< Marko 3 >

1 Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
Jésus entra une autre fois dans la synagogue, et il y avait là un homme qui avait une main sèche.
2 Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
Et ils l'observaient, pour voir s'il le guérirait le jour du sabbat, afin de l'accuser.
3 Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, “Njoo hapa katikati.”
Alors il dit à l'homme qui avait la main sèche: Tiens-toi là au milieu.
4 Kisha, akawauliza, “Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao hawakusema neno.
Puis il leur dit: Est-il permis de faire du bien dans les jours de sabbat, ou de faire du mal? de sauver une personne, ou de la laisser périr? Et ils se turent.
5 Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, “Nyosha mkono wako!” Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
Alors, les regardant avec indignation, et étant affligé de l'endurcissement de leur cœur, il dit à cet homme: Étends ta main. Et il l'étendit, et sa main devint saine comme l'autre.
6 Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
Et les pharisiens étant sortis, tinrent aussitôt conseil avec les hérodiens contre lui, pour le faire périr.
7 Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
Alors Jésus se retira avec ses disciples vers la mer, et une grande multitude le suivait de la Galilée, de la Judée,
8 Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
De Jérusalem, de l'Idumée et d'au-delà du Jourdain. Et ceux des environs de Tyr et de Sidon, ayant entendu parler des grandes choses qu'il faisait, vinrent aussi vers lui en grand nombre.
9 Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
Et il dit à ses disciples qu'il y eût une petite barque toute prête auprès de lui, à cause de la multitude, de peur qu'elle ne le pressât trop.
10 Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
Car il en avait guéri plusieurs, de sorte que tous ceux qui avaient des maladies se jetaient sur lui pour le toucher.
11 Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, “Wewe ni Mwana wa Mungu!”
Et quand les esprits immondes le voyaient, ils se prosternaient devant lui et s'écriaient: Tu es le Fils de Dieu!
12 Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
Mais il leur défendait, avec menace, de le faire connaître.
13 Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
Il monta ensuite sur la montagne, et appela ceux qu'il jugea à propos, et ils vinrent à lui.
14 naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
Et il en établit douze pour être avec lui, pour les envoyer prêcher,
15 na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
Et pour avoir la puissance de guérir les malades et de chasser les démons.
16 Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
C'était Simon, auquel il donna le nom de Pierre;
17 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake “wanangurumo”),
Puis Jacques fils de Zébédée, et Jean frère de Jacques, auxquels il donna le nom de Boanerges, c'est-à-dire, enfants du tonnerre;
18 Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
Et André, Philippe, Barthélemi, Matthieu, Thomas, Jacques fils d'Alphée, Thaddée, Simon le Cananite,
19 Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
Et Judas l'Iscariote, qui fut celui qui le trahit.
20 Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
Puis ils retournèrent à la maison; et une multitude s'y assembla encore, de sorte qu'ils ne pouvaient pas même prendre leur repas.
21 Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
Ses parents l'ayant appris, sortirent pour le prendre; car on disait: Il est hors de sens.
22 Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, “Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo.”
Et les scribes qui étaient descendus de Jérusalem, disaient: Il est possédé de Béelzébul, et il chasse les démons par le prince des démons.
23 Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, “Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
Mais Jésus, les ayant appelés, leur dit par des similitudes: Comment Satan peut-il chasser Satan?
24 Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
Car si un royaume est divisé contre lui-même, ce royaume-là ne saurait subsister;
25 Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
Et si une maison est divisée contre elle-même, cette maison-là ne saurait subsister;
26 Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
De même, si Satan s'élève contre lui-même et est divisé, il ne peut subsister; mais il prend fin.
27 “Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
Personne ne peut entrer dans la maison d'un homme fort et piller son bien, s'il n'a auparavant lié cet homme fort; et alors il pillera sa maison.
28 “Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
Je vous dis en vérité, que toutes sortes de péchés seront pardonnés aux enfants des hommes, ainsi que les blasphèmes par lesquels ils auront blasphémé;
29 lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
Mais quiconque aura blasphémé contre le Saint-Esprit, n'en obtiendra jamais le pardon; mais il sera sujet à une condamnation éternelle. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 (Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”)
Jésus parla ainsi, parce qu'ils disaient: Il est possédé d'un esprit immonde.
31 Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
Ses frères et sa mère arrivèrent donc, et se tenant dehors ils l'envoyèrent appeler; et la multitude était assise autour de lui.
32 Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona.”
Et on lui dit: Voilà, ta mère et tes frères sont là dehors, qui te demandent.
33 Yesu akawaambia, “Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?”
Mais il répondit: Qui est ma mère, ou qui sont mes frères?
34 Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, “Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
Et jetant les yeux sur ceux qui étaient autour de lui, il dit: Voici ma mère et mes frères.
35 Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu.”
Car quiconque fera la volonté de Dieu, celui-là est mon frère, et ma sœur et ma mère.

< Marko 3 >