< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
apara ncha kiNvashUnyapUpotsavasya kAla upasthite
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
pradhAnayAjakA adhyAyakAshcha yathA taM hantuM shaknuvanti tathopAyAm acheShTanta kintu lokebhyo bibhyuH|
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
etastin samaye dvAdashashiShyeShu gaNita IShkariyotIyarUDhimAn yo yihUdAstasyAntaHkaraNaM shaitAnAshritatvAt
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
sa gatvA yathA yIshuM teShAM kareShu samarpayituM shaknoti tathA mantraNAM pradhAnayAjakaiH senApatibhishcha saha chakAra|
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
tena te tuShTAstasmai mudrAM dAtuM paNaM chakruH|
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
tataH so NgIkR^itya yathA lokAnAmagochare taM parakareShu samarpayituM shaknoti tathAvakAshaM cheShTitumArebhe|
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
atha kiNvashUnyapUpotmavadine, arthAt yasmin dine nistArotsavasya meSho hantavyastasmin dine
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
yIshuH pitaraM yohana nchAhUya jagAda, yuvAM gatvAsmAkaM bhojanArthaM nistArotsavasya dravyANyAsAdayataM|
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
tadA tau paprachChatuH kuchAsAdayAvo bhavataH kechChA?
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
tadA sovAdIt, nagare praviShTe kashchijjalakumbhamAdAya yuvAM sAkShAt kariShyati sa yanniveshanaM pravishati yuvAmapi tanniveshanaM tatpashchAditvA niveshanapatim iti vAkyaM vadataM,
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
yatrAhaM nistArotsavasya bhojyaM shiShyaiH sArddhaM bhoktuM shaknomi sAtithishAlA kutra? kathAmimAM prabhustvAM pR^ichChati|
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
tataH sa jano dvitIyaprakoShThIyam ekaM shastaM koShThaM darshayiShyati tatra bhojyamAsAdayataM|
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
tatastau gatvA tadvAkyAnusAreNa sarvvaM dR^iShdvA tatra nistArotsavIyaM bhojyamAsAdayAmAsatuH|
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
atha kAla upasthite yIshu rdvAdashabhiH preritaiH saha bhoktumupavishya kathitavAn
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
mama duHkhabhogAt pUrvvaM yubhAbhiH saha nistArotsavasyaitasya bhojyaM bhoktuM mayAtivA nChA kR^itA|
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
yuShmAn vadAmi, yAvatkAlam IshvararAjye bhojanaM na kariShye tAvatkAlam idaM na bhokShye|
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
tadA sa pAnapAtramAdAya Ishvarasya guNAn kIrttayitvA tebhyo datvAvadat, idaM gR^ihlIta yUyaM vibhajya pivata|
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
yuShmAn vadAmi yAvatkAlam IshvararAjatvasya saMsthApanaM na bhavati tAvad drAkShAphalarasaM na pAsyAmi|
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
tataH pUpaM gR^ihItvA IshvaraguNAn kIrttayitvA bha NktA tebhyo datvAvadat, yuShmadarthaM samarpitaM yanmama vapustadidaM, etat karmma mama smaraNArthaM kurudhvaM|
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
atha bhojanAnte tAdR^ishaM pAtraM gR^ihItvAvadat, yuShmatkR^ite pAtitaM yanmama raktaM tena nirNItanavaniyamarUpaM pAnapAtramidaM|
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
pashyata yo mAM parakareShu samarpayiShyati sa mayA saha bhojanAsana upavishati|
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
yathA nirUpitamAste tadanusAreNA manuShyaputrasya gati rbhaviShyati kintu yastaM parakareShu samarpayiShyati tasya santApo bhaviShyati|
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
tadA teShAM ko jana etat karmma kariShyati tat te parasparaM praShTumArebhire|
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
aparaM teShAM ko janaH shreShThatvena gaNayiShyate, atrArthe teShAM vivAdobhavat|
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
asmAt kAraNAt sovadat, anyadeshIyAnAM rAjAnaH prajAnAmupari prabhutvaM kurvvanti dAruNashAsanaM kR^itvApi te bhUpatitvena vikhyAtA bhavanti cha|
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
kintu yuShmAkaM tathA na bhaviShyati, yo yuShmAkaM shreShTho bhaviShyati sa kaniShThavad bhavatu, yashcha mukhyo bhaviShyati sa sevakavadbhavatu|
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
bhojanopaviShTaparichArakayoH kaH shreShThaH? yo bhojanAyopavishati sa kiM shreShTho na bhavati? kintu yuShmAkaM madhye. ahaM parichArakaivAsmi|
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
apara ncha yuyaM mama parIkShAkAle prathamamArabhya mayA saha sthitA
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
etatkAraNAt pitrA yathA madarthaM rAjyamekaM nirUpitaM tathAhamapi yuShmadarthaM rAjyaM nirUpayAmi|
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
tasmAn mama rAjye bhojanAsane cha bhojanapAne kariShyadhve siMhAsaneShUpavishya chesrAyelIyAnAM dvAdashavaMshAnAM vichAraM kariShyadhve|
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
aparaM prabhuruvAcha, he shimon pashya titaunA dhAnyAnIva yuShmAn shaitAn chAlayitum aichChat,
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
kintu tava vishvAsasya lopo yathA na bhavati etat tvadarthaM prArthitaM mayA, tvanmanasi parivarttite cha bhrAtR^iNAM manAMsi sthirIkuru|
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
tadA sovadat, he prabhohaM tvayA sArddhaM kArAM mR^iti ncha yAtuM majjitosmi|
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
tataH sa uvAcha, he pitara tvAM vadAmi, adya kukkuTaravAt pUrvvaM tvaM matparichayaM vAratrayam apahvoShyase|
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
aparaM sa paprachCha, yadA mudrAsampuTaM khAdyapAtraM pAdukA ncha vinA yuShmAn prAhiNavaM tadA yuShmAkaM kasyApi nyUnatAsIt? te prochuH kasyApi na|
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
tadA sovadat kintvidAnIM mudrAsampuTaM khAdyapAtraM vA yasyAsti tena tadgrahItavyaM, yasya cha kR^ipANo nAsti tena svavastraM vikrIya sa kretavyaH|
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
yato yuShmAnahaM vadAmi, aparAdhijanaiH sArddhaM gaNitaH sa bhaviShyati| idaM yachChAstrIyaM vachanaM likhitamasti tanmayi phaliShyati yato mama sambandhIyaM sarvvaM setsyati|
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
tadA te prochuH prabho pashya imau kR^ipANau| tataH sovadad etau yatheShTau|
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
atha sa tasmAdvahi rgatvA svAchArAnusAreNa jaitunanAmAdriM jagAma shiShyAshcha tatpashchAd yayuH|
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
tatropasthAya sa tAnuvAcha, yathA parIkShAyAM na patatha tadarthaM prArthayadhvaM|
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
pashchAt sa tasmAd ekasharakShepAd bahi rgatvA jAnunI pAtayitvA etat prArthayA nchakre,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
he pita ryadi bhavAn sammanyate tarhi kaMsamenaM mamAntikAd dUraya kintu madichChAnurUpaM na tvadichChAnurUpaM bhavatu|
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
tadA tasmai shaktiM dAtuM svargIyadUto darshanaM dadau|
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
pashchAt sotyantaM yAtanayA vyAkulo bhUtvA punardR^iDhaM prArthayA nchakre, tasmAd bR^ihachChoNitabindava iva tasya svedabindavaH pR^ithivyAM patitumArebhire|
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
atha prArthanAta utthAya shiShyANAM samIpametya tAn manoduHkhino nidritAn dR^iShTvAvadat
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
kuto nidrAtha? parIkShAyAm apatanArthaM prarthayadhvaM|
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
etatkathAyAH kathanakAle dvAdashashiShyANAM madhye gaNito yihUdAnAmA janatAsahitasteShAm agre chalitvA yIshoshchumbanArthaM tadantikam Ayayau|
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
tadA yIshuruvAcha, he yihUdA kiM chumbanena manuShyaputraM parakareShu samarpayasi?
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
tadA yadyad ghaTiShyate tadanumAya sa NgibhiruktaM, he prabho vayaM ki kha Ngena ghAtayiShyAmaH?
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
tata ekaH karavAlenAhatya pradhAnayAjakasya dAsasya dakShiNaM karNaM chichCheda|
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
adhUnA nivarttasva ityuktvA yIshustasya shrutiM spR^iShTvA svasyaM chakAra|
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
pashchAd yIshuH samIpasthAn pradhAnayAjakAn mandirasya senApatIn prAchInAMshcha jagAda, yUyaM kR^ipANAn yaShTIMshcha gR^ihItvA mAM kiM choraM dharttumAyAtAH?
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
yadAhaM yuShmAbhiH saha pratidinaM mandire. atiShThaM tadA mAM dharttaM na pravR^ittAH, kintvidAnIM yuShmAkaM samayondhakArasya chAdhipatyamasti|
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
atha te taM dhR^itvA mahAyAjakasya niveshanaM ninyuH| tataH pitaro dUre dUre pashchAditvA
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
bR^ihatkoShThasya madhye yatrAgniM jvAlayitvA lokAH sametyopaviShTAstatra taiH sArddham upavivesha|
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
atha vahnisannidhau samupaveshakAle kAchiddAsI mano nivishya taM nirIkShyAvadat pumAnayaM tasya sa Nge. asthAt|
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
kintu sa tad apahnutyAvAdIt he nAri tamahaM na parichinomi|
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
kShaNAntare. anyajanastaM dR^iShTvAbravIt tvamapi teShAM nikarasyaikajanosi| pitaraH pratyuvAcha he nara nAhamasmi|
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
tataH sArddhadaNDadvayAt paraM punaranyo jano nishchitya babhAShe, eSha tasya sa NgIti satyaM yatoyaM gAlIlIyo lokaH|
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
tadA pitara uvAcha he nara tvaM yad vadami tadahaM boddhuM na shaknomi, iti vAkye kathitamAtre kukkuTo rurAva|
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
tadA prabhuNA vyAdhuTya pitare nirIkShite kR^ikavAkuravAt pUrvvaM mAM trirapahnoShyase iti pUrvvoktaM tasya vAkyaM pitaraH smR^itvA
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
bahirgatvA mahAkhedena chakranda|
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
tadA yai ryIshurdhR^itaste tamupahasya praharttumArebhire|
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
vastreNa tasya dR^ishau baddhvA kapole chapeTAghAtaM kR^itvA paprachChuH, kaste kapole chapeTAghAtaM kR^itavAna? gaNayitvA tad vada|
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
tadanyat tadviruddhaM bahunindAvAkyaM vaktumArebhire|
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
atha prabhAte sati lokaprA nchaH pradhAnayAjakA adhyApakAshcha sabhAM kR^itvA madhyesabhaM yIshumAnIya paprachChuH, tvam abhiShikatosi na vAsmAn vada|
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
sa pratyuvAcha, mayA tasminnukte. api yUyaM na vishvasiShyatha|
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
kasmiMshchidvAkye yuShmAn pR^iShTe. api mAM na taduttaraM vakShyatha na mAM tyakShyatha cha|
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
kintvitaH paraM manujasutaH sarvvashaktimata Ishvarasya dakShiNe pArshve samupavekShyati|
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
tataste paprachChuH, rtiha tvamIshvarasya putraH? sa kathayAmAsa, yUyaM yathArthaM vadatha sa evAhaM|
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
tadA te sarvve kathayAmAsuH, rtiha sAkShye. ansasmin asmAkaM kiM prayojanaM? asya svamukhAdeva sAkShyaM prAptam|

< Luka 22 >