< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
And the feast of the unleavened bread, which is called a Passover, was drawing near.
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
And the High-priests and the Scribes were seeking, how they might get rid of him; for they feared the people.
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
But Satan entered into Judas, him called Iscariot, being of the number of the twelve;
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
and, departing, he conversed with the High-priests and Captains, as to how, unto them, he might deliver him up.
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
And they rejoiced, and bargained with him to give him, silver;
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
and he freely consented, and began seeking a good opportunity for delivering him up, in the absence of a multitude, unto them.
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Now the day of the unleavened bread a came, —on which it was needful to be sacrificing the passover.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
And he sent forth Peter and John, saying—Go, and make ready, for us, the passover, that we may eat.
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
And, they, said unto him—Where wiliest thou, we should make ready?
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
And, he, said unto them—Lo! when ye have entered into the city, there will meet you a man, bearing, an earthen-jar of water: follow him into the house into which he is entering.
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
And ye shall say unto the master of the house—The teacher saith unto thee, where is the lodging, where, the passover, with my disciples, I may eat?
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
And, he, unto you, will shew, a large upper room, spread: there, make ready.
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
And, departing, they found according as he had said unto them, and made ready the passover.
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
And, when the hour arrived, he reclined, and the apostles with him.
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
And he said unto them—I have greatly desired, to eat, this passover, with you before I suffer;
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
For, I say unto you—In nowise shall I eat it, until it have been fulfilled in the kingdom of God.
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
And, accepting a cup, giving thanks, he said—Take this, and divide among yourselves;
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
For, I say unto you—In nowise shall I drink henceforth of the fruit of the vine, until, the kingdom of God, shall come.
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
And, taking a loaf, he gave thanks, and brake, and gave unto them, saying—This is my body which in your behalf is being given: this, be ye doing, in remembrance, of me.
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
And—the cup, in like manner, after the taking of supper, saying—This cup, is the new covenant in my blood, which, in your behalf, is to be poured out.
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
Nevertheless, lo! the hand of him who is delivering me up, is with me upon the table.
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
Because, the Son of Man, indeed, according to what is marked out, goeth his way; nevertheless, alas! for that man through whom he is being delivered up.
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
And, they, began to be enquiring together, among themselves, as to which, then, it could be, from among them, who, this thing, was about to perpetrate!
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
And it came to pass that there was, a rivalry also, among them, as to which of them seemed to be greater [than the rest].
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
And, he, said unto them—The kings of the nations, lord it over them, and, they who wield authority over them, benefactors, are called.
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
But, ye, not so! On the contrary—the greater among you, Let him become as, the younger, and, he that governeth, as, he that ministereth,
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
For which is greater—he that reclineth? or he that ministereth? Is not he that reclineth? But, I, am, in your midst, as he that ministereth,
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
Ye, however, are they who have remained throughout with me in my temptations;
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
And, I, covenant unto you—as my Father hath covenanted unto me—a kingdom,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
That ye may eat and drink, at my table, in my kingdom, and sit upon thrones, judging, the twelve tribes of Israel.
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
Simon! Simon! lo! Satan, hath claimed you, to sift as wheat;
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
But, I, have entreated for thee, that thy faith may not fail. And, thou, once thou hast turned, strengthen thy brethren.
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
But, he, said unto him—Lord! with thee, am I, ready, both into prison and unto death, to be going.
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
And, he, said: I tell thee, Peter—A cock will not crow this day, until, thrice, thou deny that thou knowest me.
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
And he said unto them—When I sent you forth, without purse or satchel or sandals, of anything, came ye short? And, they, said—Of nothing!
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
And he said unto them—But, now, he that hath a purse, let him take it, in like manner also, a satchel; and, he that hath nothing, let him sell his mantle, and buy a sword!
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
For I say unto you—This that is written, must needs be completed in me, —And, with lawless ones, was he reckoned; for, even that which concerneth me, hath, completion.
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
And, they, said—Lord, lo! two swords, here! And, he, said unto them—’Tis, enough!
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
And going out, he went, according to his custom, unto the Mount of Olives; and the disciples [also] followed him.
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
And, coming up to the place, he said unto them—Be praying, lest ye enter into temptation.
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
And, he, was torn from them about a stone’s throw; and, bending his knees, he began to pray,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
saying—Father! if thou please, bear aside this cup from me. Nevertheless, not my will, but thine, be accomplished.
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
And there appeared unto him a messenger from heaven, strengthening him, —
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
and, coming to be in an agony, more intensely, was he praying; and his perspiration became, as if great drops of blood, falling upon the ground.
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
And, arising from prayer, he came unto his disciples, and found them falling asleep by reason of their grief;
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
and he said unto them—Why are ye slumbering? Arise! and be praying, lest ye enter into temptation.
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
While yet he was speaking, lo! a multitude; and, he that was called Judas, one of the twelve, was leading them on, —and he drew near unto Jesus, to kiss him.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
But, Jesus, said to him—Judas! with a kiss, the Son of Man, dost thou deliver up?
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
And they who were about him, seeing what would be, said—Lord! shall we smite with the sword?
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
And a certain one from among them smote, the High-priest’s, servant, and took off his right ear.
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
But Jesus, answering, said—Let be—as long as this! …And, touching the ear, he healed him.
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
And Jesus said unto the High-priests, and Captains of the temple, and Elders, who had come against him—As against a robber, have ye come out, with swords and clubs?
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
Daily, was I with you, in the temple, and yet ye stretched not forth your hands against me! …But, this, is your hour, and the authority of darkness.
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
And, having arrested him, they led him away, and took him into the house of the High-priest; and, Peter, was following afar.
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
And, they having kindled up a fire in the midst of the court, and taken seats together, Peter was for sitting among them.
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
But, a certain maid-servant, seeing him seating himself towards the light, and looking steadfastly at him, said—This one also, was, with him.
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
But, he, denied, saying—I know him not, woman!
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
And, after a little, another, beholding him, said—Thou also, art, from among them. But, Peter, said—Man! I am not.
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
And, about one hour having passed, a certain other, began stoutly to insist, saying—Of a truth, this one also, was with him; for indeed he is, a Galilaean.
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
But Peter said—Man! I know not what thou art saying! And, instantly while yet he was speaking, a cock crew.
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
And the Lord turned, and looked at Peter; and Peter was put in mind of the declaration of the Lord, how he had said to him—Before, a cock, crow this day, thou wilt deny me thrice!
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
[And, going forth outside, he wept bitterly.]
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
And, the men who held him bound, kept mocking him, with blows;
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
and, blindfolding him, questioned him, saying—Prophesy! which is he that smote thee?
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
and, many other things, with profane speech, were they saying unto him.
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
And, when it became day, the Eldership of the people was gathered together—both High-priests and Scribes, —and they led him away into their high-council, saying—If, thou, art the Christ, tell us!
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
But he said unto them—If I should tell, you, in nowise would ye believe,
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
And, if I should put questions, in nowise would ye answer;
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
But, henceforth, shall the Son of Man be seated on the right hand of the power of God.
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
And they all said—Thou, then, art the Son of God? And, he, unto them said—Ye, say [it], —because, I, am.
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
And, they, said—What, further, need have we, of witness? We ourselves, have heard it from his mouth.

< Luka 22 >