< Marko 14 >

1 Ilikuwa siku mbili tu kabla ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
Now after two days was the Passover and the unleavened bread. And the chief priests and the scholars sought how, having take him with trickery, they might kill him,
2 Lakini walisema, “Tusimtie nguvuni wakati wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
but they said, Not during the feast, lest there will be an uproar of the people.
3 Yesu alikuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, Mkoma. Alipokuwa mezani kula chakula, mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya nardo safi ya thamani kubwa alikuja, akaivunja hiyo chupa, akammiminia Yesu marashi hayo kichwani.
And while he was in Bethany in the house of Simon the leper, as he sat relaxing, a woman came having an alabaster cruse of ointment of pure spikenard, very valuable. And having broken the alabaster cruse, she poured it on his head.
4 Baadhi ya watu waliokuwa hapo walikasirika wakajisemea, “Kwa nini kupoteza ovyo marashi haya?
And some were indignant within themselves, saying, Why has this waste of the ointment happened?
5 Yangaliweza kuuzwa kwa fedha kiasi cha denari mia tatu, wakapewa maskini!” Wakamkemea huyo mama.
For this could have been sold for over three hundred denarii, and given to the poor. And they grumbled at her.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mwacheni; kwa nini mnamsumbua? Amenitendea jambo jema.
But Jesus said, Leave her be. Why do ye cause troubles for her? She performed a good work on me.
7 Maskini mnao daima pamoja nanyi; mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaopenda. Lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
For ye always have the poor with you, and whenever ye may desire ye can do them well, but ye do not always have me.
8 Yeye amefanya alivyoweza; ameupaka mwili wangu marashi kuutayarisha kwa maziko.
She applied what she had to anoint my body. She did it beforehand for the burial.
9 Nawaambieni kweli, popote ulimwenguni Habari Njema itakapohubiriwa, kitendo hiki alichofanya kitatajwa kwa ajili ya kumkumbuka.”
And truly I say to you, wherever this good news may be preached in the whole world, also what she did will be told for a memorial of her.
10 Kisha Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, alienda kwa makuhani wakuu ili kumsaliti Yesu.
And Judas Iscariot, one of the twelve, went away to the chief priests, so that he might betray him to them.
11 Makuhani wakuu waliposikia habari hiyo, walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Basi, Yuda akaanza kutafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.
And when they heard it, they were glad, and promised to give him silver. And he sought how he might betray him conveniently.
12 Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wakati ambapo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wake walimwuliza, “Wataka tukuandalie wapi karamu ya Pasaka?”
And on the first day of unleavened bread, when they killed the Passover, his disciples say to him, Where do thou want, after going, we should prepare that thou may eat the Passover?
13 Basi Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake akiwaambia, “Nendeni mjini, nanyi mtakutana na mtu anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni
And he sends forth two of his disciples, and says to them, Go into the city, and a man carrying a pitcher of water will meet you. Follow him.
14 mpaka katika nyumba atakayoingia, mkamwambie mwenye nyumba, Mwalimu anasema: wapi chumba changu ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
And wherever he may enter, say ye to the house-ruler, The teacher says, Where is the guest room, where I may eat the Passover with my disciples?
15 Naye atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani kilichotayarishwa na kupambwa. Tuandalieni humo.”
And he himself will show you a large upper room spread out ready. Prepare ye for us there.
16 Wanafunzi wakaondoka, wakaenda mjini, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia. Wakaandaa karamu ya Pasaka.
And his disciples went forth, and came into the city, and found just as he had said to them. And they prepared the Passover.
17 Ilipokuwa jioni, Yesu alifika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
And having become evening he comes with the twelve.
18 Walipokuwa mezani wakila, Yesu alisema, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu anayekula pamoja nami, atanisaliti.”
And as they were relaxing and eating, Jesus said, Truly I say to you, that one of you eating with me will betray me.
19 Hapo wanafunzi wake wakaanza kuhuzunika, wakamwuliza mmojammoja, “Je, ni mimi?”
They began to be sorrowful, and to say to him one by one, Not I? and another, Not I?
20 Yesu akawaambia, “Ni mmoja wenu ninyi kumi na wawili, anayechovya mkate pamoja nami katika bakuli.
And having answered, he said to them, It is one of the twelve dipping with me in the dish.
21 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake; lakini, ole wake mtu yule anayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa!”
The Son of man indeed goes as it is written about him, but woe to that man through whom the Son of man is betrayed! It was good for him if that man was not born.
22 Walipokuwa wanakula, Yesu alitwaa mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni; huu ni mwili wangu.”
And as they were eating, Jesus having taken bread, having blessed, he broke in pieces, and gave to them, and said, Take, eat, this is my body.
23 Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa; nao wote wakanywa katika kikombe hicho.
And after taking the cup, having expressed thanks, he gave to them, and they all drank from it.
24 Akawaambia, “Hii ni damu yangu inayothibitisha agano la Mungu, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi.
And he said to them, This is my blood of the new covenant, which is poured out for many.
25 Kweli nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa upya katika Ufalme wa Mungu.”
Truly I say to you, that I will no more drink of the fruit of the grapevine, until that day when I drink it anew in the kingdom of God.
26 Kisha wakaimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
And when they sang a hymn, they went out onto the mount of Olives.
27 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami; maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji nao kondoo watatawanyika.
And Jesus says to them, All ye will be caused to stumble by me this night, because it is written, I will strike the shepherd, and the sheep will be scattered.
28 Lakini nikisha fufuka, nitawatangulieni kule Galilaya.”
But after I am raised up, I will go before you into Galilee.
29 Petro akamwambia “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakukana kamwe!”
But Peter said to him, Even if all will be caused to stumble, yet not I.
30 Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.”
And Jesus says to him, Truly I say to thee, that thou today, in this night, before a cock sounds twice, will deny me thrice.
31 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakuacha kamwe.” Wanafunzi wote pia wakasema vivyo hivyo.
But he spoke more extreme, If I must die with thee, I will, no, not deny thee. And they all spoke the same way also.
32 Basi, wakafika katika bustani iitwayo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati mimi nasali.”
And they come to a place the name of which was Gethsemane. And he says to his disciples, Sit ye here until I pray.
33 Kisha akawachukua Petro, Yakobo na Yohane; akaanza kufadhaika sana na kuhangaika.
And he takes Peter and James and John with him, and began to be greatly disturbed, and very distressed.
34 Akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe.”
And he says to them, My soul is deeply grieved, to the point of death. Remain ye here, and watch.
35 Akaenda mbele kidogo, akajitupa chini kifudifudi, akasali kwamba, kama ingewezekana, asiipitie saa hiyo ya mateso.
And having gone forward a little, he fell on the ground, and prayed that, if it were possible, the hour might pass from him.
36 Akasema, “Baba yangu, kwako mambo yote yanawezekana. Uniondolee kikombe hiki; lakini isiwe kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”
And he said, Abba, Father, all things are possible to thee. Remove this cup from me, but not what I want, but what thou want.
37 Kisha akarudi kwa wanafunzi wale watatu, akawakuta wamelala. Basi, akamwuliza Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?”
And he comes and finds them sleeping. And he says to Peter, Simon, Do thou sleep? Could thou not watch one hour?
38 Kisha akawaambia, “Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Watch ye and pray that ye may not enter into temptation. Truly, the spirit is willing, but the flesh is weak.
39 Akaenda kusali tena akirudia maneno yaleyale.
And again having departed, he prayed, having said the same statement.
40 Kisha akarudi tena, akawakuta wamelala. Macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Hawakujua la kumjibu.
And having returned, he found them again sleeping, for their eyes were weighed down, and they knew not what they should reply to him.
41 Alipowajia mara ya tatu aliwaambia, “Mnalala bado na kupumzika? Sasa imetosha! Saa imefika! Mwana wa Mtu anakabidhiwa kwa watu waovu.
And he comes the third time, and says to them, Sleep the remaining, and take your rest. It is enough. The hour has come. Behold, the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
42 Amkeni, twendeni zetu. Tazameni, yule atakayenisaliti amekaribia.”
Arise, let us be going. Behold, he who betrays me has come near.
43 Yesu alipokuwa bado anasema, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akafika pamoja na umati wa watu wenye mapanga na marungu. Watu hao walikuwa wametumwa na makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee.
And straightaway, while he still spoke, Judas, being one of the twelve, comes, and with him a great multitude with swords and clubs from the chief priests, and the scholars, and the elders.
44 Msaliti Yuda alikuwa amewapa ishara: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni, mkampeleke chini ya ulinzi.”
Now he who betrayed him had given them a sign, saying, Whomever I may kiss is he. Seize him, and lead away securely.
45 Yuda alipofika tu, alimwendea Yesu moja kwa moja, akasema, “Mwalimu!” Kisha akambusu.
And when he came, straightaway having approached him, he says, Rabbi, Rabbi, and kissed him much.
46 Basi, hao watu wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
And they threw their hands on him, and seized him.
47 Mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja na Yesu akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
And a certain one of those who stood by, having drawn his sword, struck the bondman of the high priest, and cut off his ear.
48 Yesu akawaambia, “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
And having answered, Jesus said to them, Have ye come out as against a robber with swords and clubs to arrest me?
49 Kila siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini sasa lazima Maandiko Matakatifu yatimie.”
I was daily near you, teaching in the temple, and ye did not seize me-but that the scriptures might be fulfilled.
50 Hapo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
And having forsook him, they all fled.
51 Kulikuwa na kijana mmoja aliyekuwa anamfuata Yesu akiwa amevaa shuka. Nao wakajaribu kumkamata.
And a certain one young man followed with him, having been wrapped naked in a linen cloth. And the young men seized him,
52 Lakini yeye akaponyoka, akaiachilia ile shuka, akakimbia uchi.
but having left behind the linen cloth, he fled from them naked.
53 Basi, wakampeleka Yesu kwa Kuhani Mkuu ambapo makuhani wakuu wote, wazee na walimu wa Sheria walikuwa wamekutanika.
And they led Jesus away to the high priest. And all the chief priests and the elders and the scholars assemble with him.
54 Petro alimfuata Yesu kwa mbali, akaingia ndani ya ya wa Kuhani Mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto.
And Peter followed him from a distance, as far as inside the courtyard of the high priest, and was sitting with the subordinates, and warming himself near the light.
55 Makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa kumshtaki Yesu wapate kumwua, lakini hawakupata.
Now the chief priests and the whole council sought testimony against Jesus in order to put him to death, and did not find it.
56 Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.
For many testified falsely against him, and their testimonies were not consistent.
57 Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:
And some men having stood up, testified falsely against him, saying,
58 “Tulimsikia mtu huyu akisema, Nitaliharibu Hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono.”
We heard him saying, I will destroy this temple made with hands, and by three days I will build another not made with hands.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.
And not even this way was their testimony consistent.
60 Basi, Kuhani Mkuu akasimama katikati yao, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
And the high priest having stood up in the midst, he demanded Jesus, saying, Thou answer nothing? What is it these men testify against thee?
61 Lakini yeye akakaa kimya; hakusema hata neno moja. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Mtukufu?”
But he remained silent, and answered nothing. Again the high priest demanded him, and says to him, Are thou the Christ, the Son of the Blessed?
62 Yesu akajibu, “Naam, mimi ndiye. Tena, mtamwona Mwana wa Mtu amekaa upande wa kulia wa Mwenyezi, akija katika mawingu ya mbinguni.”
And Jesus said, I am. And ye will see the Son of man sitting at the right hand of Power, and coming with the clouds of the sky.
63 Hapo Kuhani Mkuu akararua joho lake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi?
And the high priest having torn his clothes, he says, What further need have we of witnesses?
64 Mmesikia kufuru yake! Ninyi mwaonaje?” Wote wakaamua kwamba anastahili kuuawa.
Ye have heard the blasphemy. What does it seem to you? And they all condemned him to be deserving of death.
65 Basi, baadhi yao wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, wakampiga na kumwambia, “Bashiri ni nani aliyekupiga!” Hata watumishi wakamchukua, wakampiga makofi.
And some began to spit on him, and to cover his face, and to strike him with a fist, and to say to him, Prophesy. And the subordinates were throwing him with slaps.
66 Petro alipokuwa bado chini ukumbini, mmoja wa wajakazi wa kuhani Mkuu alikuja.
And as Peter was below in the courtyard, one of the servant girls of the high priest comes.
67 Alipomwona Petro akiota moto, alimtazama, akamwambia, “Hata wewe ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.”
And having seen Peter warming himself, having looked at him, she says, Thou also were with Jesus of Nazareth.
68 Lakini Petro akakana, “Sijui, wala sielewi unayosema!” Kisha Petro akaondoka, akaenda nje uani. Hapo jogoo akawika.
But he denied, saying, I know not, nor understand what thou say. And he went outside onto the porch, and a cock sounded.
69 Yule mjakazi alipomwona tena Petro, akaanza tena kuwaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, “Mtu huyu ni mmoja wao.”
And the servant girl having seen him, she began again to say to those who stood by, This man is from them.
70 Petro akakana tena. Baadaye kidogo, watu waliokuwa wamesimama hapo wakamwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, maana wewe ni Mgalilaya.”
But he again denied it. And after a little while again those who stood by said to Peter, Surely thou are from them, for thou are a Galilean, and thy accent is similar.
71 Lakini Petro akaanza kulaani na kuapa akisema, “Mimi simjui mtu huyu mnayesema habari zake.”
But he began to curse and to swear, I do not know this man of whom ye speak.
72 Hapo jogoo akawika mara ya pili. Basi, Petro akakumbuka jinsi Yesu alivyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Petro akabubujika machozi.
And the second time a cock sounded. And Peter remembered the saying that Jesus said to him, Before a cock sounds twice, thou will deny me thrice. And having broke down, he wept.

< Marko 14 >