< Marko 2 >

1 Baada ya siku kadhaa, Yesu alirudi Kafarnaumu, watu wakapata habari kwamba alikuwa nyumbani.
And having again entered into Capernaum, after some days it was heard that he was in a house.
2 Basi, wakaja watu wengi sana hata nafasi yoyote ikakosekana mlangoni. Yesu alikuwa akiwahubiria ujumbe wake,
And straightaway many were gathered together, so as to accommodate no more, not even near the door. And he spoke the word to them.
3 wakati mtu mmoja aliyepooza alipoletwa kwake akiwa amechukuliwa na watu wanne.
And they come bringing to him a paralyzed man, being taken by four men.
4 Kwa sababu ya huo umati wa watu, hawakuweza kumpeleka karibu na Yesu. Basi, wakatoboa sehemu ya dari iliyokuwa juu ya mahali alipokuwa Yesu. Walipokwisha pata nafasi, wakamteremsha huyo mtu akiwa amelala juu ya mkeka.
And not being able to come near to him because of the crowd, they uncovered the roof where he was. And when they had broken through, they let down the bed on which the paralyzed man lay.
5 Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.”
And having seen their faith, Jesus says to the paralyzed man, Child, thy sins are forgiven thee.
6 Baadhi ya walimu wa Sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao,
But some of the scholars were sitting there, and deliberating in their hearts,
7 “Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake.”
Why does this man speak blasphemies this way. Who can forgive sins but one, God?
8 Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
And straightaway Jesus, having perceived in his spirit that they so deliberated within themselves, said to them, Why do ye deliberate these things in your hearts?
9 Ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia mtu huyu aliyepooza, Umesamehewa dhambi zako, au kumwambia, Inuka! Chukua mkeka wako utembee?
Which is easier, to say to the paralyzed man, Thy sins are forgiven thee, or to say, Arise, and take up thy bed and walk?
10 Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza,
But that ye may know that the Son of man has authority on earth to forgive sins (he says to the paralyzed man),
11 “Nakwambia simama, chukua mkeka wako uende nyumbani!”
I say to thee, Arise, and take up thy bed, and go to thy house.
12 Mara, watu wote wakiwa wanamtazama, huyo mtu akainuka, akauchukua mkeka wake, akaenda zake. Watu wote wakashangaa na kumtukuza Mungu wakisema, “Hatujapata kamwe kuona jambo kama hili.”
And straightaway he arose, and having taken up the bed, he went forth before them all, so as for all to be amazed, and to glorify God, saying, We never saw it like this.
13 Yesu alikwenda tena kando ya ziwa. Umati wa watu ukamwendea, naye akaanza kuwafundisha.
And he went forth again by the sea, and all the multitude resorted to him, and he taught them.
14 Alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Yesu akamwambia, “Nifuate!” Lawi akasimama, akamfuata.
And as he passed by he saw Levi the son of Alphaeus sitting at the tax office. And he says to him, Follow thou me. And having risen, he followed him.
15 Baadaye, Yesu alikuwa amekaa mezani, nyumbani kwa Lawi, kula chakula. Watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wamemfuata Yesu na wengi wao wakawa wamekaa mezani pamoja naye na wanafunzi wake.
And it came to pass, while he was dining in his house, that many tax collectors and sinners were dining with Jesus and his disciples, for there were many, and they followed him.
16 Basi, baadhi ya walimu wa Sheria ambao walikuwa Mafarisayo walipomwona Yesu akila pamoja na watu wenye dhambi na watoza ushuru, wakawauliza wanafunzi wake, “Kwa nini anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
And the scholars of the Pharisees, when they saw him eating with the tax collectors and sinners, they said to his disciples, Why is it that he eats and drinks with tax collectors and sinners?
17 Yesu alipowasikia, akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.”
And when Jesus heard it he says to them, Those who are strong have no need of a physician, but those faring badly. I came not to call the righteous, but sinners for repentance.
18 Wakati mmoja wanafunzi wa Yohane na wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wanafunga. Basi, watu wakaja, wakamwuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wa Yohane na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
And John's disciples and those of the Pharisees were fasting. And they come and say to him, Why do John's disciples and those of the Pharisees fast, but the disciples with you do not fast?
19 Yesu akajibu, “Walioalikwa harusini wanawezaje kufunga kama bwana harusi yupo pamoja nao? Wakati wote wawapo pamoja na bwana harusi hawawezi kufunga.
And Jesus said to them, The sons of the wedding hall cannot fast while the bridegroom is with them. As long as they have the bridegroom with them, they cannot fast.
20 Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
But the days will come when the bridegroom is taken away from them, and then they will they fast in those day.
21 “Hakuna mtu anayekata kiraka kutoka katika nguo mpya na kukishonea katika nguo kuukuu. Kama akifanya hivyo, hicho kiraka kipya kitararuka kutoka hilo vazi kuukuu, nalo litaharibika zaidi.
And no man sews a new patch of cloth on an old garment, otherwise the patch of it pulls away, the new from the old, and a tear becomes worse.
22 Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai itavipasua hivyo viriba, nayo divai pamoja na hivyo viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!”
And no man puts new wine into old wineskins, otherwise the new wine bursts the wineskins, and the wine is spilled, and the wineskins will be destroyed. But new wine must be put into fresh wineskins.
23 Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano. Walipokuwa wanatembea, wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano.
And it came to pass, that he was passing through the grain fields on the sabbath day, and his disciples began to make a path while plucking the ears.
24 Mafarisayo wakawaambia, “Tazama! Kwa nini wanafanya jambo ambalo si halali kufanya wakati wa Sabato?”
And the Pharisees said to him, Look, why are they doing what is not permitted on the sabbath day?
25 Yesu akawajibu, “Je, hamjapata kusoma juu ya kile alichofanya Daudi wakati alipohitaji chakula? Yeye pamoja na wenzake waliona njaa,
And he said to them, Did ye never read what David did when he had need, and was hungry, he and those with him?
26 naye akaingia ndani ya Nyumba ya Mungu, akala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Jambo hili lilifanyika wakati Abiathari alikuwa Kuhani Mkuu. Na ni makuhani tu peke yao waliokuwa wameruhusiwa kula mikate hiyo. Lakini Daudi aliila, tena akawapa na wenzake.”
How he entered into the house of God under Abiathar the high priest, and ate the loaves of the presentation, which is not permitted to eat except for the priests. And he also gave to those who were with him?
27 Basi, Yesu akawaambia, “Sabato iliwekwa kwa ajili ya binadamu na si binadamu kwa ajili ya Sabato!
And he said to them, The sabbath came into being for sake of man, and not man for sake of the sabbath.
28 Kwa hiyo, Mwana wa Mtu ni Bwana hata wa Sabato.”
So then the Son of man is lord even of the sabbath.

< Marko 2 >