< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
And the third day a wedding occurred in Cana of Galilee, and the mother of Jesus was there.
2 naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
And Jesus also was invited, and his disciples, to the wedding.
3 Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”
And having lacked wine the mother of Jesus says to him, They have no wine.
4 Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”
And Jesus says to her, What is with me and with thee, woman? My hour is not yet here.
5 Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
His mother says to the helpers, Whatever he may say to you, do.
6 Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
Now there were six stone water pots laying there in accordance with the purification of the Jews, containing two or three measures each.
7 Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
Jesus says to them, Fill the water pots with water. And they filled them until over.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”
And he says to them, Draw out now, and carry to the feast-ruler. And they carried.
9 Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
And when the feast-ruler tasted the water that became wine, and had not known from where it was (but the helpers who drew the water had known), the feast-ruler called the bridegroom,
10 akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”
and says to him, Every man sets out the good wine first, and when they drank much, then the lesser. Thou have kept the good wine until now.
11 Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
This is the beginning of the signs Jesus did in Cana of Galilee, and he manifested his glory. And his disciples believed in him.
12 Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
After this he went down to Capernaum, he and his mother and his brothers and his disciples. And they remained there not many days.
13 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
And the Passover of the Jews was near, and Jesus went up to Jerusalem.
14 Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
And he found sitting in the temple those who sell oxen and sheep and doves, and the moneychangers.
15 Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
And having made a whip from cords, he drove all out from the temple, both the sheep and the oxen. And he poured out the coins of the moneychangers, and turned over their tables.
16 Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!”
And he said to those who sell the doves, Take these things from here. Make not my Father's house a house of merchandise.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: “Upendo wangu kwa nyumba yako waniua.”
And his disciples remembered that it is written, Zeal for thy house will consume me.
18 Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, “Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?”
The Jews therefore answered, and said to him, What sign do thou show us since thou do these things?
19 Yesu akawaambia, “Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.”
Jesus answered and said to them, Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
20 Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?”
The Jews therefore said, This temple was forty-six years being built, and will thou raise it up in three days?
21 Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
But that man spoke about the temple of his body.
22 Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
When therefore he was raised from the dead his disciples remembered that he spoke this, and they believed the scripture and the word that Jesus said.
23 Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
Now when he was in Jerusalem at the Passover during the feast, many believed in his name seeing his signs that he did.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
But Jesus did not trust himself to them, because he knew all men,
25 Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
and because he had no need that any man should testify about man, for he himself knew what was in man.

< Yohana 2 >