< Luka 12 >

1 Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
Meanwhile the people had gathered in thousands, so that they trod on one another, when Jesus, addressing himself to his disciples, began by saying to them, ‘Be on your guard against the leaven – that is, the hypocrisy – of the Pharisees.
2 Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
There is nothing, however covered up, which will not be uncovered, nor anything kept secret which will not become known.
3 Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
So all that you have said in the dark will be heard in the light, and what you have spoken in the ear, within closed doors, will be proclaimed on the housetops.
4 “Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
To you who are my friends I say, Do not be afraid of those who kill the body, but after that can do no more.
5 Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
I will show you of whom you should be afraid. Be afraid of him who, after killing you, has the power to fling you into Gehenna. Yes, I say, be afraid of him. (Geenna g1067)
6 Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
Are not five sparrows sold for two copper coins? Yet not one of them has escaped God’s notice.
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
No, even the hairs of your head are all numbered. Do not be afraid; you are of more value than many sparrows.
8 “Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
Everyone, I tell you, who publicly acknowledges me, the Son of Man, also, will acknowledge before God’s angels;
9 Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
but the person who publicly disowns me will be altogether disowned before God’s angels.
10 “Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Everyone who will say anything against the Son of Man will be forgiven, but for the person who slanders the Holy Spirit there will be no forgiveness.
11 “Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
Whenever they take you before the synagogue Courts or the magistrates or other authorities, do not be anxious as to how you will defend yourselves, or what your defence will be, or what you will say;
12 Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
for the Holy Spirit will show you at the moment what you ought to say.’
13 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
‘Teacher,’ a man in the crowd said to Jesus, ‘tell my brother to share the property with me.’
14 Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
But Jesus said to him, ‘Man, who made me a judge or an arbiter between you?’
15 Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
And then he added, ‘Take care to keep yourselves free from every form of covetousness; for even in the height of their prosperity a person’s true life does not depend on what they have.’
16 Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
Then Jesus told them this parable – ‘There was once a rich man whose land was very fertile;
17 Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
and he began to ask himself “What will I do, for I have nowhere to store my crops?
18 Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
This is what I will do,” he said; “I will pull down my barns and build larger ones, and store all my grain and my goods in them;
19 Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
and I will say to myself, Now you have plenty of good things put by for many years; take your ease, eat, drink, and enjoy yourself.”
20 Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
But God said to the man “Fool! This very night your life is being demanded; and as for all you have prepared – who will have it?”
21 Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
So it is with those who lay by wealth for themselves and are not rich to the glory of God.’
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
And Jesus said to his disciples, ‘That is why I say to you, Do not be anxious about the life here – what you can get to eat; or about your body – what you can get to wear.
23 Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
For life is more than food, and the body than its clothes.
24 Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
Think of the ravens – they neither sow nor reap; they have neither storehouse nor barn; and yet God feeds them! And how much more precious are you than birds!
25 Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
But which of you, by being anxious, can prolong your life a moment?
26 Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
And, if you cannot do even the smallest thing, why be anxious about other things?
27 Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
Think of the lilies, and how they grow. They neither toil nor spin; yet, I tell you, even Solomon in all his splendour was not robed like one of these.
28 Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
If, even in the field, God so clothes the grass which is living today and tomorrow will be thrown into the oven, how much more will he clothe you, you of little faith!
29 “Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
And you – do not be always seeking what you can get to eat or what you can get to drink; and do not waver.
30 Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
These are the things for which all the nations of the world are seeking, and your Father knows that you need them.
31 Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
No, seek his kingdom, and these things will be added for you.
32 “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
So do not be afraid, my little flock, for your Father has been pleased to give you the kingdom.
33 Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
‘Sell what belongs to you, and give in charity. Make yourselves purses that will not wear out – an inexhaustible treasure in heaven, where no thief comes near, or moth works ruin.
34 Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
For where your treasure is, there also will your heart be.
35 “Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
Make yourselves ready, with your lamps alight;
36 muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
and be like servants who are waiting for their Master’s return from his wedding, so that, when he comes and knocks, they may open the door for him at once.
37 Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
Happy are those servants whom, on his return, the Master will find watching. I tell you that he will make himself ready, and have them take their places at the table, and will come and serve them.
38 Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
Whether it is late at night, or in the early morning that he comes, if he finds all as it should be, then happy are they.
39 Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
This you do know, that, had the owner of the house known at what time the thief was coming, he would have been on the watch, and would not have let his house be broken into.
40 Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
You must also prepare, for when you are least expecting him the Son of Man will come.’
41 Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
‘Master,’ said Peter, ‘are you telling this parable with reference to us or to everyone?’
42 Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
‘Who, then,’ replied the Master, ‘is that trustworthy steward, the careful man, who will be placed by his master over his establishment, to give them their rations at the proper time?
43 Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Happy will that servant be whom his master, when he comes home, will find doing this.
44 Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
His master, I tell you, will put him in charge of the whole of his property.
45 Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
But should that servant say to himself “My master is a long time coming,” and begin to beat the menservants and the maidservants, and to eat and drink and get drunk,
46 bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
that servant’s master will come on a day when he does not expect him, and at an hour of which he is unaware, and will flog him severely and assign him his place among the untrustworthy.
47 Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
The servant who knows his master’s wishes and yet does not prepare and act accordingly will receive many lashes;
48 Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
while one who does not know his master’s wishes, but acts so as to deserve a flogging, will receive but few. From everyone to whom much has been given much will be expected, and from the man to whom much has been entrusted the more will be demanded.
49 “Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
I came to cast fire on the earth; and what more can I wish, if it is already kindled?
50 Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
There is a baptism that I must undergo, and how great is my distress until it is over!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
Do you think that I am here to bring peace on earth? No, I tell you, but to cause division.
52 Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
For from this time, if there are five people in a house, they will be divided, three against two, and two against three.
53 Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
Father will be opposed to son and son to father, mother to daughter and daughter to mother, mother-in-law to her daughter-in-law and daughter-in-law to her mother-in-law.’
54 Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
And to the people Jesus said, ‘When you see a cloud rising in the west, you say at once “There is a storm coming,” and come it does.
55 Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
And when you see that the wind is in the south, you say “It will be burning hot,” and so it proves.
56 Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
Hypocrites! You know how to judge of the earth and the sky; how is it, then, that you cannot judge of this time?
57 “Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
Why don’t you yourselves decide what is right?
58 Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
When, for instance, you are going with your opponent before a magistrate, on your way to the court do your best to be quit of him; otherwise he might drag you before the judge, then the judge will hand you over to the bailiff of the court, and the bailiff throw you into prison.
59 Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”
You will not, I tell you, come out until you have paid the very last cent.’

< Luka 12 >