< Marko 1 >

1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the Good News of Jesus Christ, the Son of God.
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
As it is written in the prophets, “Behold, I send my messenger before your face, who will prepare your way before you:
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
the voice of one crying in the wilderness, ‘Make ready the way of the Lord! Make his paths straight!’”
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
John came baptizing in the wilderness and preaching the baptism of repentance for forgiveness of sins.
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
All the country of Judea and all those of Jerusalem went out to him. They were baptized by him in the Jordan river, confessing their sins.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
John was clothed with camel’s hair and a leather belt around his waist. He ate locusts and wild honey.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
He preached, saying, “After me comes he who is mightier than I, the thong of whose sandals I am not worthy to stoop down and loosen.
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I baptized you in water, but he will baptize you in the Holy Spirit.”
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
In those days, Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John in the Jordan.
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
Immediately coming up from the water, he saw the heavens parting and the Spirit descending on him like a dove.
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
A voice came out of the sky, “You are my beloved Son, in whom I am well pleased.”
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
Immediately the Spirit drove him out into the wilderness.
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
He was there in the wilderness forty days, tempted by Satan. He was with the wild animals; and the angels were serving him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
Now after John was taken into custody, Jesus came into Galilee, preaching the Good News of God’s Kingdom,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
and saying, “The time is fulfilled, and God’s Kingdom is at hand! Repent, and believe in the Good News.”
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
Passing along by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew, the brother of Simon, casting a net into the sea, for they were fishermen.
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
Jesus said to them, “Come after me, and I will make you into fishers for men.”
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
Immediately they left their nets, and followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
Going on a little further from there, he saw James the son of Zebedee, and John his brother, who were also in the boat mending the nets.
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
Immediately he called them, and they left their father, Zebedee, in the boat with the hired servants, and went after him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
They went into Capernaum, and immediately on the Sabbath day he entered into the synagogue and taught.
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
They were astonished at his teaching, for he taught them as having authority, and not as the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
Immediately there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he cried out,
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
saying, “Ha! What do we have to do with you, Jesus, you Nazarene? Have you come to destroy us? I know who you are: the Holy One of God!”
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
Jesus rebuked him, saying, “Be quiet, and come out of him!”
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
The unclean spirit, convulsing him and crying with a loud voice, came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
They were all amazed, so that they questioned among themselves, saying, “What is this? A new teaching? For with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him!”
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
The report of him went out immediately everywhere into all the region of Galilee and its surrounding area.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
Immediately, when they had come out of the synagogue, they came into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
Now Simon’s wife’s mother lay sick with a fever, and immediately they told him about her.
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
He came and took her by the hand and raised her up. The fever left her immediately, and she served them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
At evening, when the sun had set, they brought to him all who were sick and those who were possessed by demons.
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
All the city was gathered together at the door.
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
He healed many who were sick with various diseases and cast out many demons. He didn’t allow the demons to speak, because they knew him.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
Early in the morning, while it was still dark, he rose up and went out, and departed into a deserted place, and prayed there.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
Simon and those who were with him searched for him.
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
They found him and told him, “Everyone is looking for you.”
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
He said to them, “Let’s go elsewhere into the next towns, that I may preach there also, because I came out for this reason.”
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
He went into their synagogues throughout all Galilee, preaching and casting out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
A leper came to him, begging him, kneeling down to him, and saying to him, “If you want to, you can make me clean.”
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
Being moved with compassion, he stretched out his hand, and touched him, and said to him, “I want to. Be made clean.”
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
When he had said this, immediately the leprosy departed from him and he was made clean.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
He strictly warned him and immediately sent him out,
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
and said to him, “See that you say nothing to anybody, but go show yourself to the priest and offer for your cleansing the things which Moses commanded, for a testimony to them.”
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
But he went out, and began to proclaim it much, and to spread about the matter, so that Jesus could no more openly enter into a city, but was outside in desert places. People came to him from everywhere.

< Marko 1 >