< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
Now the Feast of Unleavened Bread was drawing near, which is called Passover,
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
and the chief priests and the scribes were looking for a way to get rid of Jesus quietly, for they were afraid of the people.
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
Then Satan entered into Judas, the one called Iscariot, who was numbered among the twelve.
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
He went away and discussed with the chief priests and officers how he might deliver Jesus up to them.
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
They were glad and agreed to give him money.
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
So he accepted the offer and began looking for an opportunity to deliver Jesus up to them in the absence of a crowd.
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Then came the day for the Feast of Unleavened Bread, when the Passover lamb had to be sacrificed.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
Jesus sent Peter and John, saying, “Go prepare the Passover for us, so that we may eat it.”
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
They said to him, “Where do yoʋ want us to prepare it?”
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
He said to them, “Behold, when you enter the city, a man carrying a jug of water will meet you. Follow him into the house he enters
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
and say to the master of the house, ‘The Teacher asks yoʋ, “Where is the guest room where I may eat the Passover with my disciples?”’
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
He will then show you a large upper room that is furnished; prepare it there.”
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
So they went and found it just as Jesus had told them, and they prepared the Passover.
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
When the hour came, Jesus reclined at the table, and the twelve apostles were with him.
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
He said to them, “I have earnestly desired to eat this Passover with you before I suffer.
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
For I tell you that I will certainly not eat it again until it is fulfilled in the kingdom of God.”
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
Then he took a cup, and after giving thanks he said, “Take this and divide it among yourselves.
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
For I tell you, I will certainly not drink again from the fruit of the vine until the kingdom of God comes.”
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
Then he took bread, and when he had given thanks, he broke it and gave it to them, saying, “This is my body, which is given for you. Do this in remembrance of me.”
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
In the same way, he also took the cup after they had eaten supper, saying, “This cup is the new covenant in my blood, which is poured out for you.
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
But behold, the hand of the one who is going to betray me is with mine on the table.
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
The Son of Man indeed goes as it has been determined, but woe to that man by whom he is betrayed.”
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
Then they began to discuss with one another which one of them it could be who would do this.
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
A dispute also arose among them as to which of them was considered to be greater.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
So Jesus said to them, “The kings of the Gentiles exercise lordship over them, and those who have authority over them are called benefactors.
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
But it must not be so with you; rather the greatest among you must become like the youngest, and the leader must become like one who serves.
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
For who is greater? The one who reclines at the table or the one who serves? Is it not the one who reclines at the table? But I am among you as one who serves.
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
“You have stayed with me in my trials.
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
And I bestow on you a kingdom, just as my Father bestowed one on me,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
so that you may eat and drink at my table. And you will sit on thrones judging the twelve tribes of Israel.”
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
Then the Lord said, “Simon, Simon, behold, Satan has demanded to have you, so that he might sift you like wheat.
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
But I have prayed for yoʋ that yoʋr faith may not fail. Once yoʋ have turned back, strengthen yoʋr brothers.”
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
Peter said to him, “Lord, I am ready to go with yoʋ both to prison and to death.”
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
Jesus said, “I tell yoʋ, Peter, a rooster will certainly not crow today before yoʋ have denied three times that yoʋ know me.”
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
Then Jesus said to them, “When I sent you without a moneybag, knapsack, or sandals, did you lack anything?” They said, “Nothing.”
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
Then he said to them, “But now he who has a moneybag must take it, and likewise a knapsack. And he who does not have a sword must sell his garment and buy one.
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
For I tell you that this Scripture must still be fulfilled in me: ‘He was numbered with the lawless.’ For what is written about me is reaching its fulfillment.”
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
So they said, “Lord, behold, here are two swords.” He said to them, “That is enough!”
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
Then Jesus went out and made his way to the Mount of Olives, as was his custom, and his disciples followed him.
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
When he came to the place, he said to them, “Pray that you may not enter into temptation.”
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
Then he withdrew from them about a stone's throw away and knelt down and prayed,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
“Father, if yoʋ are willing to take this cup away from me, do so; nevertheless, not my will, but yoʋrs be done.”
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
Then an angel from heaven appeared to him and strengthened him.
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
Being in agony, he prayed more earnestly, and his sweat became like drops of blood falling to the ground.
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
When he rose from prayer and came to the disciples, he found them sleeping because of their sorrow.
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
So he said to them, “Why are you sleeping? Rise and pray, lest you enter into temptation.”
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
While he was still speaking, behold, a crowd approached, and the man called Judas, one of the twelve, was leading them. He drew near to Jesus to kiss him,
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
and Jesus said to him, “Judas, are you betraying the Son of Man with a kiss?”
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
When those who were around him saw what was about to happen, they said to him, “Lord, shall we strike with the sword?”
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
Then one of them struck the servant of the high priest and cut off his right ear.
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
But Jesus responded, “No more of this!” And he touched the man's ear and healed him.
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
Then Jesus said to the chief priests, the officers of the temple, and the elders who had come out against him, “Have you come out with swords and clubs as you would against a robber?
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
I was with you daily in the temple courts, and you did not lay a hand on me. But this is your hour, when the power of darkness reigns.”
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
Then they arrested him, led him away, and brought him to the house of the high priest, and Peter was following at a distance.
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
Some there had kindled a fire in the middle of the courtyard and sat down together, and Peter sat down among them.
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
When a servant girl saw him sitting in the light of the fire, she looked at him intently and said, “This man also was with him.”
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
But Peter denied him, saying, “Woman, I do not know him.”
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
After a little while, someone else saw him and said, “Yoʋ also are one of them.” But Peter said, “Man, I am not.”
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
After about an hour had gone by, another man kept insisting, “Truly this man also was with him, for he too is a Galilean.”
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
But Peter said, “Man, I do not know what yoʋ are talking about!” And immediately, while he was still speaking, a rooster crowed.
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Then the Lord turned and looked at Peter, and Peter remembered what the Lord had said to him, “Before a rooster crows, yoʋ will deny me three times.”
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
And Peter went out and wept bitterly.
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
Now the men who were holding Jesus in custody began mocking him and beating him.
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
They also blindfolded him and kept striking his face, saying to him, “Prophesy! Who is it that struck yoʋ?”
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
And they said many other things against him, reviling him.
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
When daybreak came, the elders of the people gathered together, both chief priests and scribes, and they led Jesus up to their Sanhedrin and said,
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
“If yoʋ are the Christ, tell us.” But he said to them, “If I tell you, you will surely not believe.
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
And if I ask you a question, you will surely not answer me or release me.
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
But from now on the Son of Man will be seated at the right hand of the power of God.”
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
So they all said, “Are yoʋ then the Son of God?” He said to them, “You yourselves say that I am.”
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
Then they said, “What further need do we have of testimony? For we ourselves have heard it from his own mouth.”

< Luka 22 >