< Luka 3 >

1 Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
Piecpadsmitā ķeizara Tiberijus valdīšanas gadā, kad Poncius Pilatus bija zemes valdītājs Jūdejā un Hērodus valdnieks Galilejā un Filips, viņa brālis, valdnieks Iturejā un Trakonites tiesā un Lizanijus valdnieks Abilenē,
2 na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
Apakš tiem augstiem priesteriem Annasa un Kajafasa, Dieva vārds notika uz Jāni, Zaharijas dēlu, tuksnesī.
3 Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
Un viņš gāja pa visu Jardānes apgabalu, sludinādams kristību uz atgriešanos no grēkiem par grēku piedošanu.
4 Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
Itin kā rakstīts pravieša Jesajas grāmatā, kas saka: “Saucēja balss tuksnesī: “Sataisiet Tā Kunga ceļu, dariet līdzenas Viņa tekas.
5 Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
Visas ielejas lai top pildītas, un visi kalni un pakalni lai top zemoti, un kas nelīdzens, lai top līdzens, un kas celmains, par staigājamu ceļu;
6 Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
Un visa miesa redzēs Tā Kunga pestīšanu.””
7 Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
Tāpēc viņš sacīja uz tiem ļaudīm, kas izgāja, ka no viņa tiktu kristīti: “Jūs odžu dzimums, kas jums ir rādījis izbēgt no nākamās dusmības?
8 Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
Tāpēc nesiet pienākamus atgriešanās augļus; un nesākat savā prātā sacīt: “Mums ir Ābrahāms par tēvu.” Jo Es jums saku, ka Dievs no šiem akmeņiem Ābrahāmam spēj bērnus radīt.
9 Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
Jau arī cirvis kokiem pie saknes pielikts; tāpēc ikkatrs koks, kas nenes labus augļus, top nocirsts un ugunī iemests.”
10 Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
Un tie ļaudis tam jautāja un sacīja: “Ko tad mums būs darīt?”
11 Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
Viņš atbildēja un uz tiem sacīja: “Kam divi svārki, tas lai dod tam, kam nav; un kam ir barība, lai dara tāpat.”
12 Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
Bet arī muitnieki nāca, ka liktos kristīties, un uz to sacīja: “Mācītāj, ko mums būs darīt?”
13 Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
Un viņš uz tiem sacīja: “Neņemiet vairāk, nekā jums ir nospriests.”
14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
Bet arī karavīri tam jautāja un sacīja: “Ko tad mums būs darīt?” Un viņš uz tiem sacīja: “Nedariet nevienam pāri, neapmelojiet nevienu un esat mierā ar savu algu.”
15 Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
Bet tiem ļaudīm gaidot un visiem savā prātā par Jāni domājot, vai tas neesot Kristus,
16 Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Jānis visiem atbildēja sacīdams: “Es jūs gan kristīju ar ūdeni, bet Viens nāks, spēcīgāks, nekā es, Tam es neesmu cienīgs atraisīt Viņa kurpju siksnas. Tas jūs kristīs ar Svētu Garu un uguni;
17 Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
Tam vēteklis rokā, un Viņš tīrīs Savu klonu caur caurim un sakrās kviešus Savā klētī, bet pelavas sadedzinās ar neizdzēšamu uguni.”
18 Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
Arī vēl daudz citu ko mācīdams, viņš pasludināja tiem ļaudīm prieka vēsti.
19 Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
Bet Hērodus, viens no tiem četriem valdniekiem, no viņa pārmācīts Hērodeijas, Filipa, sava brāļa, sievas dēļ, un visa ļauna dēļ, ko Hērodus bija darījis,
20 Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
Pie visa tā arī šo vēl darīja, ka Jāni ieslēdza cietumā.
21 Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
Un notikās, kad visi ļaudis tapa kristīti, un arī Jēzus bija kristīts un Dievu pielūdza, tad debesis atvērās,
22 na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
Un Svētais Gars nolaidās uz Viņu redzamā ģīmī kā balodis; un balss atskanēja no debesīm sacīdama: “Tu esi Mans mīļais Dēls, pie Tevis Man ir labs prāts.”
23 Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
Un Viņš pats, Jēzus, bija trīsdesmitā gadā un bija pēc ļaužu domām Jāzepa dēls, tas bija Elus dēls,
24 Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
Tas Matata, tas Levja, tas Melkus, tas Janna, tas Jāzepa dēls,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
Tas Matatijas, tas Amosa, tas Naūma, tas Eslus, tas Nagaja dēls,
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
Tas Maāta, tas Matatijas, tas Zemeja, tas Jāzepa, tas Jūdas dēls,
27 mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
Tas Jāņa, tas Rezas, tas Corobabeļa, tas Zalatiēļa, tas Nerus dēls,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
Tas Melķus, tas Addas, tas Kozama, tas Elmodama, tas Era dēls,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
Tas Jāzepa, tas Eliēcera, tas Jorema, tas Matata, tas Levja dēls,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
Tas Sīmeana, tas Jūdas, tas Jāzepa, tas Jonana, tas Eliaķima dēls,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
Tas Meleas, tas Menas, tas Matatas, tas Natana, tas Dāvida dēls,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
Tas Isajus, tas Obeda, tas Boasa, tas Zalmana, tas Nahšona dēls,
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
Tas Aminadaba, tas Arama, tas Hecrona, tas Vāreca, tas Jūdas dēls,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
Tas Jēkaba, tas Īzaka, tas Ābrahāma, tas Tārus, tas Nahora dēls,
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
Tas Serugs, tas Regus, tas Pelegs, tas Ēbera, tas Šalus dēls,
36 mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
Tas Kainana, tas Arvaksada, tas Zema, tas Noas, tas Lāmeha dēls,
37 mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
Tas Matuzalas, tas Enoha, tas Jareda, tas Mahalaleēla, tas Kainana dēls,
38 mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
Tas Enosa, tas Seta, tas Ādama dēls, tas Dieva.

< Luka 3 >