< Luka 21 >

1 Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
He looked up, and saw the rich people who were putting their gifts into the treasury.
2 akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
He saw a certain poor widow casting in two small bronze coins.
3 Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
He said, “Truly I tell you, this poor widow put in more than all of them,
4 Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
for all these put in gifts for God from their abundance, but she, out of her poverty, put in all that she had to live on.”
5 Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
As some were talking about the temple and how it was decorated with beautiful stones and gifts, he said,
6 “Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
“As for these things which you see, the days will come, in which there will not be left here one stone on another that will not be thrown down.”
7 Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
They asked him, “Teacher, so when will these things be? What is the sign that these things are about to happen?”
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
He said, “Watch out that you don’t get led astray, for many will come in my name, saying, ‘Ena Na [I AM (the Living God)], I am he,’ and, ‘The time is at hand.’ Therefore don’t follow them.
9 Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
When you hear of wars and disturbances, don’t be terrified, for these things must happen first, but the end won’t come immediately.”
10 Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
Then he said to them, “Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom.
11 Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
There will be great earthquakes, famines, and plagues in various places. There will be terrors and great signs from heaven.
12 Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
But before all these things, they will lay their hands on you and will persecute you, delivering you up to synagogues and prisons, bringing you before kings and governors for my name’s sake.
13 Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
It will turn out as a testimony for you.
14 Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
Settle it therefore in your hearts not to meditate beforehand how to answer,
15 kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
for I will give you a mouth and wisdom which all your adversaries will not be able to withstand or to contradict.
16 Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
You will be handed over even by parents, brothers, relatives, and friends. They will cause some of you to be put to death.
17 Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
You will be hated by all men for my name’s sake.
18 Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
And not a hair of your head will perish.
19 Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
“By your endurance you will win your lives.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
“But when you see Jerusalem [City of peace] surrounded by armies, then know that its desolation is at hand.
21 Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
Then let those who are in Judea [Praise] flee to the mountains. Let those who are in the middle of her depart. Let those who are in the country not enter therein.
22 Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
For these are days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
Woe to those who are pregnant and to those who nurse infants in those days! For there will be great distress in the land, and wrath to this people.
24 Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
They will fall by the edge of the sword, and will be led captive into all the nations. Jerusalem [City of peace] will be trampled down by the Gentiles, until the times of the Gentiles are fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
There will be signs in the sun, moon, and stars; and on the earth anxiety of nations, in perplexity for the roaring of the sea and the waves;
26 Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
men fainting for fear, and for expectation of the things which are coming on the world: for the powers of the heavens will be shaken.
27 Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
Then they will see the Son of Man coming in a cloud with power and great glory.
28 Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
But when these things begin to happen, look up, and lift up your heads, because your redemption is near.”
29 Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
He told them a parable. “See the fig tree, and all the trees.
30 Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
When they are already budding, you see it and know by your own selves that the summer is already near.
31 Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Even so you also, when you see these things happening, know that God’s Kingdom is near.
32 Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
Most certainly I tell you, this generation will not pass away until all things are accomplished.
33 Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
Heaven and earth will pass away, but my words will by no means pass away.
34 “Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
“So be careful, or your hearts will be loaded down with carousing, drunkenness, and cares of this life, and that day will come on you suddenly.
35 Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
For it will come like a snare on all those who dwell on the surface of all the earth.
36 Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
Therefore be watchful all the time, praying that you may be counted worthy to escape all these things that will happen, and to stand before the Son of Man.”
37 Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
Every day Yeshua [Salvation] was teaching in the temple, and every night he would go out and spend the night on the mountain that is called Olivet.
38 Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
All the people came early in the morning to him in the temple to hear him.

< Luka 21 >