< Mathayo 6 >

1 “Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
Be careful not to do your charity before men in order to be seen by them, otherwise ye have no reward from your Father in the heavens.
2 “Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
When therefore thou do charity, do not sound a trumpet before thee, as the hypocrites do in the synagogues and in the streets, so that they may have glory by men. Truly I say to you, they have their reward.
3 Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
But when thou do charity, let not thy left hand know what thy right hand does,
4 Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
so that thy charity may be in secret. And thy Father who sees in secret will himself reward thee in the open.
5 “Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
And when thou pray, thou shall not be as the hypocrites, because they love to pray having stood in the synagogues and in the corners of the thoroughfares, so that they may be seen by men. Truly I say to you, they have their reward.
6 Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
But thou, when thou pray, enter into thy private room, and having shut thy door, pray to thy Father in secret, and thy Father who sees in secret will reward thee in the open.
7 “Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
And while praying do not use vain repetitions as the heathen do, for they think that they will be heard by their much speaking.
8 Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
Be not therefore like them, for your Father knows what things ye have need of before ye ask him.
9 Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
Pray ye therefore this way: Our Father in the heavens, hallowed be thy name.
10 Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
May thy kingdom come. May thy will happen on the earth as also in heaven.
11 Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
Give us this day the bread sufficient for us.
12 Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
And forgive us our debts as we also forgive our debtors.
13 Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
And bring us not into temptation, but deliver us from evil, because from thee is the kingdom and the power and the glory into the ages. Truly.
14 “Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
For if ye forgive men their trespasses, your heavenly Father will also forgive you.
15 Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
But if ye forgive not men their trespasses, neither will your Father forgive your trespasses.
16 “Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
And when ye fast, become not like the gloomy looking hypocrites, for they make their faces unsightly, so that they may appear fasting to men. Truly I say to you, they have their reward.
17 Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
But when thou fast, anoint thy head, and wash thy face,
18 ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
so that thou may not appear fasting to men, but to thy Father in secret. And thy Father, who sees in secret, will reward thee.
19 “Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
Lay not up for yourselves treasures upon the earth, where moth and rust deteriorates, and where thieves break through and steal,
20 Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
but lay up for yourselves treasures in heaven, where neither moth nor rust deteriorates, and where thieves do not break through nor steal.
21 Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
For where your treasure is, there will your heart be also.
22 “Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
The light of the body is the eye. If therefore thine eye is sound, thy whole body will be bright.
23 Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
But if thine eye is bad, thy whole body will be dark. If therefore the light that is in thee is darkness, how great is the darkness!
24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
No man can serve two masters, for either he will hate the one, and love the other, or he will hold to one, and disparage the other. Ye cannot serve God and mammon.
25 “Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
Because of this I say to you, be not anxious about your life, what ye may eat, or what ye may drink, nor yet for your body, what ye may wear. Is not the life more than the food, and the body than the clothing?
26 Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
Look to the birds of the sky, because they sow not, nor do they reap, nor gather into barns, and your heavenly Father feeds them. Are ye not more valuable then they?
27 Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
And which man of you by being anxious can add one cubit to his life span?
28 “Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
And why are ye anxious about clothing? Consider the lilies of the field, how they grow. They toil not, nor do they spin,
29 Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
yet I say to you, that not even Solomon in all his glory was arrayed like one of these.
30 Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
And if God so clothes the grass of the field, which today is, and tomorrow is cast into an oven, will he not much more you, O ye of little faith?
31 “Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
Be not therefore anxious, saying, What may we eat? or, What may we drink? or, What may we wear?
32 Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
For the Gentiles seek after all these things, for your heavenly Father knows that ye need all these things.
33 Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
But seek ye first the kingdom of God and his righteousness, and all these things will be added to you.
34 Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.
Be not therefore anxious for the morrow, for the morrow will be anxious about things of itself. Sufficient for the day is the evil of it.

< Mathayo 6 >