< Luka 1 >

1 Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
Quoniam quidem multi conati sunt ordinare narrationem, quae in nobis completae sunt, rerum:
2 Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
sicut tradiderunt nobis, qui ab initio ipsi viderunt, et ministri fuerunt sermonis:
3 Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
visum est et mihi, assecuto omnia a principio diligenter, ex ordine tibi scribere, optime Theophile,
4 ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
ut cognoscas eorum verborum, de quibus eruditus es, veritatem.
5 Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
Fuit in diebus Herodis, regis Iudaeae, sacerdos quidam nomine Zacharias de vice Abia, et uxor illius de filiabus Aaron, et nomen eius Elisabeth.
6 Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
Erant autem iusti ambo ante Deum, incedentes in omnibus mandatis, et iustificationibus Domini sine querela,
7 Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
et non erat illis filius eo quod esset Elisabeth sterilis, et ambo processissent in diebus suis.
8 Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
Factum est autem, cum sacerdotio fungeretur Zacharias in ordine vicis suae ante Deum,
9 Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
secundum consuetudinem sacerdotii, sorte exiit ut incensum poneret, ingressus in templum Domini:
10 Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
et omnis multitudo populi erat orans foris hora incensi.
11 Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
Apparuit autem illi Angelus Domini, stans a dextris altaris incensi.
12 Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
Et Zacharias turbatus est videns, et timor irruit super eum.
13 Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
Ait autem ad illum Angelus: Ne timeas Zacharia, quoniam exaudita est deprecatio tua: uxor tua Elisabeth pariet tibi filium, et vocabis nomen eius Ioannem:
14 Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
et erit gaudium tibi, et exultatio, et multi in nativitate eius gaudebunt:
15 Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
erit enim magnus coram Domino: vinum, et siceram non bibet, et Spiritu sancto replebitur adhuc ex utero matris suae:
16 Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
et multos filiorum Israel convertet ad Dominum Deum ipsorum:
17 Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
et ipse praecedet ante illum in spiritu, et virtute Eliae: ut convertat corda patrum in filios, et incredulos ad prudentiam iustorum, parare Domino plebem perfectam.
18 Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
Et dixit Zacharias ad Angelum: Unde hoc sciam? ego enim sum senex, et uxor mea processit in diebus suis.
19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
Et respondens Angelus dixit ei: Ego sum Gabriel, qui asto ante Deum: et missus sum loqui ad te, et haec tibi evangelizare.
20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
Et ecce eris tacens, et non poteris loqui usque in diem, quo haec fiant, pro eo quod non credidisti verbis meis, quae implebuntur in tempore suo.
21 Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
Et erat plebs expectans Zachariam: et mirabantur quod tardaret ipse in templo.
22 Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
Egressus autem non poterat loqui ad illos, et cognoverunt quod visionem vidisset in templo. Et ipse erat innuens illis, et permansit mutus.
23 Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
Et factum est, ut impleti sunt dies officii eius abiit in domum suam:
24 Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
post hos autem dies concepit Elisabeth uxor eius, et occultabat se mensibus quinque, dicens:
25 “Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
Quia sic fecit mihi Dominus in diebus, quibus respexit auferre opprobrium meum inter homines.
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
In mense autem sexto, missus est Angelus Gabriel a Deo in civitatem Galilaeae, cui nomen Nazareth,
27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
ad Virginem desponsatam viro, cui nomen erat Ioseph, de domo David, et nomen virginis Maria.
28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
Et ingressus Angelus ad eam dixit: Ave gratia plena: Dominus tecum: Benedicta tu in mulieribus.
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
Quae cum audisset, turbata est in sermone eius, et cogitabat qualis esset ista salutatio.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
Et ait Angelus ei: Ne timeas Maria, invenisti enim gratiam apud Deum.
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
ecce concipies in utero, et paries filium, et vocabis nomen eius IESUM.
32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
hic erit magnus, et Filius Altissimi vocabitur, et dabit illi Dominus Deus sedem David patris eius:
33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
et regnabit in domo Iacob in aeternum, et regni eius non erit finis. (aiōn g165)
34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
Dixit autem Maria ad Angelum: Quomodo fiet istud, quoniam virum non cognosco?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
Et respondens Angelus dixit ei: Spiritus sanctus superveniet in te, et virtus Altissimi obumbrabit tibi. Ideoque et quod nascetur ex te Sanctum, vocabitur Filius Dei.
36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
Et ecce Elisabeth cognata tua, et ipsa concepit filium in senectute sua: et hic mensis sextus est illi, quae vocatur sterilis:
37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
quia non erit impossibile apud Deum omne verbum.
38 Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
Dixit autem Maria: Ecce ancilla Domini, fiat mihi secundum verbum tuum. Et discessit ab illa Angelus.
39 Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
Exurgens autem Maria in diebus illis abiit in montana cum festinatione, in civitatem Iuda:
40 Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
Et intravit in domum Zachariae, et salutavit Elisabeth.
41 Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
Et factum est, ut audivit salutationem Mariae Elisabeth, exultavit infans in utero eius: et repleta est Spiritu sancto Elisabeth:
42 akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
et exclamavit voce magna, et dixit: Benedicta tu inter mulieres, et benedictus fructus ventris tui.
43 Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
Et unde hoc mihi ut veniat mater Domini mei ad me?
44 Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
Ecce enim ut facta est vox salutationis tuae in auribus meis, exultavit in gaudio infans in utero meo.
45 Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
et beata, quae credidisti, quoniam perficientur ea, quae dicta sunt tibi a Domino.
46 Naye Maria akasema,
Et ait Maria: Magnificat anima mea Dominum:
47 “Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
et exultavit spiritus meus in Deo salutari meo.
48 Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
Quia respexit humilitatem ancillae suae: ecce enim ex hoc beatam me dicent omnes generationes.
49 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
Quia fecit mihi magna qui potens est: et sanctum nomen eius.
50 Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
Et misericordia eius a progenie in progenies timentibus eum.
51 Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
Fecit potentiam in brachio suo: dispersit superbos mente cordis sui.
52 amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
Deposuit potentes de sede, et exaltavit humiles.
53 Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
Esurientes implevit bonis: et divites dimisit inanes.
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
Suscepit Israel puerum suum, recordatus misericordiae suae.
55 Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
Sicut locutus est ad patres nostros, Abraham, et semini eius in saecula. (aiōn g165)
56 Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
Mansit autem Maria cum illa quasi mensibus tribus: et reversa est in domum suam.
57 Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
Elisabeth autem impletum est tempus pariendi, et peperit filium.
58 Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
Et audierunt vicini, et cognati eius quia magnificavit Dominus misericordiam suam cum illa, et congratulabantur ei.
59 Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
Et factum est in die octavo, venerunt circumcidere puerum, et vocabant eum nomine patris sui Zachariam.
60 Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
Et respondens mater eius, dixit: Nequaquam, sed vocabitur Ioannes.
61 Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
Et dixerunt ad illam: Quia nemo est in cognatione tua, qui vocetur hoc nomine.
62 Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
Innuebant autem patri eius, quem vellet vocari eum.
63 Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
Et postulans pugillarem scripsit, dicens: Ioannes est nomen eius. Et mirati sunt universi.
64 Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
Apertum est autem illico os eius, et lingua eius, et loquebatur benedicens Deum.
65 Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
Et factus est timor super omnes vicinos eorum: et super omnia montana Iudaeae divulgabantur omnia verba haec:
66 Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
et posuerunt omnes, qui audierant in corde suo, dicentes: Quis, putas, puer iste erit? Etenim manus Domini erat cum illo.
67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
Et Zacharias pater eius repletus est Spiritu sancto: et prophetavit, dicens:
68 “Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
Benedictus Dominus Deus Israel, quia visitavit, et fecit redemptionem plebis suae:
69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
Et erexit cornu salutis nobis: in domo David pueri sui.
70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
Sicut locutum est per os sanctorum, qui a saeculo sunt, prophetarum eius: (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
Salutem ex inimicis nostris, et de manu omnium, qui oderunt nos:
72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
Ad faciendam misericordiam cum patribus nostris: et memorari testamenti sui sancti.
73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
Iusiurandum, quod iuravit ad Abraham patrem nostrum, daturum se nobis:
74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
Ut sine timore, de manu inimicorum nostrorum liberati, serviamus illi.
75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
In sanctitate, et iustitia coram ipso, omnibus diebus nostris.
76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
Et tu puer, propheta Altissimi vocaberis: praeibis enim ante faciem Domini parare vias eius:
77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
Ad dandam scientiam salutis plebi eius: in remissionem peccatorum eorum:
78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
Per viscera misericordiae Dei nostri: in quibus visitavit nos, oriens ex alto:
79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
Illuminare his, qui in tenebris, et in umbra mortis sedent: ad dirigendos pedes nostros in viam pacis.
80 Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
Puer autem crescebat, et confortabatur spiritu: et erat in desertis usque in diem ostensionis suae ad Israel.

< Luka 1 >