< Luka 23 >

1 Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
Toda la compañía se levantó y le llevó ante Pilato.
2 Wakaanza kumshtaki wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme.”
Comenzaron a acusarle, diciendo: “Hemos encontrado a este hombre pervirtiendo a la nación, prohibiendo pagar los impuestos al César y diciendo que él mismo es el Cristo, un rey.”
3 Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
Pilato le preguntó: “¿Eres tú el rey de los judíos?” Le respondió: “Eso dices tú”.
4 Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, “Sioni kosa lolote katika mtu huyu.”
Pilato dijo a los jefes de los sacerdotes y a la multitud: “No encuentro fundamento para una acusación contra este hombre”.
5 Lakini wao wakasisitiza wakisema: “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa.”
Pero ellos insistieron, diciendo: “Él agita al pueblo, enseñando en toda Judea, comenzando desde Galilea hasta este lugar.”
6 Pilato aliposikia hayo, akauliza, “Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?”
Pero cuando Pilato oyó mencionar a Galilea, preguntó si el hombre era galileo.
7 Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
Al enterarse de que estaba en la jurisdicción de Herodes, lo envió a Herodes, que también estaba en Jerusalén en esos días.
8 Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
Cuando Herodes vio a Jesús, se alegró mucho, pues hacía tiempo que quería verlo, porque había oído hablar mucho de él. Esperaba ver algún milagro hecho por él.
9 Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
Lo interrogó con muchas palabras, pero no le respondió.
10 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
Los jefes de los sacerdotes y los escribas estaban de pie, acusándolo con vehemencia.
11 Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
Herodes y sus soldados lo humillaron y se burlaron de él. Vistiéndolo con ropas lujosas, lo enviaron de vuelta a Pilato.
12 Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
Ese mismo día Herodes y Pilato se hicieron amigos entre sí, pues antes eran enemigos entre sí.
13 Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
Pilato convocó a los jefes de los sacerdotes, a los gobernantes y al pueblo,
14 akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
y les dijo: “Me habéis traído a este hombre como a uno que pervierte al pueblo, y he aquí, habiéndolo examinado delante de vosotros, no he encontrado fundamento para acusar a este hombre de las cosas de que le acusáis.
15 Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
Tampoco lo ha hecho Herodes, pues os he enviado a él, y ved que no ha hecho nada digno de muerte.
16 Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
Por lo tanto, lo castigaré y lo liberaré”.
17 Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
Ahora bien, tenía que soltarles un prisionero en la fiesta.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
Pero todos gritaron juntos, diciendo: “¡Quita a este hombre! Y suéltanos a Barrabás!
19 (Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
que había sido encarcelado por una revuelta en la ciudad y por asesinato.
20 Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
Entonces Pilato les habló de nuevo, queriendo liberar a Jesús,
21 lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
pero ellos gritaron diciendo: “¡Crucifícalo! Crucifícalo!”
22 Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
La tercera vez les dijo: “¿Por qué? ¿Qué mal ha hecho este hombre? No he encontrado en él ningún delito capital. Por tanto, lo castigaré y lo soltaré”.
23 Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
Pero ellos urgían a grandes voces, pidiendo que fuera crucificado. Sus voces y las de los jefes de los sacerdotes prevalecieron.
24 Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
Pilato decretó que se hiciera lo que ellos pedían.
25 Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
Liberó al que habían metido en la cárcel por insurrección y asesinato, por el que pedían, pero entregó a Jesús a la voluntad de ellos.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
Cuando se lo llevaron, agarraron a un tal Simón de Cirene, que venía del campo, y le pusieron la cruz para que la llevara tras Jesús.
27 Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
Le seguía una gran multitud del pueblo, incluidas las mujeres, que también le lloraban y se lamentaban.
28 Yesu akawageukia, akasema, “Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
Pero Jesús, dirigiéndose a ellas, les dijo: “Hijas de Jerusalén, no lloréis por mí, sino llorad por vosotras y por vuestros hijos.
29 Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
Porque he aquí que vienen días en que dirán: ‘Benditas sean las estériles, los vientres que nunca dieron a luz y los pechos que nunca amamantaron’.
30 Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
Entonces comenzarán a decir a los montes: “¡Caigan sobre nosotros!” y a las colinas: “Cúbrannos.
31 Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”
Porque si hacen estas cosas en el árbol verde, ¿qué se hará en el seco?”
32 Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
Había también otros, dos delincuentes, conducidos con él para ser ejecutados.
33 Walipofika mahali paitwapo, “Fuvu la Kichwa,” ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
Cuando llegaron al lugar que se llama “La Calavera”, lo crucificaron allí con los criminales, uno a la derecha y el otro a la izquierda.
34 Yesu akasema, “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya.” Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
Jesús dijo: “Padre, perdónalos, porque no saben lo que hacen”. Repartiendo sus vestidos entre ellos, echaron suertes.
35 Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: “Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!”
El pueblo se quedó mirando. Los jefes que estaban con ellos también se burlaban de él, diciendo: “Ha salvado a otros. Que se salve a sí mismo, si éste es el Cristo de Dios, su elegido”.
36 Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
Los soldados también se burlaron de él, acercándose y ofreciéndole vinagre,
37 wakisema: “Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
y diciendo: “Si eres el Rey de los Judíos, sálvate”.
38 Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: “Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.”
También se escribió sobre él una inscripción en letras de griego, latín y hebreo: “ESTE ES EL REY DE LOS JUDÍOS”.
39 Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: “Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia.”
Uno de los delincuentes ahorcados le insultó diciendo: “¡Si eres el Cristo, sálvate a ti mismo y a nosotros!”.
40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: “Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
Pero el otro contestó, y reprendiéndole le dijo: “¿Ni siquiera temes a Dios, viendo que estás bajo la misma condena?
41 Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
Y nosotros, ciertamente, con justicia, pues recibimos la debida recompensa por nuestras obras, pero este hombre no ha hecho nada malo.”
42 Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.”
Le dijo a Jesús: “Señor, acuérdate de mí cuando vengas a tu Reino”.
43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
Jesús le dijo: “Te aseguro que hoy estarás conmigo en el Paraíso”.
44 Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
Era ya como la hora sexta, y las tinieblas llegaron a toda la tierra hasta la hora novena.
45 na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
El sol se oscureció y el velo del templo se rasgó en dos.
46 Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
Jesús, gritando a gran voz, dijo: “Padre, en tus manos encomiendo mi espíritu”. Dicho esto, expiró.
47 Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”
Cuando el centurión vio lo que se había hecho, glorificó a Dios, diciendo: “Ciertamente éste era un hombre justo.”
48 Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
Toda la multitud que se había reunido para ver esto, al ver lo que se había hecho, volvió a su casa golpeándose el pecho.
49 Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
Todos sus conocidos y las mujeres que le seguían desde Galilea se quedaron a distancia, viendo estas cosas.
50 Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
He aquí que había un hombre llamado José, que era miembro del consejo, hombre bueno y justo
51 Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
(no había consentido su consejo y su obra), de Arimatea, ciudad de los judíos, que también esperaba el Reino de Dios.
52 Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
Este hombre fue a Pilato y pidió el cuerpo de Jesús.
53 Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
Lo bajó, lo envolvió en una tela de lino y lo puso en un sepulcro tallado en piedra, donde nunca se había puesto a nadie.
54 Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
Era el día de la Preparación, y se acercaba el sábado.
55 Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
Las mujeres que habían venido con él desde Galilea le siguieron, y vieron el sepulcro y cómo estaba colocado su cuerpo.
56 Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.
Volvieron y prepararon especias y ungüentos. El sábado descansaron según el mandamiento.

< Luka 23 >