< Marko 15 >

1 Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
Por la mañana, los jefes de los sacerdotes, con los ancianos, los escribas y todo el consejo, celebraron una consulta, ataron a Jesús, lo llevaron y lo entregaron a Pilato.
2 Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
Pilato le preguntó: “¿Eres tú el Rey de los judíos?” Respondió: “Eso dices tú”.
3 Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
Los jefes de los sacerdotes le acusaron de muchas cosas.
4 Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
Pilato volvió a preguntarle: “¿No tienes respuesta? Mira cuántas cosas declaran contra ti”.
5 Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
Pero Jesús no respondió más, por lo que Pilato se maravilló.
6 Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
En la fiesta solía liberar a un prisionero, cualquiera que pidiesen.
7 Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
Había uno llamado Barrabás, atado con sus compañeros de insurrección, hombres que en la insurrección habían cometido un asesinato.
8 Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
La multitud, gritando, comenzó a pedirle que hiciera lo que siempre hacía por ellos.
9 Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
Pilato les respondió diciendo: “¿Queréis que os suelte al Rey de los judíos?”
10 Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
Porque se dio cuenta de que por envidia los jefes de los sacerdotes lo habían entregado.
11 Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
Pero los jefes de los sacerdotes incitaron a la multitud para que les soltara a Barrabás en su lugar.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
Pilato volvió a preguntarles: “¿Qué debo hacer, pues, con el que llamáis Rey de los judíos?”
13 Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
Volvieron a gritar: “¡Crucifícalo!”
14 Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
Pilato les dijo: “¿Qué mal ha hecho?” Pero ellos gritaron con fuerza: “¡Crucifícalo!”
15 Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
Pilato, queriendo complacer a la multitud, les soltó a Barrabás y entregó a Jesús, después de haberlo azotado, para que fuera crucificado.
16 Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
Los soldados lo llevaron dentro del patio, que es el pretorio, y convocaron a toda la cohorte.
17 Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
Lo vistieron de púrpura y le pusieron una corona de espinas.
18 Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
Comenzaron a saludarlo: “¡Salve, rey de los judíos!”
19 Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
Le golpearon la cabeza con una caña, le escupieron y, doblando las rodillas, le rindieron homenaje.
20 Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
Cuando se burlaron de él, le quitaron el manto de púrpura y le pusieron sus propios vestidos. Lo llevaron para crucificarlo.
21 Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
Obligaron a uno que pasaba por allí, procedente del campo, Simón de Cirene, padre de Alejandro y de Rufo, a ir con ellos para que llevara su cruz.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
Le llevaron al lugar llamado Gólgota, que es, según la interpretación, “El lugar de la calavera”.
23 Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
Le ofrecieron de beber vino mezclado con mirra, pero no lo tomó.
24 Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
Al crucificarlo, se repartieron sus vestidos, echando a suertes lo que debía tomar cada uno.
25 Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
Era la hora tercera cuando lo crucificaron.
26 Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
Sobre él estaba escrita la superposición de su acusación: “EL REY DE LOS JUDÍOS”.
27 Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
Con él crucificaron a dos ladrones, uno a su derecha y otro a su izquierda.
28 Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
Se cumplió la Escritura que dice: “Fue contado con los transgresores”.
29 Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
Los que pasaban por allí le blasfemaban, moviendo la cabeza y diciendo: “¡Ja! Tú que destruyes el templo y lo construyes en tres días,
30 Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
sálvate a ti mismo y baja de la cruz”.
31 Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
Asimismo, también los jefes de los sacerdotes, burlándose entre ellos con los escribas, decían: “Ha salvado a otros. No puede salvarse a sí mismo.
32 Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
Que baje ahora de la cruz el Cristo, el Rey de Israel, para que le veamos y le creamos.” Los que estaban crucificados con él también le insultaban.
33 Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
Cuando llegó la hora sexta, hubo oscuridad sobre toda la tierra hasta la hora novena.
34 Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
A la hora novena, Jesús clamó a gran voz, diciendo: “Eloi, Eloi, lama sabachthani?”, que es, interpretado, “Dios mío, Dios mío, ¿por qué me has abandonado?”
35 Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
Algunos de los que estaban allí, al oírlo, dijeron: “He aquí que llama a Elías”.
36 Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
Uno corrió y, llenando una esponja de vinagre, la puso en una caña y se la dio a beber, diciendo: “Déjalo. A ver si viene Elías a bajarlo”.
37 Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
Jesús gritó con fuerza y entregó el espíritu.
38 Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
El velo del templo se rasgó en dos desde arriba hasta abajo.
39 Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
Cuando el centurión, que estaba frente a él, vio que gritaba así y exhalaba, dijo: “¡Verdaderamente este hombre era el Hijo de Dios!”
40 Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
Había también mujeres que miraban desde lejos, entre las cuales estaban María Magdalena y María la madre de Santiago el Menor y de José, y Salomé;
41 Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
las cuales, estando él en Galilea, le seguían y le servían; y otras muchas que subieron con él a Jerusalén.
42 Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
Cuando llegó la noche, por ser el día de la preparación, es decir, la víspera del sábado,
43 Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
vino José de Arimatea, miembro destacado del consejo, que también buscaba el Reino de Dios. Entró audazmente a Pilato y pidió el cuerpo de Jesús.
44 Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
Pilato se sorprendió al oír que ya estaba muerto; y llamando al centurión, le preguntó si llevaba mucho tiempo muerto.
45 Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
Al enterarse por el centurión, concedió el cuerpo a José.
46 Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
Compró un lienzo y, bajándolo, lo envolvió en el lienzo y lo depositó en un sepulcro excavado en una roca. Hizo rodar una piedra contra la puerta del sepulcro.
47 Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.
María Magdalena y María, la madre de Josés, vieron dónde estaba depositado.

< Marko 15 >