< Luka 22 >

1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
除酵节(又名逾越节)近了。
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
祭司长和文士想法子怎么才能杀害耶稣,是因他们惧怕百姓。
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
这时,撒但入了那称为加略人犹大的心;他本是十二门徒里的一个。
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
他去和祭司长并守殿官商量,怎么可以把耶稣交给他们。
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
他们欢喜,就约定给他银子。
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
他应允了,就找机会,要趁众人不在跟前的时候把耶稣交给他们。
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
除酵节,须宰逾越羊羔的那一天到了。
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
耶稣打发彼得、约翰,说:“你们去为我们预备逾越节的筵席,好叫我们吃。”
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
他们问他说:“要我们在哪里预备?”
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
耶稣说:“你们进了城,必有人拿着一瓶水迎面而来,你们就跟着他,到他所进的房子里去,
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
对那家的主人说:‘夫子说:客房在哪里?我与门徒好在那里吃逾越节的筵席。’
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
他必指给你们摆设整齐的一间大楼,你们就在那里预备。”
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
他们去了,所遇见的正如耶稣所说的;他们就预备了逾越节的筵席。
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
时候到了,耶稣坐席,使徒也和他同坐。
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
耶稣对他们说:“我很愿意在受害以先和你们吃这逾越节的筵席。
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
我告诉你们,我不再吃这筵席,直到成就在 神的国里。”
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
耶稣接过杯来,祝谢了,说:“你们拿这个,大家分着喝。
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
我告诉你们,从今以后,我不再喝这葡萄汁,直等 神的国来到。”
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
又拿起饼来,祝谢了,就擘开,递给他们,说:“这是我的身体,为你们舍的,你们也应当如此行,为的是记念我。”
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
饭后也照样拿起杯来,说:“这杯是用我血所立的新约,是为你们流出来的。
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
看哪,那卖我之人的手与我一同在桌子上。
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
人子固然要照所预定的去世,但卖人子的人有祸了!”
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
他们就彼此对问,是哪一个要做这事。
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
门徒起了争论,他们中间哪一个可算为大。
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
耶稣说:“外邦人有君王为主治理他们,那掌权管他们的称为恩主。
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
但你们不可这样;你们里头为大的,倒要像年幼的,为首领的,倒要像服事人的。
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
是谁为大?是坐席的呢?是服事人的呢?不是坐席的大吗?然而,我在你们中间如同服事人的。
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
我在磨炼之中,常和我同在的就是你们。
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
我将国赐给你们,正如我父赐给我一样,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
叫你们在我国里,坐在我的席上吃喝,并且坐在宝座上,审判以色列十二个支派。”
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
主又说:“西门!西门!撒但想要得着你们,好筛你们像筛麦子一样;
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
但我已经为你祈求,叫你不至于失了信心。你回头以后,要坚固你的弟兄。”
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
彼得说:“主啊,我就是同你下监,同你受死,也是甘心!”
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
耶稣说:“彼得,我告诉你,今日鸡还没有叫,你要三次说不认得我。”
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
耶稣又对他们说:“我差你们出去的时候,没有钱囊,没有口袋,没有鞋,你们缺少什么没有?”他们说:“没有。”
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
耶稣说:“但如今有钱囊的可以带着,有口袋的也可以带着,没有刀的要卖衣服买刀。
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
我告诉你们,经上写着说:‘他被列在罪犯之中。’这话必应验在我身上,因为那关系我的事必然成就。”
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
他们说:“主啊,请看!这里有两把刀。”耶稣说:“够了。”
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
耶稣出来,照常往橄榄山去,门徒也跟随他。
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
到了那地方,就对他们说:“你们要祷告,免得入了迷惑。”
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
于是离开他们约有扔一块石头那么远,跪下祷告,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
说:“父啊!你若愿意,就把这杯撤去;然而,不要成就我的意思,只要成就你的意思。”
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
有一位天使从天上显现,加添他的力量。
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
耶稣极其伤痛,祷告更加恳切,汗珠如大血点滴在地上。
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
祷告完了,就起来,到门徒那里,见他们因为忧愁都睡着了,
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
就对他们说:“你们为什么睡觉呢?起来祷告,免得入了迷惑!”
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
说话之间,来了许多人。那十二个门徒里名叫犹大的,走在前头,就近耶稣,要与他亲嘴。
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
耶稣对他说:“犹大!你用亲嘴的暗号卖人子吗?”
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
左右的人见光景不好,就说:“主啊!我们拿刀砍可以不可以?”
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
内中有一个人把大祭司的仆人砍了一刀,削掉了他的右耳。
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
耶稣说:“到了这个地步,由他们吧!”就摸那人的耳朵,把他治好了。
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
耶稣对那些来拿他的祭司长和守殿官并长老说:“你们带着刀棒出来拿我,如同拿强盗吗?
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
我天天同你们在殿里,你们不下手拿我。现在却是你们的时候,黑暗掌权了。”
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
他们拿住耶稣,把他带到大祭司的宅里。彼得远远地跟着。
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
他们在院子里生了火,一同坐着;彼得也坐在他们中间。
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
有一个使女看见彼得坐在火光里,就定睛看他,说:“这个人素来也是同那人一伙的。”
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
彼得却不承认,说:“女子,我不认得他。”
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
过了不多的时候,又有一个人看见他,说:“你也是他们一党的。”彼得说:“你这个人!我不是。”
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
约过了一小时,又有一个人极力地说:“他实在是同那人一伙的,因为他也是加利利人。”
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
彼得说:“你这个人!我不晓得你说的是什么!”正说话之间,鸡就叫了。
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
主转过身来看彼得,彼得便想起主对他所说的话:“今日鸡叫以先,你要三次不认我。”
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
他就出去痛哭。
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
看守耶稣的人戏弄他,打他,
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
又蒙着他的眼,问他说:“你是先知,告诉我们打你的是谁?”
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
他们还用许多别的话辱骂他。
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
天一亮,民间的众长老连祭司长带文士都聚会,把耶稣带到他们的公会里,
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
说:“你若是基督,就告诉我们。”耶稣说:“我若告诉你们,你们也不信;
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
我若问你们,你们也不回答。
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
从今以后,人子要坐在 神权能的右边。”
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
他们都说:“这样,你是 神的儿子吗?”耶稣说:“你们所说的是。”
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
他们说:“何必再用见证呢?他亲口所说的,我们都亲自听见了。”

< Luka 22 >