< Luka 3 >

1 Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
In the fiftenthe yeare of the raygne of Tiberius the Emperoure Pontius Pylate beinge leftenaut of Iurie and Herode beinge Tetrach of Galile and his brother Philip Tetrach in Iturea and in the region of Traconites and Lysanias the Tetrach of Abyline
2 na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
when Anna and Cayphas were the hye prestes: the worde of God came vnto Iohn ye sonne of zacharias in the wildernes.
3 Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
And he came in to all the coostes aboute Iordan preachynge the baptyme of repentaunce for the remission of synnes
4 Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
at it is written in the boke of the sayinges of Esaias ye Prophet which sayeth: The voyce of a cryar in wyldernes prepare the waye of the Lorde make hys pathes strayght.
5 Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
Every valley shalbe fylled and every moutayne and hyll shalbe brought lowe. And crocked thinges shalbe made streight: and the rough wayes shalbe made smoth:
6 Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
and all flesshe shall se the saveour sent of God.
7 Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
Then sayde he to the people that were come to be baptysed of him: O generacion of vipers who hath taught you to flye from the wrath to come?
8 Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
Bringe forth due frutes of repentaunce and begynne not to saye in youre selves we have Abraham to oure father. For I saye vnto you: God is able of these stones to reyse vp chyldren vnto Abraham.
9 Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
Now also ys the axe leyd vnto the rote of the trees: so yt every tree which bringeth not forth good frute shalbe hewe doune and caste in to ye fyre.
10 Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
And the people axed him sayinge: What shall we do then?
11 Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
He answered and sayde vnto them: He that hath two coottes let him parte with him that hath none: and he that hath meate let him do lyke wyse.
12 Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
Then came ther Publicans to be baptised and sayde vnto him: Master what shall we do?
13 Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
And he sayde vnto the: requyre no more then that which ys appoynted vnto you.
14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
The soudyoures lyke wyse demaunded of hym sayinge: and what shall we do? And he sayde to them: Do violence to noo ma: nether trouble eny man wrongfully: but be content with youre wages.
15 Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
As the people were in a doute and all men disputed in their hertes of Iohn whether he were very Christ:
16 Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Ihon answered and sayde to them all: I baptyse you wt water but a stronger then I cometh after me whose shue latchet I am not worthy to vnlouse: he will baptise you with the holy goost and with fyre:
17 Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
which hath his fanne in his hond and will pourge his floore and will gader the corne into his barne: but the chaffe wyll he bourne with fyre that never shalbe quenched.
18 Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
And many other thinges in his exhortacion preached he vnto the people.
19 Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
Then Herode the Tetrach (when he was rebuked of him for Herodias his brother Philippes wyfe and for all the evyls which Herod had done)
20 Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
added this above all and leyd Iohn in preson.
21 Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
And yt fortuned as all the people receaved baptyme (and when Iesus was baptised and dyd praye) that heave was opened
22 na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
and the holy goost came doune in a bodely shape lyke a dove vpo him and a voyce came fro heve sayinge: Thou arte my dere sonne in the do I delyte.
23 Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
And Iesus him silfe was about thirty yere of age when he begane beinge as men supposed the sonne of Ioseph. which Ioseph was the sonne of Heli
24 Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
which was the sonne of Mathat which was the sonne of Levi: which was the sonne of Melchi: which was the sonne of Ianna: which was the sonne of Ioseph:
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
which was the sonne of Matatthias: which was the sonne of Amos: which was the sonne of Nahum: which was the sonne of Esli: which was the sonne of Nagge:
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
which was the sonne of Maath: which was the sonne of Matathias: which was the sonne of Semei: which was the sonne of Ioseph: which was the sonne of Iuda:
27 mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
which was the sonne of Iohanna: which was the sonne of Rhesya: which was the sonne of zorobabel: which was the sonne of Salathiel: which was the sonne of Neri:
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
which was the sonne of Melchi: which was the sonne of Addi: which was the sonne of Cosam: which was the sonne of Helmadam: which was the sonne of Her:
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
which was the sonne of Ieso: which was the sonne of Helieser: which was the sonne of Ioram: which was the sonne of Mattha: which was the sonne of Levi:
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
which was the sonne of Simeon: which was the sonne of Iuda: which was the sonne of Ioseph: which was the sonne of Ionam: which was the sonne of Heliachim:
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
which was the sonne of Melea: which was the sonne of Menam: which was the sonne of Mathathan: which was the sonne of Nathan: which was the sonne of David:
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
which was the sonne of Iesse: which was the sonne of Obed: which was the sonne of Boos: which was the sonne of Salmon: which was the sonne of Naason:
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
which was the sonne of Aminadab: which was the sonne of Aram: which was the sonne of Esrom: which was the sonne of Phares: which was the sonne of Iuda:
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
which was the sonne of Iacob: which was the sonne of Ysaac: which was the sonne of Abraham: which was the sonne of Tharra: which was the sonne of Nachor:
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
which was the sonne of Saruch: which was the sonne of Ragau: which was the sonne of Phalec: which was the sonne of Heber: which was the sonne of Sala:
36 mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
which was the sonne of Cainan: which was the sonne of Arphaxat: which was the sonne of Sem: which was the sonne of Noe: which was the sonne of Lameth:
37 mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
which was the sonne of Mathusala: which was the sonne of Enoch: which was the sonne of Iareth: which was the sonne of Malalehel. which was the sonne of Cainan:
38 mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
which was the sonne of Enos: which was the sonne of Seth: which was the sonne of Adam: which was the sonne of God.

< Luka 3 >