< Luka 6 >

1 Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
One (Sabbath/Jewish day of rest), while Jesus was walking through some grain fields with his disciples, the disciples picked some of the heads of grain. They rubbed them in their hands [to separate the grains from the husks], and ate the grain. [The law of Moses permitted people to do that if they were hungry].
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
Some Pharisees [who were watching] said to Jesus, “(You should not be doing on our rest day [work] that [our] laws forbid!/Why are you doing on our rest day [work] that our laws forbid?)” [RHQ]
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
[Jesus wanted to show them that the record in Scriptures indicated that God permitted people to disobey certain religious laws when they needed food]. [So] he replied, “[It is written in the Scriptures] what [our revered ancestor, King] David did when he and the men with him were hungry. You have read about that, ([but you do not think about what it implies/so why do you not think about what it implies]?) [RHQ]
4 Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
David entered God’s big worship tent [and asked for some food]. [The high priest gave him] the bread that the priests had presented to God. It was permitted [in] one of [Moses’ laws] that only the priests could eat that bread. But [even though David was not a priest], he ate some, and gave some to the men who were with him. [And God did not consider that what David did was wrong]!”
5 Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
Jesus also said to them, “[I am] the one who came from heaven, so [I] have the authority [to determine what is right for my disciples to do on] the day of rest!”
6 Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
Another (Sabbath/Jewish day of rest) Jesus entered a (synagogue/Jewish meeting place) and taught the people. There was a man there whose right hand was shriveled.
7 Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
The men who taught the [Jewish] laws and the Pharisees [who were there] watched Jesus, to see if he would heal the man (on the Sabbath/on the Jewish rest day). They did this so that, [if he healed the man], they would accuse him [of disobeying their laws by working on the day of rest].
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
But Jesus knew what they were thinking. So he said to the man with the shriveled hand, “Come and stand here [in front of everyone]!” So the man got up and stood there.
9 Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
Then Jesus said to the others, “I ask you this: Do the laws that [God gave Moses] permit [people] to do what is good (on the Sabbath/on the Jewish rest day), or [do they permit people] to harm [others]? [Do they permit us] to save [a person’s] life [on our day of rest] or to let [him] die [HYP] [by refusing to help him]?”
10 Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
[They refused to answer him. So] after he looked around at them all, he said to the man, “Stretch out your [shriveled] hand!” The man did that, and his hand became all right again!
11 Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
But the men who taught the Jewish laws and the Pharisees were very angry, and they discussed with one another what they could do to [get rid of] Jesus.
12 Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
About that time [Jesus] went up into the hills to pray. He prayed to God all night.
13 Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
The next day he summoned all his disciples to come near him. From them he chose twelve men, whom he called apostles.
14 Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
They were Simon, to whom he gave the [new] name, Peter; Andrew, Peter’s [younger] brother; James and [his younger brother], John; Philip; Bartholomew;
15 Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
Matthew, whose other name was Levi; Thomas; [another] James, the [son] of Alpheus; Simon, who belonged to the party [that encouraged people to] rebel [against the Roman government];
16 Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
Judas, the [son] of [another] James; and Judas Iscariot (OR, Judas, the man from Kerioth [Town]), the one who later (betrayed Jesus./enabled the Jewish leaders to seize Jesus.)
17 Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
[Jesus] came down from the hills with his disciples and stood on a level area. There was a very big crowd of his disciples there. There was also a large group of people who had come from Jerusalem and from many [other] places [in] Judea [district], and from the coastal areas near Tyre and Sidon [cities].
18 Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
They came to hear Jesus talk to them and to be healed {and for him to heal them} from their diseases. He also healed those whom evil spirits had troubled.
19 Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
Everyone [in the crowd] tried to touch him, because he was healing everyone by [his/God’s] power.
20 Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
He looked [MTY] at his disciples and said, “[God] is pleased with you [who know] that you lack what [he wants you to have; ] he will allow you to be the people whose lives he rules over.
21 Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
[God] is pleased with you who sincerely desire to receive what [MTY] [he wants you to have]; he will give you what you need, until you are satisfied. [God] is pleased with you that grieve now [because of sin]. Later you will be joyful.
22 “Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
[God] is pleased with you when [other] people hate you, when they will not let you join them, when they insult you, when they say that you are evil because [you believe in] me, the one who came from heaven.
23 Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
When that happens, rejoice! Jump up and down because you are so happy! [God will give] you a great reward in heaven! [When they do these things to you, it will prove that you are God’s servants]. (OR, [People have always treated God’s servants like that].) Do not forget that these people’s ancestors did the same things to the prophets [who served God faithfully]!
24 Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
But there will be terrible punishment for you that are rich; the happiness you have received [from your riches] is the only happiness that you will get.
25 Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
There will be terrible punishment for you who [think that you] have all that you need now; you will [realize] that these things will not make you feel satisfied. There will be terrible punishment for you who are joyful now; you will [later] be very sad.
26 Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
When most [HYP] people speak well about you, trouble is ahead for you; [it will not prove that you are God’s servants, because] your ancestors used to speak well about those who falsely [claimed that they were] prophets.”
27 “Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
“But I say this to each of you [disciples] who are listening [to what I say]: Love your enemies [as well as your friends]. Do good things for those who hate you!
28 Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
[Ask God to] bless those who curse you! Pray for those who mistreat you!
29 Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
If someone [insults one of you by] striking you on one of your cheeks, turn your face [so that he can strike] the other cheek [also]. If [a bandit] wants to take away your [(sg)] coat, let him also have your shirt.
30 Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
Give something to everyone who asks you [(sg) for something]. If someone takes away things that belong to you [(sg)], do not ask him to return them.
31 Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
In whatever way you [(pl)] want others to act toward you, that is the way that you should act toward them.
32 “Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
If you love [only] those who love you, do not [expect God] to praise you for [doing that] [RHQ], [because] even sinners love those who love them.
33 Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
If you do good things [only] for those who do good things for you, do not [expect God] to reward you [for doing that] [RHQ], [because] even sinners do that.
34 Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
If you lend [things or money only] to those who you expect will give something back to you, do not [expect that God] will reward you [RHQ] [for doing that]. Even sinners lend to other sinners, because they expect them to pay everything back.
35 Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
Instead, love your enemies! Do good things for them! Lend to them, and do not expect them to pay anything back! [If you do that, God will give] you a big reward. And you will be [acting like] his children [should]. Remember that God is kind to people who are not grateful and to people who are wicked, [and he expects you to be like that too].
36 Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
Act mercifully toward others, just like your Father [in heaven acts] mercifully [toward you].”
37 “Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
“Do not say how sinfully others have acted, and then [God] will not say how sinfully you have acted. Do not condemn others, and then [he] will not condemn you [DOU]. Forgive others [for the evil things that they have done to you], and then [God] will forgive you.
38 Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
Give [good things to others], and then [God] will give [good] things to you. It will be [as though] [MET] [God is putting things in a basket] for you. He will give you a full amount, pressed down in the basket, which he will shake [so that he can put more in], and it will spill over the sides! [Remember that] the way you act [toward others] will be the way that [God] will act toward you!”
39 Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
He also told [his disciples] this parable [to show them that they should be like him, and not be like the Jewish religious leaders]: “(You certainly would not [expect] a blind man to lead another blind man./Would you [expect] a blind man to lead [another] blind man?) [RHQ] If he tried to do [that], (they would both probably fall into a hole!/wouldn’t they both probably fall into a hole?) [RHQ] [I am your teacher, and you disciples should be like me].
40 Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
A disciple should not [expect to be] better known than his teacher. But if a student is fully trained {if someone fully trains a student}, the student can become like his teacher [MET]. [So you should be content to be like me].
41 Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
(Why do you notice [someone else’s small faults]?/None of you should be concerned about [someone else’s small faults] [MET, RHQ].) [That would be like] noticing a speck in that person’s eye. But you should be concerned about [your own big faults. They are like] planks in your own eye, [which you do not notice].
42 Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
(You [(sg)] should not say, ‘Friend, let me take out that speck in your eye!’ when you do not notice the log in your own eye!/Why do you say, ‘Friend, let me take out that speck in your eye!’ when you do not notice the log in your own eye?) [RHQ] [If you do that], you are a hypocrite! You should first [stop committing your own sins. That will be like] removing the plank from your own eye. Then, as a result, you will have the spiritual insight you need to help others get rid of the [faults that are like] specks in their eyes.”
43 “Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
“[People are like trees] [MET]. Healthy trees do not bear bad fruit (OR, bear only good fruit), and unhealthy trees do not bear good fruit.
44 Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
[Just like you] can tell if a tree is good or bad by looking at its fruit, [you can tell which people are good and which are bad by looking at the way they] conduct their lives. [For example, because thornbushes cannot produce figs], no one can pick figs from thornbushes. And [since bramble bushes cannot produce grapes], no one can [pick] grapes from bramble bushes.
45 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
[Similarly], good people will conduct their lives in a good way because they think a lot of good [things], and evil people will live in an evil way because they think a lot of evil [things]. The basic principle is that people speak [and act] according to all that they think.”
46 “Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
“[Because people should obey what their masters tell them], (it is disgraceful that you say that I am your master but you do not do what I tell you!/why do you say that I am your master but you do not do what I tell you?) [RHQ]
47 Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
Some people come to me, and hear my messages and obey them. I will tell you what they are like.
48 Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
They are like a man who dug deep [into the ground to prepare to build his house]. He made sure that the foundation was on solid ground. Then when there was a flood, the water tried to wash away the house. But the river could not shake the house, because it was built {he built it} on a solid [foundation].
49 Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”
But some people hear my messages but do not obey them. They are like a man who built a house on top of the ground without [digging] a foundation. When the river flooded, the house collapsed immediately and was completely ruined. [So it is important for you to obey what I teach you].”

< Luka 6 >