed nim wszystkie plemiona ziemi. Tak, amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
Ja jestem Alfa i Omega, początek i koniec, mówi Pan, który jest i który był, i który ma przyjść, Wszechmogący.
9 Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
Ja, Jan, który też [jestem] waszym bratem i współuczestnikiem w ucisku i królestwie oraz w cierpliwości Jezusa Chrystusa, byłem na wyspie zwanej Patmos z powodu słowa Bożego i świadectwa Jezusa Chrystusa.
10 Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
Znalazłem się w zachwyceniu Ducha w dniu Pańskim i usłyszałem za sobą głos potężny jakby trąby;
11 Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
Który mówił: Ja jestem Alfa i Omega, pierwszy i ostatni. Co widzisz, napisz w księdze i poślij do siedmiu kościołów, które są w Azji: do Efezu, Smyrny, Pergamonu, Tiatyry, Sardes, Filadelfii i Laodycei.
12 Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
I odwróciłem się, aby zobaczyć, co to za głos mówił do mnie. A gdy się odwróciłem, zobaczyłem siedem złotych świeczników;
13 na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
A pośród tych siedmiu świeczników [kogoś] podobnego do Syna Człowieczego, ubranego w długą szatę i przepasanego na piersi złotym pasem.
14 Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
Jego głowa i włosy [były] białe jak biała wełna, jak śnieg, a jego oczy jak płomień ognia.
15 miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
Jego stopy podobne do mosiądzu, jakby w piecu rozżarzonego, a jego głos jak szum wielu wód.
16 Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
W swej prawej ręce miał siedem gwiazd, a z jego ust wychodził ostry miecz obosieczny. Jego oblicze [było] jak słońce, [gdy] świeci w [pełni] swej mocy.
17 Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
Gdy go zobaczyłem, padłem do jego stóp jak martwy i położył na mnie swą prawą rękę, mówiąc mi: Nie bój się! Ja jestem pierwszy i ostatni;
18 Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
I żyjący, a byłem umarły. A oto żyję na wieki wieków i mam klucze piekła i śmierci. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
Napisz to, co widziałeś, i co jest, i co ma się stać potem.
20 Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.
Tajemnica siedmiu gwiazd, które widziałeś w mojej prawej ręce i siedmiu złotych świeczników [jest taka]: siedem gwiazd to aniołowie siedmiu kościołów, a siedem świeczników, które widziałeś, to siedem kościołów.

< Ufunuo 1 >