< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
adpropinquabat autem dies festus azymorum qui dicitur pascha
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
et quaerebant principes sacerdotum et scribae quomodo eum interficerent timebant vero plebem
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
intravit autem Satanas in Iudam qui cognominatur Scarioth unum de duodecim
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
et abiit et locutus est cum principibus sacerdotum et magistratibus quemadmodum illum traderet eis
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
et gavisi sunt et pacti sunt pecuniam illi dare
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
et spopondit et quaerebat oportunitatem ut traderet illum sine turbis
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
venit autem dies azymorum in qua necesse erat occidi pascha
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
et misit Petrum et Iohannem dicens euntes parate nobis pascha ut manducemus
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
at illi dixerunt ubi vis paremus
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
et dixit ad eos ecce introeuntibus vobis in civitatem occurret vobis homo amphoram aquae portans sequimini eum in domum in qua intrat
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
et dicetis patri familias domus dicit tibi magister ubi est diversorium ubi pascha cum discipulis meis manducem
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
et ipse vobis ostendet cenaculum magnum stratum et ibi parate
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
euntes autem invenerunt sicut dixit illis et paraverunt pascha
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
et cum facta esset hora discubuit et duodecim apostoli cum eo
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
et ait illis desiderio desideravi hoc pascha manducare vobiscum antequam patiar
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
dico enim vobis quia ex hoc non manducabo illud donec impleatur in regno Dei
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
et accepto calice gratias egit et dixit accipite et dividite inter vos
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
dico enim vobis quod non bibam de generatione vitis donec regnum Dei veniat
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
et accepto pane gratias egit et fregit et dedit eis dicens hoc est corpus meum quod pro vobis datur hoc facite in meam commemorationem
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
similiter et calicem postquam cenavit dicens hic est calix novum testamentum in sanguine meo quod pro vobis funditur
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
verumtamen ecce manus tradentis me mecum est in mensa
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
et quidem Filius hominis secundum quod definitum est vadit verumtamen vae illi homini per quem traditur
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
et ipsi coeperunt quaerere inter se quis esset ex eis qui hoc facturus esset
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
facta est autem et contentio inter eos quis eorum videretur esse maior
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
dixit autem eis reges gentium dominantur eorum et qui potestatem habent super eos benefici vocantur
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
vos autem non sic sed qui maior est in vobis fiat sicut iunior et qui praecessor est sicut ministrator
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
nam quis maior est qui recumbit an qui ministrat nonne qui recumbit ego autem in medio vestrum sum sicut qui ministrat
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
vos autem estis qui permansistis mecum in temptationibus meis
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
et ego dispono vobis sicut disposuit mihi Pater meus regnum
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
ut edatis et bibatis super mensam meam in regno et sedeatis super thronos iudicantes duodecim tribus Israhel
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
ait autem Dominus Simon Simon ecce Satanas expetivit vos ut cribraret sicut triticum
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
ego autem rogavi pro te ut non deficiat fides tua et tu aliquando conversus confirma fratres tuos
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
qui dixit ei Domine tecum paratus sum et in carcerem et in mortem ire
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
et ille dixit dico tibi Petre non cantabit hodie gallus donec ter abneges nosse me
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
et dixit eis quando misi vos sine sacculo et pera et calciamentis numquid aliquid defuit vobis at illi dixerunt nihil
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
dixit ergo eis sed nunc qui habet sacculum tollat similiter et peram et qui non habet vendat tunicam suam et emat gladium
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
dico enim vobis quoniam adhuc hoc quod scriptum est oportet impleri in me et quod cum iniustis deputatus est etenim ea quae sunt de me finem habent
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
at illi dixerunt Domine ecce gladii duo hic at ille dixit eis satis est
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
et egressus ibat secundum consuetudinem in montem Olivarum secuti sunt autem illum et discipuli
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
et cum pervenisset ad locum dixit illis orate ne intretis in temptationem
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
et ipse avulsus est ab eis quantum iactus est lapidis et positis genibus orabat
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
dicens Pater si vis transfer calicem istum a me verumtamen non mea voluntas sed tua fiat
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
apparuit autem illi angelus de caelo confortans eum et factus in agonia prolixius orabat
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
et factus est sudor eius sicut guttae sanguinis decurrentis in terram
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
et cum surrexisset ab oratione et venisset ad discipulos suos invenit eos dormientes prae tristitia
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
et ait illis quid dormitis surgite orate ne intretis in temptationem
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
adhuc eo loquente ecce turba et qui vocabatur Iudas unus de duodecim antecedebat eos et adpropinquavit Iesu ut oscularetur eum
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
Iesus autem dixit ei Iuda osculo Filium hominis tradis
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
videntes autem hii qui circa ipsum erant quod futurum erat dixerunt ei Domine si percutimus in gladio
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
et percussit unus ex illis servum principis sacerdotum et amputavit auriculam eius dextram
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
respondens autem Iesus ait sinite usque huc et cum tetigisset auriculam eius sanavit eum
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
dixit autem Iesus ad eos qui venerant ad se principes sacerdotum et magistratus templi et seniores quasi ad latronem existis cum gladiis et fustibus
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
cum cotidie vobiscum fuerim in templo non extendistis manus in me sed haec est hora vestra et potestas tenebrarum
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
conprehendentes autem eum duxerunt ad domum principis sacerdotum Petrus vero sequebatur a longe
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
accenso autem igni in medio atrio et circumsedentibus illis erat Petrus in medio eorum
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
quem cum vidisset ancilla quaedam sedentem ad lumen et eum fuisset intuita dixit et hic cum illo erat
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
at ille negavit eum dicens mulier non novi illum
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
et post pusillum alius videns eum dixit et tu de illis es Petrus vero ait o homo non sum
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
et intervallo facto quasi horae unius alius quidam adfirmabat dicens vere et hic cum illo erat nam et Galilaeus est
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
et ait Petrus homo nescio quod dicis et continuo adhuc illo loquente cantavit gallus
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
et conversus Dominus respexit Petrum et recordatus est Petrus verbi Domini sicut dixit quia priusquam gallus cantet ter me negabis
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
et egressus foras Petrus flevit amare
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
et viri qui tenebant illum inludebant ei caedentes
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
et velaverunt eum et percutiebant faciem eius et interrogabant eum dicentes prophetiza quis est qui te percussit
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
et alia multa blasphemantes dicebant in eum
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
et ut factus est dies convenerunt seniores plebis et principes sacerdotum et scribae et duxerunt illum in concilium suum dicentes si tu es Christus dic nobis
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
et ait illis si vobis dixero non creditis mihi
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
si autem et interrogavero non respondebitis mihi neque dimittetis
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
ex hoc autem erit Filius hominis sedens a dextris virtutis Dei
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
dixerunt autem omnes tu ergo es Filius Dei qui ait vos dicitis quia ego sum
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
at illi dixerunt quid adhuc desideramus testimonium ipsi enim audivimus de ore eius

< Luka 22 >