< Luka 8 >

1 Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
AND it was after these things that Jeshu itinerated among the cities and villages, and preached and announced the kingdom of Aloha, and his twelve with him,
2 Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
and those women who had been healed from infirmities and from evil spirits, Mariam who was called Magdalitha, she from whom he had cast out seven devils,
3 Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
and Juchana the wife of Kusa, chief of the household of Herodes, and Shushan, and many others, who ministered unto him from their possessions.
4 Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
And when a great multitude had assembled, and from all the cities had come to him, he discoursed in parables.
5 “Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
A sower went forth to sow his seed. And as he sowed, some fell by the road-side; and it was trodden down, and the fowl devoured it.
6 Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
And other fell upon the rock; and it immediately sprang up, and, because it had no moisture, it withered.
7 Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
And other fell among thorns, and they sprang up with it, and choked it.
8 Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia.” Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, “Mwenye masikio na asikie!”
And other fell into ground good and fair, and sprang up, and made fruit an hundredfold. And when he had said these (words), he cried, Whoever hath ears to hear, let him hear.
9 Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
And his disciples asked him, What is (the signification of) this parable?
10 Naye akajibu, “Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
But he said to them, To you it is given to know the mysteries of the kingdom of Aloha; but to those who are the rest in similitudes is it spoken; that while seeing they may not see, and while hearing they may not understand.
11 “Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
But this is the parable: The seed is the word of Aloha.
12 Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
Now they by the road-side are they who hear the word; and the adversary cometh, and taketh up the word from their hearts, that they should not believe and be saved.
13 Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
But those who fell upon the rock are those who, when they hear, with joy receive the word; yet root they have not, but for a time is their faith, and in the time of temptation they are offended.
14 Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
But that which fell among thorns are they who hear the word, and by the cares, and by the riches, and by the lusts of the world, they are choked, and fruit they give not.
15 Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
But that which (was) in good ground are they who, with hearts humble and good, hear the word and retain, and give fruits with perseverance.
16 “Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
NO man lighteth a lamp, and covereth it with a measure, or setteth it under a bed; but setteth it upon a candlestick, that every one who cometh in may see the light of it.
17 “Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
For there is nothing hidden which shall not be revealed, and nothing secret that shall not be known and come into openness.
18 “Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa.”
Take heed how you hear: for unto him who hath, it shall be given; and from him who hath not, that also which he thinketh that he hath shall be taken from him.
19 Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
Now came to him his mother and his brethren, and could not speak with him on account of the assembly.
20 Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
And they said to him, Thy mother and thy brethren are standing without, desiring to see thee.
21 Lakini Yesu akawaambia watu wote, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika.”
But he answered and said to them, These are my mother and my brethren, they who hear the word of Aloha, and do it.
22 Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo.” Basi, wakaanza safari.
NOW it was on one of the days that Jeshu ascended and sat in a vessel and his disciples: and he said to them, Let us pass to the other side of the water.
23 Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
But as they went, Jeshu himself slept. And there became a storm of wind on the water, and nigh was the vessel to be swallowed up.
24 Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, “Bwana, Bwana! Tunaangamia!” Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
And they approached (and) awoke him, saying to him, Our master, our master, we perish! But he arose and rebuked the winds and the waves of the sea; and they quieted, and there was a calm.
25 Kisha akawaambia, “Iko wapi imani yenu?” Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, “Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?”
And he said to them, Where is your faith? But they, afraid, wondered, saying one with another, Who is this that also commandeth the winds, and to whom the waves and the sea are obedient?
26 Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
And they went forward and came to the country of the Godroyee, which is over against Galila.
27 Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
And when he had gone forth to the land, there met him a certain man from the city, who had a devil in him a great time, and (who) wore no clothes, and in a house dwelt not, but in the place of the buried.
28 Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa “We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!”
But when he saw Jeshu, he cried out, and fell before him, and said in a high voice, What to us and to thee, Jeshu, son of Aloha Marima? I beseech of thee, torment me not.
29 Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
For Jeshu commanded the unclean spirit to come forth from the man. For long was the time that he had been enthralled of him; and (when) bound with chains, and kept with fetters, he had burst asunder his bonds, and had been driven by the demon into the waste.
30 Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Yeye akajibu, “Jina langu ni Jeshi” —kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
And Jeshu demanded of him, What is thy name? He saith to him, Legion: because that many devils had entered into him.
31 Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
And they besought from him that he would not cast them out to go into the abyss. (Abyssos g12)
32 Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
Now there was there a great herd of many swine which fed on the hill: and they besought from him that he would permit them to enter into the swine. And he permitted them.
33 Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
And the demons went forth from the man, and entered into the swine; and the whole herd went directly to the precipice, and plunged into the waters, and were suffocated.
34 Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
And when the herdmen saw the thing that was done, they fled, and made known in the city and in the villages.
35 Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
And the men went forth to see the thing which was done. And they came to Jeshu, and found the man from whom the demons had gone out, clothed, sober, and sitting at the feet of Jeshu. And they feared.
36 Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
And they who had seen it showed to them how the man of the demon had been healed.
37 Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
And the whole multitude of the Godroyee besought of Jeshu that he would go from them, because great fear had taken them. And he, Jeshu, ascended the ship, and returned from them.
38 Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
But he, the man from whom had gone forth the demons, besought of him that he might be with him. But Jeshu dismissed him, and said to him,
39 “Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea.” Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
Return to thine house, and show what Aloha hath done for thee. And he went and proclaimed in every city what Jeshu had done for him.
40 Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
WHEN Jeshu returned, a great multitude received him: for they were all expecting him.
41 Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
And a certain man whose name was Jorush, head of the synagogue, fell before the feet of Jeshu, and besought him to enter into his house;
42 kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
for he had an only daughter, as a daughter of twelve years, and she was nigh unto death. And as Jeshu went with him, the great multitude pressed him.
43 Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
And a certain woman whose blood had gushed forth twelve years, she who among the physicians had spent all her substance, but could not be healed by any one,
44 Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
approached him from behind, and touched the border of his garment, and immediately stood the flowing of her blood.
45 Yesu akasema, “Ni nani aliyenigusa?” Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, “Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!”
And Jeshu said, Who touched me? And when all denied, Shemun Kipha and those with him said, Raban, the crowd straiteneth and presseth thee, and sayest thou, Who touched me?
46 Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka.”
But he said, Some one hath touched me, for I know that power hath gone forth from me.
47 Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
And she, the woman, when she saw that she was not hid, came trembling and fell (and) worshipped him. And she told before all the people for what cause she had touched him, and how at once she had been healed.
48 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
But he, Jeshu, said to her, Be comforted, my daughter: thy faith hath saved thee, go in peace.
49 Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: “Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?”
And while he was speaking, there came a man from the chief of the synagogue and said to him, Thy daughter is dead, weary not the Malphona.
50 Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, “Usiogope; amini tu, naye atapona.”
But Jeshu heard, and said to the father of the damsel, Fear not, only believe, and she lives!
51 Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
But Jeshu came to the house, and he suffered no man to enter with him, save Shemun, and Jakub, and Juchanon, and the father of the damsel, and her mother.
52 Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, “Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!”
And they were all weeping and wailing for her; but Jeshu said, Weep not, for she is not dead, but asleep.
53 Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
And they laughed at him, for they knew that she was dead.
54 Lakini Yesu akamshika mkono akasema, “Mtoto amka!”
But he put every man forth without. And he took her by the hand, and called and said, Damsel, arise.
55 Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
And her spirit returned, and she arose. And he directed that they should give her to eat.
56 Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.
And her parents were astonished; but he cautioned them that no man they should tell what he had done.

< Luka 8 >