< Mathayo 27 >

1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
Al amanecer, todos los jefes de los sacerdotes y los ancianos del pueblo se pusieron de acuerdo contra Jesús para matarlo.
2 Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
Lo ataron, lo llevaron y lo entregaron a Poncio Pilato, el gobernador.
3 Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
Entonces Judas, el que lo traicionó, al ver que Jesús era condenado, sintió remordimiento y devolvió las treinta monedas de plata a los sumos sacerdotes y a los ancianos,
4 Akawaambia, “Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe.” Lakini wao wakasema, “Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako.”
diciendo: “He pecado al entregar sangre inocente.” Pero ellos dijeron: “¿Qué es eso para nosotros? Vosotros os ocupáis de ello”.
5 Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
Arrojó las piezas de plata en el santuario y se marchó. Luego se fue y se ahorcó.
6 Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, “Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu.”
Los jefes de los sacerdotes tomaron las piezas de plata y dijeron: “No es lícito ponerlas en el tesoro, pues es el precio de la sangre.”
7 Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
Se asesoraron y compraron con ellas el campo del alfarero para enterrar a los extranjeros.
8 Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
Por eso ese campo ha sido llamado “El campo de la sangre” hasta el día de hoy.
9 Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: “Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
Entonces se cumplió lo que se había dicho por medio del profeta Jeremías, que decía “Tomaron las treinta piezas de plata, el precio de aquel sobre el que se había fijado un precio, al que algunos de los hijos de Israel le dieron precio,
10 wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.”
y los dieron para el campo del alfarero, como el Señor me ordenó”.
11 Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, “Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamwambia, “Wewe umesema.”
Jesús se presentó ante el gobernador y éste le preguntó: “¿Eres tú el rey de los judíos?” Jesús le dijo: “Tú lo dices”.
12 Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
Cuando fue acusado por los sumos sacerdotes y los ancianos, no respondió nada.
13 Hivyo Pilato akamwuliza, “Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?”
Entonces Pilato le dijo: “¿No oyes cuántas cosas declaran contra ti?”.
14 Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
No le respondió, ni siquiera una palabra, de modo que el gobernador se maravilló mucho.
15 Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
En la fiesta, el gobernador acostumbraba a liberar a la multitud un prisionero que ellos deseaban.
16 Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
Tenían entonces un preso notable llamado Barrabás.
17 Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, “Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?”
Así pues, cuando se reunieron, Pilato les dijo: “¿A quién queréis que os suelte? ¿A Barrabás, o a Jesús, que se llama Cristo?”
18 Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
Porque sabía que por envidia le habían entregado.
19 Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: “Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
Mientras estaba sentado en el tribunal, su mujer le mandó decir: “No tengas nada que ver con ese justo, porque hoy he sufrido muchas cosas en sueños por su culpa.”
20 Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
Los jefes de los sacerdotes y los ancianos persuadieron a las multitudes para que pidieran a Barrabás y destruyeran a Jesús.
21 Mkuu wa mkoa akawauliza, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?” Wakamjibu, “Baraba!”
Pero el gobernador les respondió: “¿A cuál de los dos queréis que os suelte?” Dijeron: “¡Barabbas!”
22 Pilato akawauliza, “Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?” Wote wakasema, “Asulubiwe!”
Pilato les dijo: “¿Qué haré, pues, a Jesús, que se llama Cristo?” Todos le decían: “¡Que lo crucifiquen!”
23 Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wao wakazidi kupaaza sauti: “Asulubiwe!”
Pero el gobernador dijo: “¿Por qué? ¿Qué mal ha hecho?” Pero ellos gritaban mucho, diciendo: “¡Que lo crucifiquen!”.
24 Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe.”
Al ver Pilato que no se ganaba nada, sino que se iniciaba un alboroto, tomó agua y se lavó las manos ante la multitud, diciendo: “Yo soy inocente de la sangre de este justo. Vosotros os encargáis de ello”.
25 Watu wote wakasema, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
Todo el pueblo respondió: “¡Que su sangre sea sobre nosotros y sobre nuestros hijos!”
26 Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
Entonces les soltó a Barrabás, pero a Jesús lo azotó y lo entregó para que lo crucificaran.
27 Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Entonces los soldados del gobernador llevaron a Jesús al pretorio y reunieron a toda la guarnición contra él.
28 Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
Lo desnudaron y le pusieron un manto escarlata.
29 Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”
Trenzaron una corona de espinas y se la pusieron en la cabeza, y una caña en la mano derecha; se arrodillaron ante él y se burlaron, diciendo: “¡Salve, Rey de los judíos!”
30 Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
Le escupían, tomaban la caña y le golpeaban en la cabeza.
31 Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
Después de burlarse de él, le quitaron el manto, le pusieron su ropa y lo llevaron a crucificar.
32 Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
Al salir, encontraron a un hombre de Cirene, de nombre Simón, y le obligaron a ir con ellos para que llevara su cruz.
33 Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la kichwa,”
Cuando llegaron a un lugar llamado “Gólgota”, es decir, “El lugar de la calavera”,
34 wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
le dieron a beber vino agrio mezclado con hiel. Cuando lo probó, no quiso beber.
35 Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
Cuando lo crucificaron, se repartieron su ropa echando suertes,
36 Wakaketi, wakawa wanamchunga.
y se sentaron a velarlo allí.
37 Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, “Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.”
Colocaron sobre su cabeza la acusación escrita: “ESTE ES JESÚS, EL REY DE LOS JUDÍOS”.
38 Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
Entonces había dos ladrones crucificados con él, uno a su derecha y otro a la izquierda.
39 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
Los que pasaban le blasfemaban, moviendo la cabeza
40 “Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!”
y diciendo: “Tú, que destruyes el templo y lo construyes en tres días, sálvate a ti mismo. Si eres el Hijo de Dios, baja de la cruz”.
41 Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
Asimismo, los jefes de los sacerdotes, burlándose con los escribas, los fariseos y los ancianos, decían:
42 “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
“Ha salvado a otros, pero no puede salvarse a sí mismo. Si es el Rey de Israel, que baje ahora de la cruz, y creeremos en él.
43 Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka.”
Él confía en Dios. Que Dios lo libere ahora, si lo quiere; porque ha dicho: “Yo soy el Hijo de Dios””.
44 Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
También los ladrones que estaban crucificados con él le lanzaron el mismo reproche.
45 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
Desde la hora sexta hubo oscuridad sobre toda la tierra hasta la hora novena.
46 Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eli, Eli, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Hacia la hora novena, Jesús gritó con gran voz, diciendo: “Elí, Elí, ¿lama sabactani?” Es decir, “Dios mío, Dios mío, ¿por qué me has abandonado?”
47 Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, “Anamwita Eliya.”
Algunos de los que estaban allí, al oírlo, dijeron: “Este hombre llama a Elías”.
48 Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
Inmediatamente, uno de ellos corrió y tomó una esponja, la llenó de vinagre, la puso en una caña y le dio de beber.
49 Wengine wakasema, “Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.”
Los demás dijeron: “Déjenlo. Vamos a ver si Elías viene a salvarlo”.
50 Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
Jesús volvió a gritar con fuerza y entregó su espíritu.
51 Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
He aquí que el velo del templo se rasgó en dos desde arriba hasta abajo. La tierra tembló y las rocas se partieron.
52 makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
Se abrieron los sepulcros y resucitaron muchos cuerpos de los santos que habían dormido;
53 nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
y saliendo de los sepulcros después de su resurrección, entraron en la ciudad santa y se aparecieron a muchos.
54 Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
El centurión y los que estaban con él observando a Jesús, al ver el terremoto y las cosas que se hacían, se espantaron, diciendo: “¡Verdaderamente éste era el Hijo de Dios!”
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
Estaban allí mirando desde lejos muchas mujeres que habían seguido a Jesús desde Galilea, sirviéndole.
56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
Entre ellas estaban María Magdalena, María la madre de Santiago y de José, y la madre de los hijos de Zebedeo.
57 Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
Cuando llegó la noche, vino un hombre rico de Arimatea llamado José, que también era discípulo de Jesús.
58 Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
Este hombre fue a Pilato y pidió el cuerpo de Jesús. Entonces Pilato ordenó que se entregara el cuerpo.
59 Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
José tomó el cuerpo, lo envolvió en una tela de lino limpia
60 akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
y lo puso en su propio sepulcro nuevo, que había excavado en la roca. Luego hizo rodar una gran piedra contra la puerta del sepulcro y se fue.
61 Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
María Magdalena estaba allí, y la otra María, sentadas frente al sepulcro.
62 Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
Al día siguiente, que era el día siguiente al de la preparación, se reunieron los jefes de los sacerdotes y los fariseos ante Pilato,
63 Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
diciendo: “Señor, nos acordamos de lo que dijo aquel engañador cuando aún vivía: ‘Después de tres días resucitaré’.
64 Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali.”
Manda, pues, que se asegure el sepulcro hasta el tercer día, no sea que vengan sus discípulos de noche y lo roben, y digan al pueblo: ‘Ha resucitado de entre los muertos’; y el último engaño será peor que el primero.”
65 Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”
Pilato les dijo: “Tenéis una guardia. Vayan y asegúrenlo todo lo que puedan”.
66 Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.
Así que fueron con la guardia y aseguraron el sepulcro, sellando la piedra.

< Mathayo 27 >