< Filemoni 1 >

1 Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
Pablo, prisionero de Cristo Jesús, y Timoteo, nuestro hermano, a Filemón, nuestro amado colaborador,
2 na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
a la amada Apia, a Arquipo, nuestro compañero de armas, y a la asamblea en vuestra casa:
3 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
Gracia a vosotros y paz de parte de Dios nuestro Padre y del Señor Jesucristo.
4 Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
Doy gracias a mi Dios siempre, haciendo mención de vosotros en mis oraciones,
5 maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
oyendo hablar de tu amor y de la fe que tienes para con el Señor Jesús y para con todos los santos,
6 Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
para que la comunión de tu fe se haga efectiva en el conocimiento de todo lo bueno que hay en nosotros en Cristo Jesús.
7 Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
Porque tenemos mucha alegría y consuelo en tu amor, porque los corazones de los santos han sido refrescados por medio de ti, hermano.
8 Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
Por lo tanto, aunque tengo toda la audacia en Cristo para ordenaros lo que conviene,
9 Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
sin embargo, por amor, más bien apelo a vosotros, siendo uno como Pablo, anciano, pero también prisionero de Jesucristo.
10 Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
Apelo a vosotros por mi hijo Onésimo, del que me he convertido en padre en mis cadenas,
11 Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
que antes os era inútil, pero que ahora nos es útil a vosotros y a mí.
12 Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
Te lo devuelvo. Recibid, pues, a éste, es decir, a mi propio corazón,
13 Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
a quien deseaba retener conmigo, para que en vuestro nombre me sirviera en mis cadenas para la Buena Nueva.
14 Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
Pero no quise hacer nada sin tu consentimiento, para que tu bondad no fuera como por necesidad, sino por libre voluntad.
15 Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios g166)
Por lo tanto, tal vez se separó de ti por un tiempo para que lo tuvieras para siempre, (aiōnios g166)
16 Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
no ya como un esclavo, sino más que un esclavo, un hermano amado, especialmente para mí, pero cuánto más para ti, tanto en la carne como en el Señor.
17 Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
Si, pues, me consideras un socio, recíbelo como a mí.
18 Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
Pero si os ha perjudicado o os debe algo, ponedlo en mi cuenta.
19 Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
Yo, Pablo, escribo esto con mi propia mano: Te lo devolveré (sin mencionar que me debes incluso a ti mismo además).
20 Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
Sí, hermano, permíteme que me alegre de ti en el Señor. Refresca mi corazón en el Señor.
21 Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
Confiando en tu obediencia, te escribo, sabiendo que harás incluso más allá de lo que te digo.
22 Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
Prepara también una habitación de huéspedes para mí, pues espero que, gracias a vuestras oraciones, se me restituya.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
Os saluda Epafras, mi compañero de prisión en Cristo Jesús,
24 Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
así como Marcos, Aristarco, Demas y Lucas, mis compañeros de trabajo.
25 Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
La gracia de nuestro Señor Jesucristo esté con vuestro espíritu. Amén.

< Filemoni 1 >