< Luka 18 >

1 Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
Or, pour leur montrer qu'il fallait toujours prier et ne pas perdre courage, il leur adressait une parabole
2 Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
en ces termes: « Il y avait dans une ville un certain juge qui ne craignait point Dieu et n'avait d'égards pour personne;
3 Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
or dans cette ville-là était une veuve, et elle venait lui dire: « Fais-moi justice de mon adversaire. »
4 Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
Et pendant longtemps il ne le voulait pas; mais ensuite il se dit en lui-même: Quoique je ne craigne point Dieu et que je n'aie non plus d'égards pour personne,
5 lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
cependant comme cette veuve me cause du tracas, je lui ferai justice, de peur qu'elle ne finisse par venir me donner des coups. »
6 Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
Or le seigneur dit: « Écoutez ce que dit le juge inique;
7 Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
mais Dieu ne fera-t-Il pas justice à Ses élus qui crient à Lui jour et nuit, et tarde-t-Il à leur égard?
8 Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
Je vous déclare qu'il leur fera justice au plus tôt. Toutefois le fils de l'homme, quand il viendra, trouvera-t-il la foi sur la terre? »
9 Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
Or il dit aussi à quelques personnes qui possédaient pour elles-mêmes l'assurance d'être justes et qui méprisaient les autres, la parabole suivante:
10 “Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
« Deux hommes montèrent au temple pour prier, l'un était pharisien, et l'autre publicain.
11 Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
Le pharisien, se tenant debout, faisait en lui-même cette prière: « O Dieu! Je Te rends grâce de ce que je ne suis pas comme les autres hommes qui sont spoliateurs, injustes, adultères, ou même comme ce publicain:
12 Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
je jeûne deux fois la semaine, je donne la dîme de tout ce que j'acquiers. »
13 Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
Mais le publicain se tenant à distance ne se permettait pas même de lever les yeux vers le ciel, mais il se frappait la poitrine en disant: « O Dieu, aie compassion de moi qui suis pécheur! »
14 Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
Je vous le déclare, celui-ci redescendit justifié dans sa maison à l'inverse de l'autre, car quiconque s'élève lui-même sera abaissé, tandis que celui qui s'abaisse lui-même sera élevé. »
15 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
Or on lui apportait aussi les petits enfants, afin qu'il les touchât; ce que les disciples ayant vu ils les réprimandaient.
16 Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
Mais Jésus les appela à lui, en disant: « Laissez les petits enfants venir à moi, et ne les en empêchez pas, car c'est à ceux qui leur ressemblent qu'appartient le royaume de Dieu.
17 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
En vérité je vous le déclare, celui qui n'aura pas reçu le royaume de Dieu comme un petit enfant n'y entrera certainement point. »
18 Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
Et un chef l'interrogea en disant: « Bon Maître, par quelle conduite hériterai-je la vie éternelle? » (aiōnios g166)
19 Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
Mais Jésus lui dit: « Pourquoi m'appelles-tu bon? Nul n'est bon, si ce n'est un seul, Dieu.
20 Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
Tu connais les commandements: « Ne commets point d'adultère; ne tue point; ne dérobe point; ne fais point de faux témoignage; honore ton père et ta mère. »
21 Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
L'autre dit: « J'ai observé toutes ces choses dès ma jeunesse. »
22 Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
Ce que Jésus ayant ouï, il lui dit: « Il te manque encore une chose: vends tout ce que tu possèdes, et distribue-le aux pauvres, et tu auras un trésor dans les cieux; puis viens, suis-moi. »
23 Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
Mais l'autre en entendant cela devint tout triste, car il était très riche.
24 Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
Or Jésus l'ayant regardé dit: « Avec quelle difficulté ceux qui possèdent les richesses entrent-ils dans le royaume de Dieu!
25 Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
Il est en effet plus facile qu'un chameau entre par un trou d'aiguille, qu'un riche n'entre dans le royaume de Dieu. »
26 Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
Mais les auditeurs dirent: « Et qui peut être sauvé? »
27 Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
Or il dit: « Ce qui est impossible quant aux hommes est possible quant à Dieu. »
28 Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
Or Pierre lui dit: « Voici, pour nous, après avoir abandonné nos propres biens, nous t'avons suivi. »
29 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
Et il leur dit: « En vérité je vous déclare qu'il n'est personne qui, ayant abandonné maison, ou femme, ou frères, ou parents, ou enfants, à cause du royaume de Dieu,
30 atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
ne reçoive infiniment davantage dans ce temps-ci, et dans le siècle à venir la vie éternelle. » (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
Et ayant pris les douze à part, il leur dit: « Voici, nous montons à Jérusalem, et tout ce qui a été écrit par les prophètes relativement au fils de l'homme s'accomplira;
32 Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
car il sera livré aux Gentils, et il sera bafoué et injurié, et on crachera sur lui,
33 Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
et après l'avoir fouetté ils le mettront à mort, et le troisième jour il ressuscitera. »
34 Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
Et pour eux ils ne comprenaient rien à cela, et cette parole leur était cachée, et ils ne saisissaient pas ce qui avait été dit.
35 Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
Or il advint, au moment où il approchait de Jéricho, qu'un aveugle se trouvait assis près du chemin pour mendier.
36 Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
Mais ayant entendu la foule qui passait devant lui, il s'informait de ce que c'était.
37 Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
On lui dit: « C'est Jésus le Nazaréen qui passe. »
38 Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Et il s'écria: « Jésus, fils de David, aie pitié de moi. »
39 Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
Et ceux qui marchaient les premiers le réprimandaient pour le faire taire; mais lui criait de plus belle: « Fils de David, aie pitié de moi. »
40 Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
Et Jésus s'étant arrêté ordonna qu'on le lui amenât; et quand il se fut approché, il lui demanda: « Que veux-tu que je fasse pour toi? »
41 “Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
Et l'autre dit: « Seigneur, que je recouvre la vue.
42 Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
Et Jésus lui dit: « Recouvre la vue; ta foi t'a guéri. »
43 Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.
Et immédiatement il recouvra la vue, et il le suivait en glorifiant Dieu. Et tout le peuple voyant cela rendit louange à Dieu.

< Luka 18 >