< Luka 1 >

1 Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
我らの中に成りし事の物語につき、始よりの目撃者にして、
2 Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
御言の役者となりたる人々の、我らに傳へし其のままを書き列ねんと、手を著けし者あまたある故に、
3 Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
我も凡ての事を最初より詳細に推し尋ねたれば、
4 ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
テオピロ閣下よ、汝の教へられたる事の慥なるを悟らせん爲に、これが序を正して書き贈るは善き事と思はるるなり。
5 Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
ユダヤの王ヘロデの時、アビヤの組の祭司に、ザカリヤという人あり。その妻はアロンの裔にて、名をエリサベツといふ。
6 Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
二人ながら神の前に正しくして、主の誡命と定規とを、みな缺なく行へり。
7 Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
エリサベツ石女なれば、彼らに子なし、また二人とも年 邁みぬ。
8 Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
さてザカリヤその組の順番に當りて、神の前に祭司の務を行ふとき、
9 Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
祭司の慣例にしたがひて、籤をひき主の聖所に入りて、香を燒くこととなりぬ。
10 Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
香を燒くとき、民の群みな外にありて祈りゐたり。
11 Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
時に主の使あらはれて、香壇の右に立ちたれば、
12 Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
ザカリヤ之を見て、心さわぎ懼を生ず。
13 Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
御使いふ『ザカリヤよ、懼るな、汝の願は聽かれたり。汝の妻エリサベツ男子を生まん、汝その名をヨハネと名づくべし。
14 Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
なんぢに喜悦と歡樂とあらん、又おほくの人もその生るるを喜ぶべし。
15 Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
この子、主の前に大ならん、また葡萄酒と濃き酒とを飮まず、母の胎を出づるや聖 靈にて滿されん。
16 Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
また多くのイスラエルの子らを、主なる彼らの神に歸らしめ、
17 Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
且エリヤの靈と能力とをもて、主の前に往かん。これ父の心を子に、戻れる者を義人の聰明に歸らせて、整へたる民を主のために備へんとてなり』
18 Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
ザカリヤ御使にいふ『何に據りてか此の事あるを知らん。我は老人にて、妻もまた年 邁みたり』
19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
御使こたへて言ふ『われは神の御前に立つガブリエルなり、汝に語りてこの嘉き音信を告げん爲に遣さる。
20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
視よ、時いたらば必ず成就すべき我が言を信ぜぬに因り、なんぢ物 言へずなりて、此らの事の成る日までは語ること能はじ』
21 Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
民はザカリヤを俟ちゐて、其の聖所の内に久しく留るを怪しむ。
22 Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
遂に出で來りたれど語ること能はねば、彼らその聖所の内にて異象を見たることを悟る。ザカリヤは、ただ首にて示すのみ、なほ唖なりき。
23 Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
かくて務の日 滿ちたれば、家に歸りぬ。
24 Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
此の後その妻エリサベツ孕りて、五月ほど隱れをりて言ふ、
25 “Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
『主わが恥を人の中に雪がせんとて、我を顧み給ふときは、斯く爲し給ふなり』
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
その六月めに、御使ガブリエル、ナザレといふガリラヤの町にをる處女のもとに、神より遣さる。
27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
この處女はダビデの家のヨセフといふ人と許嫁せし者にて、其の名をマリヤと云ふ。
28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
御使、處女の許にきたりて言ふ『めでたし、惠まるる者よ、主なんぢと偕に在せり』
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
マリヤこの言によりて心いたく騷ぎ、斯かる挨拶は如何なる事ぞと思ひ廻らしたるに、
30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
御使いふ『マリヤよ、懼るな、汝は神の御前に惠を得たり。
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
視よ、なんぢ孕りて男子を生まん、其の名をイエスと名づくべし。
32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
彼は大ならん、至高者の子と稱へられん。また主たる神、これに其の父ダビデの座位をあたへ給へば、
33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
ヤコブの家を永遠に治めん。その國は終ることなかるべし』 (aiōn g165)
34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
マリヤ御使に言ふ『われ未だ人を知らぬに、如何にして此の事のあるべき』
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
御使こたへて言ふ『聖 靈なんぢに臨み、至高者の能力なんぢを被はん。此の故に汝が生むところの聖なる者は、神の子と稱へらるべし。
36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
視よ、なんぢの親族エリサベツも、年 老いたれど、男子を孕めり。石女といはれたる者なるに、今は孕りてはや六月になりぬ。
37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
それ神の言には能はぬ所なし』
38 Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
マリヤ言ふ『視よ、われは主の婢女なり。汝の言のごとく、我に成れかし』つひに御使はなれ去りぬ。
39 Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
その頃マリヤ立ちて山里に急ぎ往き、ユダの町にいたり、
40 Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
ザカリヤの家に入りてエリサベツに挨拶せしに、
41 Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
エリサベツその挨拶を聞くや、兒は胎内にて躍れり。エリサベツ聖 靈にて滿され、
42 akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
聲 高らかに呼はりて言ふ『をんなの中にて汝は祝福せられ、その胎の實もまた祝福せられたり。
43 Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
わが主の母われに來る、われ何によりてか之を得し。
44 Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
視よ、なんぢの挨拶の聲、わが耳に入るや、我が兒、胎内にて喜びをどれり。
45 Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
信ぜし者は幸福なるかな、主の語り給ふことは必ず成就すべければなり』
46 Naye Maria akasema,
マリヤ言ふ、『わがこころ主をあがめ、
47 “Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
わが靈はわが救主なる神を喜びまつる。
48 Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
その婢女の卑しきをも顧み給へばなり。視よ、今よりのち萬 世の人われを幸福とせん。
49 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
全能者われに大なる事を爲したまへばなり。その御名は聖なり、
50 Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
そのあはれみは代々かしこみ恐るる者に臨むなり。
51 Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
神は御腕にて權力をあらはし、心の念に高ぶる者を散し、
52 amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
權勢ある者を座位より下し、いやしき者を高うし、
53 Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
飢ゑたる者を善き物に飽かせ、富める者を空しく去らせ給ふ。
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
また我らの先祖に告げ給ひし如く、
55 Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
アブラハムとその裔とに對するあはれみを永遠に忘れじとて、僕イスラエルを助けたまへり』 (aiōn g165)
56 Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
かくてマリヤは、三月ばかりエルザベツと偕に居りて、己が家に歸れり。
57 Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
さてエリサベツ産む期みちて男子を生みたれば、
58 Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
その最寄のもの親族の者ども、主の大なる憐憫をエリサベツに垂れ給ひしことを聞きて、彼とともに喜ぶ。
59 Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
八日めになりて、其の子に割禮を行はんとて人々きたり、父の名に因みてザカリヤと名づけんとせしに、
60 Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
母こたへて言ふ『否、ヨハネと名づくべし』
61 Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
かれら言ふ『なんぢの親族の中には此の名をつけたる者なし』
62 Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
而して父に首にて示し、いかに名づけんと思ふか、問ひたるに、
63 Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
ザカリヤ書板を求めて『その名はヨハネなり』と書きしかば、みな怪しむ。
64 Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
ザカリヤの口たちどころに開け、舌ゆるみ、物いひて神を讃めたり。
65 Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
最寄に住む者みな懼をいだき、又すべて此 等のこと徧くユダヤの山里に言ひ囃されたれば、
66 Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
聞く者みな之を心にとめて言ふ『この子は如何なる者にか成らん』主の手かれと偕に在りしなり。
67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
かくて父ザカリヤ聖 靈にて滿され預言して言ふ、
68 “Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
『讃むべきかな、主イスラエルの神、その民をかへりみて贖罪をなし、
69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
我らのために救の角を、その僕ダビデの家に立て給へり。
70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
これぞ古へより聖 預言者の口をもて言ひ給ひし如く、 (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
我らを仇より、凡て我らを憎む者の手より、取り出したまふ救なる。
72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
我らの先祖に憐憫を垂れ、その聖なる契約を思し、
73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
我らの先祖アブラハムに立て給ひし御誓を忘れずして、
74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
我らを仇の手より救ひ、生涯、主の御前に、
75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
聖と義とをもて懼なく事へしめたまふなり。
76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
幼兒よ、なんぢは至高者の預言者と稱へられん。これ主の御前に先だちゆきて、其の道を備へ、
77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
主の民に罪の赦による救を知らしむればなり。
78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
これ我らの神の深き憐憫によるなり。この憐憫によりて朝のひかり、上より臨み、
79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
暗黒と死の蔭とに坐する者をてらし、我らの足を平和の路にみちびかん』
80 Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
かくて幼兒は漸に成長し、その靈 強くなり、イスラエルに現るる日まで荒野にゐたり。

< Luka 1 >