< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
Now the feast of vnleauened bread drewe neere, which is called the Passeouer.
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
And the hie Priests and Scribes sought how they might kill him: for they feared the people.
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
Then entred Satan into Iudas, who was called Iscariot, and was of the nomber of the twelue.
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
And he went his way, and communed with the hie Priestes and captaines, how he might betray him to them.
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
So they were glad, and agreed to giue him money.
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
And he consented, and sought opportunitie to betraye him vnto them, when the people were away.
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Then came the day of vnleauened bread, when the Passeouer must be sacrificed.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
And he sent Peter and Iohn, saying, Go and prepare vs the Passeouer, that we may eate it.
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
And they saide to him, Where wilt thou, that we prepare it?
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
Then he said vnto them, Beholde, when ye be entred into the citie, there shall a man meete you, bearing a pitcher of water: folowe him into the house that he entreth in,
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
And say vnto the good man of the house, The Master saith vnto thee, Where is the lodging where I shall eate my Passeouer with my disciples?
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
Then he shall shewe you a great hie chamber trimmed: there make it ready.
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
So they went, and found as he had said vnto them, and made readie the Passeouer.
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
And when the houre was come, hee sate downe, and the twelue Apostles with him.
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
Then he saide vnto them, I haue earnestly desired to eate this Passeouer with you, before I suffer.
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
For I say vnto you, Hencefoorth I will not eate of it any more, vntill it bee fulfilled in the kingdome of God.
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
And hee tooke the cup, and gaue thankes, and said, Take this, and deuide it among you,
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
For I say vnto you, I will not drinke of the fruite of the vine, vntill the kingdome of God be come.
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
And he tooke bread, and when he had giuen thankes, he brake it, and gaue to them, saying, This is my body, which is giuen for you: doe this in the remembrance of me.
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
Likewise also after supper he tooke the cup, saying, This cup is that newe Testament in my blood, which is shed for you.
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
Yet beholde, the hand of him that betrayeth me, is with me at the table.
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
And truely the Sonne of man goeth as it is appointed: but woe be to that man, by whom he is betrayed.
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
Then they began to enquire among themselues which of them it should be, that should do that.
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
And there arose also a strife among them, which of them should seeme to be ye greatest.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
But hee saide vnto them, The Kings of the Gentiles reigne ouer them, and they that beare rule ouer them, are called bountifull.
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
But yee shall not be so: but let the greatest among you be as the least: and the chiefest as he that serueth.
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
For who is greater, he that sitteth at table, or he that serueth? Is not he that sitteth at table? And I am among you as he that serueth.
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
And yee are they which haue continued with me in my tentations.
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
Therefore I appoint vnto you a kingdome, as my Father hath appointed vnto me,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
That ye may eate, and drinke at my table in my kingdome, and sit on seates, and iudge the twelue tribes of Israel.
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
And the Lord saide, Simon, Simon, beholde, Satan hath desired you, to winowe you as wheate.
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
But I haue prayed for thee, that thy faith faile not: therefore when thou art conuerted, strengthen thy brethren.
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
And he said vnto him, Lord, I am ready to goe with thee into prison, and to death.
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
But he said, I tell thee, Peter, the cocke shall not crowe this day, before thou hast thrise denied that thou knewest me.
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
And he saide vnto them, When I sent you without bagge, and scrip, and shooes, lacked ye any thing? And they said, Nothing.
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
Then he said to them, But nowe he that hath a bagge, let him take it, and likewise a scrip: and hee that hath none, let him sell his coate, and buy a sworde.
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
For I say vnto you, That yet the same which is written, must be perfourmed in me, Euen with the wicked was he nombred: for doubtlesse those things which are written of me, haue an ende.
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
And they said, Lord, beholde, here are two swordes. And he said vnto them, It is ynough.
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
And he came out, and went (as he was wont) to the mount of Oliues: and his disciples also followed him.
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
And when hee came to the place, hee said to them, Pray, lest ye enter into tentation.
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
And he was drawen aside from them about a stones cast, and kneeled downe, and prayed,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
Saying, Father, if thou wilt, take away this cuppe from mee: neuerthelesse, not my will, but thine be done.
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
And there appeared an Angell vnto him from heauen, comforting him.
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
But being in an agonie, hee prayed more earnestly: and his sweate was like drops of blood, trickling downe to the ground.
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
And he rose vp from prayer, and came to his disciples, and found them sleeping for heauinesse.
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
And he said vnto them, Why sleepe ye? rise and pray, least ye enter into tentation.
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
And while he yet spake, beholde, a companie, and he that was called Iudas one of the twelue, went before them, and came neere vnto Iesus to kisse him.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
And Iesus saide vnto him, Iudas, betrayest thou the Sonne of man with a kisse?
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
Now when they which were about him, saw what would follow, they said vnto him, Lord, shall we smite with sworde?
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
And one of them smote a seruant of the hie Priest, and strooke off his right eare.
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
Then Iesus answered, and said, Suffer them thus farre: and he touched his eare, and healed him.
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
Then Iesus said vnto the hie Priests, and captaines of the Temple, and the Elders which were come to him, Bee ye come out as vnto a theefe with swordes and staues?
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
When I was dayly with you in the Temple, yee stretched not foorth the handes against mee: but this is your very houre, and the power of darkenesse.
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
Then tooke they him, and led him, and brought him to the hie Priestes house. And Peter followed afarre off.
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
And when they had kindled a fire in the middes of the hall, and were set downe together, Peter also sate downe among them.
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
And a certaine mayde behelde him as hee sate by the fire, and hauing well looked on him, said, This man was also with him.
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
But he denied him, saying, Woman, I know him not.
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
And after a little while, another man sawe him, and saide, Thou art also of them. But Peter said, Man, I am not.
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
And about the space of an houre after, a certaine other affirmed, saying. Verely euen this man was with him: for he is also a Galilean.
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
And Peter saide, Man, I knowe not what thou sayest. And immediatly while hee yet spake, the cocke crewe.
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Then the Lord turned backe, and looked vpon Peter: and Peter remembred the worde of the Lord, how he had said vnto him, Before the cocke crowe, thou shalt denie me thrise.
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
And Peter went out, and wept bitterly.
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
And the men that helde Iesus, mocked him, and strooke him.
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
And when they had blindfolded him, they smote him on the face, and asked him, saying, Prophecie who it is that smote thee.
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
And many other thinges blasphemously spake they against him.
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
And assoone as it was day, the Elders of the people, and the hie Priests and the Scribes came together, and led him into their councill,
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
Saying, Art thou that Christ? tell vs. And he said vnto them, If I tell you, ye wil not beleeue it.
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
And if also I aske you, you will not answere me, nor let me goe.
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
Hereafter shall the Sonne of man sit at the right hand of the power of God.
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
Then sayd they all, Art thou then ye Sonne of God? And he sayd to them, Ye say, that I am.
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
Then sayd they, What neede we any further witnes? for we our selues haue heard it of his owne mouth.

< Luka 22 >