< Luka 19 >

1 Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
Jesus entered Jericho and made his way through the town.
2 Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
There was a man there, known by the name of Zacchaeus, who was a senior tax collector and a rich man.
3 Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
He tried to see what Jesus was like; but, being short, he was unable to do so because of the crowd.
4 Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
So he ran on ahead and climbed into a mulberry tree to see Jesus, for he knew that he must pass that way.
5 Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
When Jesus came to the place, he looked up and said to him, ‘Zacchaeus, be quick and come down, for I must stop at your house today.’
6 Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
So Zacchaeus got down quickly, and joyfully welcomed him.
7 Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
On seeing this, everyone began to complain, ‘He has gone to stay with a man who is an outcast.’
8 Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
But Zacchaeus stood forward and said to the Master, ‘Listen, Master! I will give half my property to the poor, and, if I have defrauded anyone of anything, I will give him back four times as much.’
9 Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
‘Salvation has come to this house today,’ answered Jesus, ‘for even this man is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
The Son of Man has come to search for those who are lost and to save them.’
11 Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
As the people were listening to this, Jesus went on to tell them a parable. He did so because he was near Jerusalem, and because they thought that the kingdom of God was going to be proclaimed at once.
12 Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
He said, ‘A nobleman once went to a distant country to receive his appointment to a kingdom and then return.
13 Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
He called ten of his servants and gave them ten pounds of silver each, and told them to trade with them during his absence.
14 Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
But his subjects hated him and sent envoys after him to say “We will not have this man as our king.”
15 “Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
On his return, after having been appointed king, he directed that the servants to whom he had given his money should be summoned, so that he might learn what amount of trade they had done.
16 Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
The first came up, and said “Sir, your ten pounds have made a hundred.”
17 Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
“Well done, good servant!” exclaimed the master. “As you have proved trustworthy in a very small matter, I appoint you governor over ten towns.”
18 Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
When the second came, he said “Your ten pounds, Sir, have produced fifty.”
19 Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
So the master said to him “And you I appoint over five towns.”
20 “Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
Another servant also came and said “Sir, here are your ten pounds; I have kept them put away in a handkerchief.
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
For I was afraid of you, because you are a stern man. You take what you have not planted, and reap what you have not sown.”
22 Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
The master answered “Out of your own mouth I judge you, you worthless servant. You knew that I am a stern man, that I take what I have not planted, and reap what I have not sown?
23 Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
Then why didn’t you put my money into a bank? And I, on my return, could have claimed it with interest.
24 Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
Take away from him the ten pounds,” he said to those standing by, “and give them to the one who has the hundred.”
25 Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
“But, Sir,” they said, “he has a hundred pounds already!”
26 Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
“I tell you,” he answered, “that, to him who has, more will be given, but, from him who has nothing, even what he has will be taken away.
27 Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
But as for my enemies, these men who would not have me as their king, bring them here and put them to death in my presence.”’
28 Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
After saying this, Jesus went on in front, going up to Jerusalem.
29 Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
It was when Jesus had almost reached Bethphage and Bethany, near the Mount of Olives, that he sent on two of the disciples.
30 akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
‘Go to the village facing us,’ he said, ‘and, when you get there, you will find a foal tethered, which no one has yet ridden; untie it and lead it here.
31 Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
And, if anybody asks you “Why are you untying it?”, you are to say this – “The Master wants it.”’
32 Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
So the two who were sent went and found it as Jesus had told them.
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
While they were untying the foal, the owners asked them – ‘Why are you untying the foal?’
34 Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
And the two disciples answered – ‘The Master wants it.’
35 Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
Then they led it back to Jesus, and threw their cloaks on the foal and put Jesus on it.
36 Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
As he went along, the people kept spreading their cloaks in the road.
37 Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
When he had almost reached the place where the road led down the Mount of Olives, everyone of the many disciples began in their joy to praise God loudly for all the miracles that they had seen:
38 wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
‘Blessed is He who comes – our king – in the name of the Lord! Peace in heaven, and glory on high.’
39 Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
Some of the Pharisees in the crowd said to him, ‘Teacher, restrain your disciples.’
40 Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
But Jesus answered, ‘I tell you that if they are silent, the stones will call out.’
41 Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
When he drew near, on seeing the city, he wept over it, and said,
42 akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
‘If only you had known, while yet there was time – even you – the things that make for peace! But now they have been hidden from your sight.
43 Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
For a time is coming when your enemies will surround you with earthworks, and encircle you, and hem you in on all sides;
44 Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
they will trample you down and your children within you, and they will not leave in you one stone on another, because you did not know the time of your visitation.’
45 Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
Jesus went into the Temple Courts and began to drive out those who were selling,
46 akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
saying as he did so, ‘Scripture says – “My house will be a house of prayer”; but you have made it a den of robbers.’
47 Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
Jesus continued to teach each day in the Temple Courts; but the chief priests and teachers of the Law were eager to take his life, and so also were the leaders of the people.
48 lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.
Yet they could not see what to do, for the people all hung on his words.

< Luka 19 >