< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
Or la fête des pains sans levain, dite la Pâque, approchait,
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
et les grands prêtres et les scribes cherchaient comment ils pourraient se défaire de lui, car ils craignaient le peuple.
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
Or Satan entra dans Judas, nommé Iscariote, qui était du nombre des douze,
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
et il vint conférer avec les grands prêtres et les chefs des gardes sur la manière de le leur livrer.
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
Et ils furent dans la joie, et ils convinrent de lui donner de l'argent,
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
et il s'engagea. Et il cherchait une bonne occasion pour le leur livrer à l'insu de la foule.
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Cependant le jour des pains sans levain arriva, dans lequel il fallait immoler la pâque;
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
et il dépêcha Pierre et Jean en disant: « Allez nous faire les préparatifs nécessaires pour que nous mangions la pâque. »
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
Mais ils lui dirent: « Où veux-tu que nous fassions les préparatifs pour que tu manges la pâque? »
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
Et il leur dit: « Voici, quand vous serez entrés dans la ville, vous rencontrerez un homme portant une cruche d'eau; suivez-le dans la maison où il entrera,
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
et dites au chef de famille: « Le maître te fait dire: Où est la chambre où je dois manger la pâque avec mes disciples? »
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
Et cet homme vous montrera une grande salle à manger garnie de lits; faites-y les préparatifs. »
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
Or s'en étant allés ils trouvèrent tout comme il le leur avait dit, et ils préparèrent la pâque.
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
Et lorsque l'heure fut arrivée, il se mit à table et les apôtres avec lui.
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
Et il leur dit: « J'ai ardemment désiré manger cette pâque avec vous avant ma passion;
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
car je vous déclare que je ne la mangerai certainement plus, jusques à ce qu'elle soit accomplie dans le royaume de Dieu. »
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
Puis, ayant pris une coupe, il dit, après avoir rendu grâces: « Prenez ceci, et distribuez-le entre vous;
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
car je vous déclare que je ne boirai certainement plus désormais du produit de la vigne, jusques à ce que le royaume de Dieu soit venu. »
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
Puis ayant pris du pain, il le rompit, après avoir rendu grâces, et il le leur donna en disant: « Ceci est mon corps, qui est donné pour vous; faites ceci en mémoire de moi; »
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
puis de même la coupe après le repas, en disant: « Cette coupe est la nouvelle alliance en mon sang, qui est versé pour vous.
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
Néanmoins, voici, la main de celui qui me livre est avec moi sur la table;
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
car le fils de l'homme s'en va, il est vrai, selon ce qui a été fixé, néanmoins malheur à cet homme par qui il est livré. »
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
Et ils se mirent à rechercher entre eux quel était donc celui d'entre eux qui devait faire cela.
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
Et il s'éleva encore parmi eux une discussion pour savoir lequel d'entre eux passait pour le plus grand;
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
mais il leur dit: « Les rois des nations les dominent, et leurs potentats sont appelés bienfaiteurs;
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
mais pour vous ne faites pas de même; au contraire, que le plus grand parmi vous devienne comme le plus jeune, et celui qui commande comme celui qui sert;
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
car qui est le plus grand, celui qui est à table ou celui qui sert? N'est-ce pas celui qui est à table? Mais moi je suis au milieu de vous comme celui qui sert.
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
Quant à vous, vous êtes ceux qui sont toujours demeurés avec moi dans mes tentations,
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
et moi, de mon côté, je dispose en votre faveur du royaume, comme mon Père en a disposé en ma faveur,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
afin que vous mangiez et que vous buviez à ma table dans mon royaume, et que vous soyez assis sur des trônes, pour juger les douze tribus d'Israël.
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
Simon, Simon, voici, Satan vous a réclamés pour vous cribler comme le blé;
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
mais moi j'ai prié pour toi, afin que ta foi ne défaille point, et toi, après être une fois revenu, affermis tes frères. »
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
Or il lui dit: « Seigneur, je suis prêt à aller avec toi et en prison et à la mort. »
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
Mais il lui dit: « Pierre, je te le déclare, aujourd'hui le coq ne chantera pas, jusqu'à ce que, par trois fois, tu aies nié que tu me connais. »
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
Et il leur dit: « Quand je vous ai envoyés sans bourse, ni besace, ni sandales, avez-vous manqué de quelque chose? » Et ils dirent: « De rien. »
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
Mais il leur dit: « Maintenant, au contraire, que celui qui a une bourse la prenne, et de même aussi sa besace, et que celui qui n'en a pas vende son manteau et s'achète une épée;
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
car je vous le déclare, il faut que ce passage de l'écriture s'accomplisse en ma personne: « Et c'est parmi des criminels qu'il a été compté; en effet ce qui me concerne va prendre fin. »
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
Mais ils dirent: « Seigneur, voici, il y a ici deux épées. » Or il leur dit: « Cela suffit. »
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
Et étant sorti il s'achemina, selon sa coutume, vers la montagne des Oliviers; or les disciples aussi le suivaient.
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
Mais lorsqu'il fut arrivé en cet endroit, il leur dit: « Priez pour ne pas entrer en tentation. »
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
Et lui-même s'éloigna d'eux à la distance d'environ un jet de pierre, et s'étant mis à genoux, il priait
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
en disant: « Père, si Tu le veux, fais passer cette coupe loin de moi! Toutefois que ce ne soit pas ma volonté, mais la tienne, qui se fasse. » [
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
Or un ange venu du ciel lui apparut pour le fortifier,
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
et étant entré en agonie, il priait avec plus d'instance; mais sa sueur devint comme des gouttes de sang, qui tombaient sur la terre.]
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
Et s'étant levé après sa prière, il vint vers ses disciples qu'il trouva endormis de tristesse,
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
et il leur dit: « Pourquoi dormez-vous? Levez-vous et priez afin que vous n'entriez pas en tentation. »
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
Pendant qu'il parlait encore, voici venir une foule, et le nommé Judas, un des douze, la précédait, et il s'approcha de Jésus pour l'embrasser.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
Mais Jésus lui dit: « Judas, c'est par un baiser que tu livres le fils de l'homme! »
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
Et ceux qui étaient avec lui voyant ce qui allait arriver dirent: « Seigneur, si nous frappions de l'épée? »
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
Et l'un d'entre eux frappa l'esclave du grand prêtre et lui enleva l'oreille droite.
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
Mais Jésus prenant la parole dit: « Attendez que ceci soit fait, » et lui ayant touché l'oreille, il le guérit.
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
Or Jésus dit aux grands prêtres et aux chefs des gardes du temple et aux anciens qui s'étaient portés contre lui: « Vous êtes sortis, comme contre un brigand, avec des épées et des bâtons.
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
Pendant que j'étais chaque jour avec vous dans le temple, vous n'avez pas mis les mains sur moi; mais c'est ici votre heure, et le règne des ténèbres. »
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
Or l'ayant saisi, ils l'emmenèrent, et ils le conduisirent dans la maison du grand, prêtre. Mais Pierre le suivait de loin.
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
Or après qu'ils eurent allumé un feu au milieu de la cour et qu'ils se furent assis ensemble, Pierre se trouvait assis au milieu d'eux.
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
Mais une servante l'ayant vu assis à la lueur du feu et l'ayant regardé fixement, dit: « Celui-ci aussi était avec lui. »
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
Mais lui le nia en disant: « Je ne le connais point, femme! »
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
Et peu après un autre l'ayant vu, dit: « Toi aussi, tu en es. » Mais Pierre dit: « O homme, je n'en suis point! »
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
Et au bout d'environ une heure un autre insistait en disant: « Certainement celui-ci aussi était avec lui; car il est aussi Galiléen. »
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
Mais Pierre dit: « O homme, j'ignore ce dont tu parles. » Et tout à coup, comme il parlait encore, un coq chanta,
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
et le seigneur s'étant retourné regarda Pierre, et Pierre se souvint de la parole du seigneur, qui lui avait dit: « Avant que le coq ait chanté aujourd'hui tu m'auras renié trois fois. »
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
Et étant sorti il pleura amèrement.
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
Et les hommes qui le tenaient le bafouaient après l'avoir frappé,
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
et l'ayant couvert d'un voile, ils l'interrogeaient en disant: « Prophétise! Quel est celui qui t'a frappé? »
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
Et ils disaient contre lui beaucoup d'autres injures.
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
Et lorsque le jour fut venu, le corps des anciens du peuple se réunit ainsi que les grands prêtres et les scribes, et ils l'amenèrent devant leur propre tribunal, en disant: « Si tu es le Christ, dis-le nous. »
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
Mais il leur dit: « Si je vous le disais, vous ne le croiriez certainement pas;
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
si, d'un autre côté, je vous interrogeais, vous ne répondriez certainement pas.
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
Mais désormais le fils de l'homme sera assis à la droite de la puissance de Dieu. «
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
Or ils dirent tous: « Tu es donc le fils de Dieu? » Or il leur dit: « C'est vous-mêmes qui dites que je le suis. »
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
Mais ils dirent: « Qu'avons-nous encore besoin de témoignage, puisque c'est nous-mêmes qui l'avons entendu de sa bouche? »

< Luka 22 >