< Luka 21 >

1 Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
And he looked up, and saw the rich men casting their gifts into the treasury.
2 akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
And he saw also a certain poor widow casting in thither two mites.
3 Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
And he said, Truthfully I say unto you, that this poor widow has cast in more than they all:
4 Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
For all these have of their abundance cast in unto the offerings of God: but she of her destitution has cast in all the living that she had.
5 Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
And as some spoke of the temple, how it was adorned with goodly stones and gifts, he said,
6 “Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
As for these things which all of you behold, the days will come, in the which there shall not be left one stone upon another, that shall not be thrown down.
7 Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
And they asked him, saying, Master, but when shall these things be? and what sign will there be when these things shall come to pass?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
And he said, Take heed that all of you be not deceived: for many shall come in my name, saying, I am Christ; and the time draws near: go all of you not therefore after them.
9 Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
But when all of you shall hear of wars and commotions, be not terrified: for these things must first come to pass; but the end is not by and by.
10 Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
Then said he unto them, Nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom:
11 Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
And great earthquakes shall be in divers places, and famines, and pestilences; and fearful sights and great signs shall there be from heaven.
12 Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
But before all these, they shall lay their hands on you, and persecute you, delivering you up to the synagogues, and into prisons, being brought before kings and rulers for my name's sake.
13 Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
And it shall turn to you for a testimony.
14 Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
Settle it therefore in your hearts, not to meditate before what all of you shall answer:
15 kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
For I will give you a mouth and wisdom, which all your adversaries shall not be able to gainsay nor resist.
16 Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
And all of you shall be betrayed both by parents, and brethren, and kinsfolks, and friends; and some of you shall they cause to be put to death.
17 Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
And all of you shall be hated of all men for my name's sake.
18 Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
But there shall not an hair of your head perish.
19 Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
In your patience possess all of you your souls.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
And when all of you shall see Jerusalem compassed with armies, then know that the desolation thereof is nigh.
21 Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
Then let them which are in Judaea flee to the mountains; and let them which are in the midst of it depart out; and let not them that are in the countries enter therein.
22 Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
For these be the days of vengeance, that all things which are written may be fulfilled.
23 Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
But woe unto them that are with child, and to them that give suck, in those days! for there shall be great distress in the land, and wrath upon this people.
24 Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
And they shall fall by the edge of the sword, and shall be led away captive into all nations: and Jerusalem shall be trodden down of the Gentiles, until the times of the Gentiles be fulfilled.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
And there shall be signs in the sun, and in the moon, and in the stars; and upon the earth distress of nations, with perplexity; the sea and the waves roaring;
26 Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Men's hearts failing them for fear, and for looking after those things which are coming on the earth: for the powers of heaven shall be shaken.
27 Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
And then shall they see the Son of man coming in a cloud with power and great glory.
28 Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
And when these things begin to come to pass, then look up, and lift up your heads; for your redemption draws nigh.
29 Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
And he spoke to them a parable; Behold the fig tree, and all the trees;
30 Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
When they now shoot forth, all of you see and know of your own selves that summer is now nigh at hand.
31 Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So likewise all of you, when all of you see these things come to pass, know all of you that the kingdom of God is nigh at hand.
32 Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
Verily I say unto you, This generation shall not pass away, till all be fulfilled.
33 Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
Heaven and earth shall pass away: but my words (logos) shall not pass away.
34 “Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
And take heed to yourselves, lest at any time your hearts be overcharged with worldly excess, and drunkenness, and cares of this life, and so that day come upon you unexpectedly.
35 Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
For as a snare shall it come on all them that dwell on the face of the whole earth.
36 Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
Watch all of you therefore, and pray always, that all of you may be accounted worthy to escape all these things that shall come to pass, and to stand before the Son of man.
37 Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
And in the day time he was teaching in the temple; and at night he went out, and abode in the mount that is called the mount of Olives.
38 Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
And all the people came early in the morning to him in the temple, in order to hear him.

< Luka 21 >