< Luka 21 >

1 Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
Having looked up now He saw the ones casting into the treasury the gifts of them rich.
2 akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
He saw then (and *k) a certain widow poor casting in lepta two.
3 Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
And He said; Truly I say to you that widow this poor more than all has cast in;
4 Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
(all *N+kO) for these out of that which was abounding to them they cast in the gifts (of God *KO) she however out of the poverty of her (all *N+kO) the livelihood that she had did cast.
5 Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
And as some were speaking about the temple that with stones goodly and with consecrated gifts it has been adorned He said;
6 “Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
[As to] these things which you are beholding, will come [the] days in which not will be left stone upon stone (here *O) which not will be thrown down.
7 Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
They asked then Him saying; Teacher, when then these things will be and what [will be] the sign when may soon be these things to take place?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
And He said; do take heed lest you may be led astray; many for will come in the name of Me saying (that: *ko) I myself am [He], and The time has drawn near. Not (therefore *K) may go after them.
9 Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
When then you may hear of wars and commotions, not may be terrified; it behooves for these things to take place first but not immediately [is] the end.
10 Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
Then He was saying to them; Will rise up nation against nation and kingdom against kingdom,
11 Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
Earthquakes both great and in different places famines and pestilences there will be, fearful sights also and from heaven signs great will there be.
12 Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
Before however these things (all *N+kO) they will lay upon you the hands of them and will persecute [you] delivering [you] to (the *no) synagogues and prisons, (leading [you] *N+kO) before kings and governors on account of the name of Me.
13 Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
It will result (now *ko) to you for a testimony.
14 Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
(do implant *N+kO) therefore (in the hearts *N+kO) of you not to premeditate to present a defense;
15 kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
I myself for will give you a mouth and wisdom which not will be able to resist (nor *N+kO) to reply to (all *N+kO) those opposing you.
16 Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
You will be betrayed then even by parents and brothers and relatives and friends and they will put to death [some] from among you.
17 Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
And you will be hated by all because of the name of Me.
18 Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
But a hair of the head of you certainly not may perish.
19 Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
By the patient endurance of you [all] (do you gain yourselves *NK+o) the souls of you [all].
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
When then you may see being encircled by encampments Jerusalem, then do know that has drawn near the desolation of her.
21 Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
Then those in Judea they should flee to the mountains, and those in midst of her they should depart out, and those in the countries not they should enter into her.
22 Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
for [the] days of avenging these are (to fill *N+kO) all things which written.
23 Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
But woe (now *k) to those in womb [pregnancy] having and to the [ones] nursing in those the days; there will be for distress great upon the land and wrath (in *k) to the people this,
24 Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
And they will fall by [the] edge of [the] sword and will be led captive into the nations all and Jerusalem will be trodden down by [the] Gentiles until (that *no) may be fulfilled (and will be *O) [the] times of [the] Gentiles.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
And (there will be *N+kO) signs in sun and moon and stars, and upon the earth distress of nations with perplexity ([the] sound *N+kO) of [the] sea and rolling surge
26 Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
when are fainting men from fear and expectation of that which is coming on the earth; for the powers of the heavens will be shaken.
27 Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
And then will they behold the Son of Man coming in a cloud with power and glory great.
28 Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
Beginning then of these things to come to pass do look up and do lift up the heads of you because draws near the redemption of you.
29 Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
And He spoke a parable to them: Behold the fig tree and all the trees.
30 Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
When they may sprout already, looking [on them] for yourselves you know that already near the summer is.
31 Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So also you yourselves when you may see these things coming to pass, do know that near is the kingdom of God.
32 Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
Amen I say to you that certainly not may have passed away generation this until when all [these things] may happen.
33 Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
The heaven and the earth (will pass away, *NK+o) but the words of Mine certainly not (will pass away. *N+kO)
34 “Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
do take heed now to yourselves otherwise otherwise (may be burdened *N+kO) of you the hearts with dissipation and drunkenness and cares of life — and may come upon you suddenly day that [very]
35 Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
as a snare; (It will enter *N+kO) for upon all those sitting upon [the] face of all the earth.
36 Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
do watch (also *N+KO) at every season praying that (you may have strength *N+KO) to escape these things all that are soon to come to pass and to stand before the Son of Man.
37 Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
He was now during the day in the temple teaching. and the evening going out He was lodging on the mount which is being called Olivet.
38 Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
And all the group of people was coming early to Him in the temple to hear Him.

< Luka 21 >