< Luka 24 >

1 Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
下一周第一天清晨,女人们带着准备好的香料来到耶稣的坟墓。
2 Walikuta lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.
但发现坟墓口的大石头已经滚到了一边,
3 Walipoingia ndani, hawakuona mwili wa Bwana Yesu.
她们走进去,却没有看到主耶稣的身体。
4 Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kung'aa sana, wakasimama karibu nao.
正为此疑惑之际,眼前忽然出现两个人,身穿闪耀发光的衣服,站在她们旁边。
5 Hao wanawake wakaingiwa na hofu, wakainama chini. Ndipo wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai kati ya wafu?
女人们很害怕,把脸伏在地上。他们对女人说:“你们为什么要在死者中寻找一个还活着的人?
6 Hayuko hapa; amefufuka. Kumbukeni aliyowaambieni alipokuwa kule Galilaya:
他不在这里,而是已经复活了。你们应当记得他在加利利时说的话,
7 Ni lazima Mwana wa Mtu atolewe kwa watu waovu, nao watamsulubisha, na siku ya tatu atafufuka.”
他说:‘人子必将被交到罪人手里,钉在十字架上,在第三日复活。’”
8 Hapo wanawake wakayakumbuka maneno yake,
她们想起了耶稣说的话,
9 wakarudi kutoka kaburini, wakawapa mitume wale kumi na mmoja na wengine habari za mambo hayo yote.
于是就离开坟地,回去把这一切告诉了十一名门徒和其他人。
10 Hao waliotoa habari hizo kwa mitume ni: Maria Magdalene, Yoana na Maria mama wa Yakobo, pamoja na wanawake wengine walioandamana nao.
那几名女性为:抹大拉的玛利亚,约亚拿和雅各的母亲玛利亚,以及其他跟随耶稣的妇女。她们把这些事告诉了众门徒。
11 Mitume waliyachukua maneno hayo kama yasiyo na msingi, hivyo hawakuamini.
但他们认为这是无稽之谈,根本不相信她们。
12 Lakini Petro alitoka, akaenda mbio hadi kaburini. Alipoinama kuchungulia ndani, akaiona tu ile sanda. Akarudi nyumbani huku akiwa anashangaa juu ya hayo yaliyotokea.
但彼得还是跑到坟墓那里查看。他弯腰看进去,只看到了坟墓里的细麻布,于是就回去了,对这一切感到非常惊奇。
13 Siku hiyohiyo, wawili kati ya wafuasi wake Yesu wakawa wanakwenda katika kijiji kimoja kiitwacho Emau, umbali wa kilomita kumi na moja kutoka Yerusalemu.
同一天,两名门徒去往一个叫以马午斯的村子,距耶路撒冷大约十一公里。
14 Wakawa wanazungumza juu ya hayo yote yaliyotukia.
他们在路上谈论着所发生的一切。
15 Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akatokea, akatembea pamoja nao.
正在交谈和争辩的时候,耶稣走上前,与他们同行。
16 Walimwona kwa macho, lakini hawakumtambua.
但他们却没有认出他。
17 Akawauliza, “Mnazungumza nini huku mnatembea?” Nao wakasimama kimya, nyuso zao wamezikunja kwa huzuni.
耶稣问到:“你们边走边聊什么呢?”他们就站住,面带愁容。
18 Mmoja, aitwaye Kleopa, akamjibu, “Je, wewe ni mgeni peke yako Yerusalemu ambaye hujui yaliyotukia huko siku hizi?”
一个名叫克利奥帕斯的门徒回答:“你造访耶路撒冷吗?关于那里发生的事情,你可能是唯一不知情的人。”
19 Naye akawajibu, “Mambo gani?” Wao wakamjibu, “Mambo yaliyompata Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii mwenye uwezo wa kutenda na kufundisha mbele ya Mungu na mbele ya watu wote.
耶稣说:“什么事?”他们说:“就是拿撒勒人耶稣的事。他是先知,在上帝和众人面前显示出了伟大的奇迹。
20 Makuhani na watawala wetu walimtoa ahukumiwe kufa, wakamsulubisha.
我们的祭司长和长官竟把他交了出去,把他判了死罪,钉在十字架上。
21 Lakini sisi tulitumaini kwamba yeye ndiye angeikomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu mambo hayo yalipotendeka.
我们一直盼望他就是救赎以色列的那个人。这些事发生到现在已经是第三天了。
22 Tena, wanawake wengine wa kwetu wametushtua. Walikwenda kaburini mapema asubuhi,
但我们中有几名妇女却有了让我们惊讶的发现。她们凌晨到坟墓那里去,
23 wasiukute mwili wake. Wakarudi wakasema kwamba walitokewa na malaika waliowaambia kwamba alikuwa hai.
却找不到他的身体。她们回来说看见天使显现,天使说他已经复活了。
24 Wengine wetu walikwenda kaburini wakashuhudia yale waliyosema hao wanawake; ila yeye hawakumwona.”
我们又有几个人到坟墓那里去看,与妇女们所说的一样,没有看见他。”
25 Kisha Yesu akawaambia, “Mbona mu wapumbavu kiasi hicho na mioyo yenu ni mizito hivyo kusadiki yote yaliyonenwa na manabii?
耶稣说:“迟钝的人呐!对于先知所说的一切,你们信得太迟钝了!
26 Je, haikumpasa Kristo kuteswa, na hivyo aingie katika utukufu wake?”
基督这样受迫害,后来不是迎来了他的荣耀吗?”
27 Akawafafanulia mambo yote yaliyomhusu yeye katika Maandiko Matakatifu kuanzia Mose hadi manabii wote.
于是他从摩西和众先知说起,把所有关于他的经文解释了一遍。
28 Walipokikaribia kile kijiji walikokuwa wanakwenda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea na safari;
他们即将抵达要去的那个村子,耶稣表现得好像是要继续前行,
29 lakini wao wakamsihi wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana kunakuchwa, na usiku unakaribia.” Basi, akaingia kijijini, akakaa pamoja nao.
两名门徒特别想把他留住:“天晚了,太阳下山了,就住在这里吧。”于是耶稣就与他们住在一起。
30 Alipoketi kula chakula pamoja nao, akachukua mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
吃饭的时候,他拿起饼,在感谢上帝后把饼掰开递给那两位门徒,
31 Mara macho yao yakafumbuliwa, wakamtambua; lakini yeye akatoweka kati yao.
他们的眼睛此刻终于看清了,认出这是耶稣,但耶稣却从他们面前消失不见了。
32 Basi, wakaambiana, “Je, mioyo yetu haikuwa inawaka ndani yetu wakati alipokuwa anatufafanulia Maandiko Matakatifu kule njiani?”
他们彼此说:“一路上他和我们说话,给我们解释经文,那时候我们的思想仿佛被火烧灼。”
33 Wakaondoka saa ileile, wakarudi Yerusalemu: wakawakuta wale mitume kumi na mmoja na wale wengine waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika
他们立刻站起来返回耶路撒冷。在那里遇见十一个门徒和其他聚在一起的人。
34 wakisema, “Hakika Bwana amefufuka, amemtokea Simoni.”
这十一位门徒说:“主果然复活了,已经向西门显现。”
35 Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
两个人就把在路上的事,以及掰开饼时如何认出耶稣的事情,讲述了一遍。
36 Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia “Amani kwenu.”
他们正在交谈之际,耶稣现身站在他们当中,说:“愿你们平安。”
37 Wakashtuka na kushikwa na hofu wakidhani wameona mzimu.
他们非常惊怕,以为看见了鬼。
38 Lakini yeye akawaambia, “Kwa nini mnafadhaika? Mbona mnakuwa na mashaka mioyoni mwenu?
耶稣问到:“你们为什么惊恐?为什么心有疑惑?
39 Angalieni mikono na miguu yangu, ya kwamba ni mimi mwenyewe. Nipapaseni mkanione, maana mzimu hauna mwili na mifupa kama mnionavyo.”
你们看我的手脚,就知道我是谁。摸摸我,你们就会更确认,因为鬼没有骨肉,但你们看,我有。”
40 Baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono na miguu.
说了这话,耶稣就把手脚给众人看。
41 Wakiwa bado katika hali ya kutosadiki kwa sababu ya furaha yao, na wakiwa wanastaajabu, akawauliza, “Mnacho chakula chochote hapa?”
众人感到如此狂喜和惊讶,以至于仍然不敢相信这一切。耶稣说:“你们这里有什么食物吗?”
42 Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa.
他们就给了他一片做好的鱼。
43 Akakichukua, akala, wote wakimwona.
他接过来,在他们面前吃了。
44 Halafu akawaambia, “Hii ndiyo maana ya maneno niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi: kwamba ilikuwa lazima kukamilisha yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Mose na katika vitabu vya manabii na katika kitabu cha Zaburi.”
然后耶稣对他们说:“我还和你们在一起时,就是这样对你们解释的:摩西律法、先知书籍和《诗篇》中记载了关于我的一切,都会成真。”
45 Kisha, akaziangazia akili zao ili wapate kuelewa Maandiko Matakatifu.
于是他打开他们的思想,让他们能够理解经书。
46 Akawaambia, “Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka wafu,
他告诉他们:“经上记着‘基督将会受害,第三天死而复生。人们要奉他的名,
47 na kwamba ni lazima, kwa jina lake, mataifa yote kuanzia na Yerusalemu yahubiriwe juu ya kutubu na kusamehewa dhambi.
宣讲悔改与赦罪之道,从耶路撒冷开始,传遍世界各地。’
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo hayo.
你们就是这一切的见证。
49 Nami mwenyewe nitawapelekeeni yule ambaye Baba aliahidi kumtuma, lakini ngojeni huku mjini mpaka mtakapopewa ile nguvu itokayo juu.”
现在我要将天父所承诺的赋予你们。但你们需要在城里等候,直到获得来自天堂的力量。”
50 Kisha akawaongoza nje ya mji hadi Bethania, akainua mikono yake juu, akawabariki.
然后他带他们走出去,走到伯大尼附近时,抬手祝福众人。
51 Alipokuwa anawabariki, akawaacha; akachukuliwa mbinguni.
在祝福的同时离开了他们,被送上天堂。
52 Wao wakamwabudu, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kubwa:
众人开始膜拜他,然后充满喜悦地回到耶路撒冷,
53 wakakaa muda wote Hekaluni wakimsifu Mungu.
此后,他们便始终都在神庙中称颂上帝。

< Luka 24 >