< Luka 1 >

1 Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
Seeing that many have taken it in hand to draw up an account of those matters which have been fully established among us,
2 Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
just as they reported them to us, who were from beginning eye- witnesses and ministers of the word,
3 Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
it seemed good to me also accurately, from the very beginning, to write them to you in order, most excellent Theophilus,
4 ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
so that you may know the certainty of the story which you have been taught by the word of mouth.
5 Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
In the reign of Herod, King of Judea, there was a certain priest, named Zachariah, belonging to the class of Abijah. He had a wife named Elizabeth,
6 Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
who was a descendant of Aaron. They were both righteous in the sight of the Lord, walking in all the commandments and ordinances of the law, blameless.
7 Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
Now they had no child, for Elizabeth was barren, and both were far advanced in years.
8 Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
Now while Zachariah was acting as priest before God in the due course of his class, it fell to his lot, according to the custom of priesthood,
9 Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
to enter into the sanctuary of the Lord and to burn incense.
10 Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
And the whole multitude of the people were without, praying at the hour of incense.
11 Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
Then there appeared to him an angel of the Lord, standing on the right side of the altar of incense.
12 Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
And as he saw him Zachariah was troubled, and fear fell upon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
But the Angel said to him. "Do not be afraid, Zachariah, because your petition has been heard, and your wife Elizabeth will bear you a son, and you are to call him John.
14 Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
"And he shall be to you a joy and an exultation, and many shall rejoice over his birth.
15 Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
"For he shall be great in the sight of the Lord, "He shall drink neither wine nor strong drink, "He shall be filled with the Holy Spirit from the hour of his birth,
16 Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
"And shall win many of the sons of Israel to the Lord, their God.
17 Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
"He shall go before Him in the wisdom and power of Elijah to turn the hearts of the fathers to their children and the disobedient to the wisdom of the righteous, and so to make ready for the Lord a people prepared for him."
18 Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
"How shall I be sure of this?" said Zachariah to the Angel. "For I am an old man and my wife is advanced in years."
19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
"I am Gabriel," answered the angel, "who stand in the presence of God; and I have been sent to speak to you and to bring and to bring you this good news.
20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
"And now you shall be silent and unable to speak until the day the day when this has taken place; because you did not believe my words - Words which will be fulfilled at their appointed time."
21 Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
Meanwhile the people were waiting for Zachariah and wondering why he stayed so long in the sanctuary.
22 Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
And when he came out he could not speak to them, and then they knew that he had seen a vision in the sanctuary. He kept making signs to them and remained dumb.
23 Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
As soon as his term of priestly service was ended he went home;
24 Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
and after those days Elizabeth, his wife, Conceived, and she hid herself five months, saying.
25 “Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
"This has the Lord done for me. He has now deigned to take the away my reproach among men."
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
Six months later the angel Gabriel was sent by God to a town in Galilee, called Nazareth,
27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
to a maiden betrothed to a man named Joseph, a descendant of David. Her name was Mary.
28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
The angel went in and said to her. "Joy to you, highly favored one! "The Lord is with you."
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
Mary was greatly agitated at his word, and was revolving in her mind what this salutation could mean.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
when the angel said to her. "Fear not Mary, for you have found grace with God.
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
"And behold, you shall conceive in your womb and bear a son; and you shall call his name Jesus.
32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
"He shall be great, and shall be called the Son of the Most High. "And the Lord God will give him the throne of his forefather David,
33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
"and he shall reign over the House of Jacob forever; and of his kingdom there shall be no end." (aiōn g165)
34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
And Mary said to the angel. "How can this be? For I have no husband?"
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
"The Holy Spirit shall come upon you," said the angel, "and the power of the most High shall overshadow you, and therefore the holy offspring which is born, shall be called the son of God.
36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
"And behold your kinswoman, Elizabeth, she also has conceived a son in her old age, and this was the sixth month with her that was called barren.
37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
"For no word of God shall be void of power."
38 Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
Then Mary said. "Behold I am Lord’s slave. Let it be to me as you have said." Then the angel departed from her.
39 Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
Soon after this Mary set out and hastened unto the hill-country to a town in Judah;
40 Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
and there she came into the house of Zachariah, and greeted Elizabeth.
41 Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
And when Elizabeth heard her salutation, the babe leaped in her womb, and Elizabeth herself was filled with the Holy Spirit,
42 akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
and called out with a loud cry. "Blessed are you among women, and blessed is your unborn child!
43 Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
"But why is this honor done me, that the mother of my Lord should come me?
44 Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
"For behold when the sound of your salutation reached my ears, the babe leaped with joy within my womb.
45 Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
"And blessed is she who believed that the Lord’s words spoken to her would be fulfilled."
46 Naye Maria akasema,
And Mary said. "My soul doth magnify the Lord,
47 “Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
"My spirit exults in the God, who is my Saviour,
48 Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
"For he has regarded the humiliation of his slave, And from this hour all ages will count me blessed.
49 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
"For he who is mighty has done great things for me; And holy is his name.
50 Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
"His mercy is unto generations and generations on those who reverence him.
51 Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
"He has showed strength with his arm. "He has scattered proud in the imagination of their hearts;
52 amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
"he has put down princes from their thrones, and has exalted those of low degree.
53 Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
"The hungry he has filled with good things, But the rich he has sent empty away.
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
"He has helped Israel, his servant, that he might remember mercy,
55 Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
"As he spoke to our forefathers, to Abraham and his offspring forever." (aiōn g165)
56 Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
So Mary stayed with Elizabeth about three months and returned home.
57 Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
Now when the time of Elizabeth’s delivery was come, she gave birth to a son;
58 Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
and her neighbors and kinsfolk heard that the Lord had magnified his mercy toward her; and they rejoiced with her,
59 Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
and came on the eighth day to circumcise the child. They were about to call him "Zachariah," after his father,
60 Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
when his mother said, "No, he is to be called John."
61 Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
Said they, "You have no relatives of that name!"
62 Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
Then they asked his father by signs what he wished to call the child.
63 Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
So he asked for a writing tablet and wrote down, "His name is John."
64 Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
Every one was surprised, and at once his mouth was opened and his tongue loosed, and he spoke, blessing God.
65 Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
And there came a great fear upon all in the neighborhood; and throughout the hill country of Judea all these sayings were much talked about.
66 Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
All the story laid it up in their hearts, saying "What, then, will this child be?" For the Lord’s hands was with him.
67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
And his father, Zachariah, was filled with the Holy Spirit and prophesied, saying.
68 “Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
"Blessed be the Lord, the God of Israel, For he has visited and redeemed his people,
69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
"And has raised up a mighty Deliverer for us In the house of his servant David,
70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
"As he spake by the mouth of his holy Prophets Which have been since the world began (aiōn g165)
71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
To deliver us from our enemies, and from the power Of all who hate us.
72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
"He showed mercy to our forefathers, He remembered his holy covenant,
73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
"The oath which he swore to Abraham, our forefather,
74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
"That he we should be delivered out of the Hand of our enemies, And should serve him without fear,
75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
"In holiness and righteousness before him All our days.
76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
"And thou, child, shalt be called the Prophet of the Most High, For thou shalt go before the Lord to prepare the way
77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
"To give to his people a knowledge of salvation Through the remission of their sins,
78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
"Through the heart of mercy of our God, Whereby the Dayspring from on high shall visit us,
79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
"To give light to those who sit in darkness and in the shadow of death, And to guide our feet into the paths of peace."
80 Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
And the child grew, and became strong in the Spirit, and remained in the desert till the day of his showing to Israel.

< Luka 1 >