< Luka 24 >

1 Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
的第一天,天還很早,婦女們便攜帶預備下的香料,來到墳墓那裏,
2 Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
見石頭已由墓穴滾開了。
3 Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
她們進去,不見了主耶穌的遺體。
4 Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
她們正為此事疑慮的時候,忽然有兩個人,穿著耀目的衣服,站在她們身邊。
5 Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
她們都害怕,把臉垂在地上,那兩個人對她們說:「妳們為什麼在死人中找活人呢﹖
6 Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
祂不在這裡了,祂已復活了。們應當記得:祂還在加利肋亞時,怎樣告訴過你們說:
7 Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka.”
「人子必須被於罪人之手,被釘在十字架上,並在第三日復活。」
8 Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
她們遂想起了祂的話,
9 wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
從墳墓那裏回去,把這一切事報告給那十一門徒及其餘的眾人,
10 Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
她們是瑪利亞瑪達肋納及約安納和雅各伯的母親瑪利亞;其餘同她們一起的婦女,也把這些事報告給宗徒。
11 Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
但婦女們的這些話,在他們看來,好像是無稽之談,不敢相信。
12 Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
伯多祿起來,跑到墳墓那裏,屈身向裡窺看,只見有殮布,就走了,心裏驚異所發生的事。
13 Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
就在那一天,他們中,有兩個人往一個村莊去,村名厄瑪烏,離耶路撒冷約六十「斯塔狄。」
14 Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
他們彼此講論所生的一切事。
15 Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
正談話討論的時候,耶穌親自走近他們,與他們同行。
16 Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
他們的眼睛卻被阻止往了,以致認不出祂來
17 Akawauliza, “Mnazungumza nini huku mnatembea?” Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
耶穌對他們說:「你們走路,彼此談論的是些什麼事﹖」他們就站往,面帶愁容。
18 Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, “Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?”
一個名叫克羅帕的,回答祂說:「獨有你在耶路撒冷作客,不知道在那裡這幾天所發生的事嗎﹖」
19 Naye akawajibu, “Mambo gani?” Wao wakamjibu, “Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
耶穌問他們說:「什麼事﹖」他們回答說:「就是有關納匝肋人耶穌的事。祂本是一位先知,在天主及眾百姓前,行事說話都權力。
20 Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
我們的司祭長及首領竟解送了祂,判了祂死罪,釘祂在十字架上。
21 Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
我們原指望祂就是那要拯救以色列的。可是─此外還有:這些事發生到今天已是第三天了。
22 Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
我們中有幾個婦女驚嚇了我們;她們清早到了墳墓那裏,
23 wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
沒有看見祂的遺體,回來說她們見了天使顯現,天使說祂復活了。
24 Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona.”
我們中也有幾個到過墳墓那裏,所遇見的事,如同婦女們所說的一樣,但是沒有看見祂。」
25 Kisha Yesu akawaambia, “Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
耶穌於是對他們說:「唉! 無知的人哪! 為信先知們所說的一切話,你們的心竟是這般遲鈍!
26 Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?”
默西亞不是必須受這些苦難,才進入祂的光榮嗎﹖」
27 Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
祂於是從梅瑟及眾先知開始,把全部經書論及祂的話,都給他們解釋了。
28 Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
當他們臨近了m囡去的村莊時,耶穌裝作還要前行。
29 lakini wao wakamsihi wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia.” Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
他們強留祂說:「請同我們一起住下吧! 因為快到晚上,天已垂暮了。」 耶穌就進去,同他們住下。
30 Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
當耶穌與他們坐下吃飯的時候,就拿起餅來,祝福了,擘開,遞給他們。
31 Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
他們的眼睛開了,這才認出耶穌來;但祂卻由他們眼前隱沒了。
32 Basi, wakaambiana, “Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?”
他們就彼此說:「當祂在路上與我們談話,給我們講解聖經的時候,我們的心不是火熱的嗎﹖」
33 Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
他們遂即動身,返回耶路撒冷,遇見那十一門徒及同同他們一起的人,正聚在一起,
34 wakisema, “Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni.”
彼此討論說:「主真復活了,並顯現給西滿了。」
35 Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
二人就把在路上的事,反在分餅時,怎樣認出了耶穌,述說了一遍。
36 Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia “Amani kwenu.”
他們正談論這事的時候,耶穌立在他們中間,向他們說:「願你們平安! 」
37 Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
眾人害怕起來,想是見了鬼神。
38 Lakini yeye akawaambia, “Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
耶穌向他們說:「你們為什麼恐懼﹖為什麼心裏起了疑惑﹖
39 Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo.”
你們看看我的手,我的腳,分明是我自己。你們摸摸我,應該知道:鬼神是沒有肉軀和骨頭的,如同你們看我,卻是有的。」
40 Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
說了這話,就把手和腳伸給他們看。
41 Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, “Mnacho chakula chochote hapa?”
他們由於歡喜,還是不敢信,只是驚訝;耶穌向他們說:「你們這裏有什麼吃的沒有﹖」
42 Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
他們便給了祂一塊烤魚。
43 Akakichukua, akala, wote wakimwona.
祂便接過來,當他們面前吃了。
44 Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”
耶穌對他們說:「我以前還同你們在一起的時候,就對你們說過這話:諸凡梅瑟法律、先知並聖詠上指著我所記載的話,都必須應驗。」
45 Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
耶穌遂開啟他們的明悟,叫他們理解經書;
46 Akawaambia, “Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
又向他們說:「經上曾這樣記載:默西亞必須受苦,第三天要從死者中復活;
47 na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
並且必須從耶路撒冷開始,因祂的名向萬邦宣講悔改,以得罪之赦。
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
你們就是這些事的見證人。
49 Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu.”
看,我要把我父所恩許的,遺發到你們身上;至於你們,你們應當留在這城中,直到佩帶上自高天而來的能力。」
50 Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
耶穌領他們出去,直到伯達尼附近,就舉手降福了他們。
51 Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
正降福他們的時候,就他們,被提升天去了。
52 Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
他們叩拜了祂,皆大歡喜地返回了耶路撒冷,
53 wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.
常在聖殿裏稱謝天主。

< Luka 24 >