< Yohana 13 >

1 Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
Avant la fête de Pâque, Jésus, sachant que son heure était venue de passer de ce monde à son Père, après avoir aimé les siens qui étaient dans le monde, les aima jusqu'à la fin.
2 Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
Pendant le souper, lorsque déjà le diable avait mis dans le cœur de Judas, fils de Simon Iscariote, le dessein de le livrer,
3 Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
Jésus, qui savait que son Père avait remis toutes choses entre ses mains, et qu'il était sorti de Dieu et s'en allait à Dieu,
4 Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
se leva de table, posa son manteau, et, ayant pris un linge, il s'en ceignit.
5 Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
Puis il versa de l'eau dans le bassin et se mit à laver les pieds de ses disciples, et à les essuyer avec le linge dont il était ceint.
6 Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, “Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?”
Il vint donc à Simon-Pierre; et Pierre lui dit: " Quoi, vous Seigneur, vous me lavez les pieds! "
7 Yesu akamjibu, “Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye.”
Jésus lui répondit: " Ce que je fais, tu ne le sais pas maintenant, mais tu le comprendras bientôt. "
8 Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn g165)
Pierre lui dit: " Non, jamais vous ne me laverez les pieds. " Jésus lui répondit: " Si je ne te lave, tu n'auras point de part avec moi. " (aiōn g165)
9 Simoni Petro akamwambia, “Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia.”
Simon-Pierre lui dit: " Seigneur, non seulement les pieds, mais encore les mains et la tête! "
10 Yesu akamwambia, “Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”
Jésus lui dit: " Celui qui a pris un bain n'a besoin que de laver ses pieds; il est pur tout entier. Et vous aussi, vous êtes purs, mais non pas tous. "
11 (Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: “Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”)
Car il savait quel était celui qui allait le livrer; c'est pourquoi il dit: " Vous n'êtes pas tous purs. "
12 Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, “Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
Après qu'il leur eut lavé les pieds, et repris son manteau, il se remit à table et leur dit: " Comprenez-vous ce que je vous ai fait?
13 Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
Vous m'appelez le Maître et le Seigneur: et vous dites bien, car je le suis.
14 Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
Si donc moi, le Seigneur et le Maître, je vous ai lavé les pieds, vous devez aussi vous laver les pieds les uns aux autres.
15 Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
Car je vous ai donné l'exemple, afin que, comme je vous ai fait, vous fassiez aussi vous-mêmes.
16 Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
En vérité, en vérité, je vous le dis, le serviteur n'est pas plus grand que son maître, ni l'apôtre plus grand que celui qui l'a envoyé.
17 Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
Si vous savez ces choses vous êtes heureux, pourvu que vous les pratiquiez.
18 “Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
Je ne dis pas cela de vous tous; je connais ceux que j'ai élus; mais il faut que l'Écriture s'accomplisse: Celui qui mange le pain avec moi, a levé le talon contre moi.
19 Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
Je vous le dis dès maintenant, avant que la chose arrive, afin que, lorsqu'elle sera arrivée, vous reconnaissiez qui je suis.
20 Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma.”
En vérité, en vérité, je vous le dis, quiconque me reçoit, reçoit celui qui m'a envoyé. "
21 Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!”
Ayant ainsi parlé, Jésus fut troublé en son esprit; et il affirma expressément: " En vérité, en vérité, je vous le dis, un de vous me livrera. "
22 Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
Les disciples se regardaient les uns les autres, ne sachant de qui il parlait.
23 Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
Or, l'un d'eux était couché sur le sein de Jésus; c'était celui que Jésus aimait.
24 Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: “Mwulize anasema juu ya nani.”
Simon-Pierre lui fit donc signe pour lui dire: " Qui est celui dont il parle? "
25 Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, “Bwana, ni nani?”
Le disciple, s'étant penché sur le sein de Jésus, lui dit: " Seigneur, qui est-ce? "
26 Yesu akajibu, “Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye.” Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
Jésus répondit: " C'est celui à qui je présenterai le morceau trempé. " Et ayant trempé du pain, il le donna à Judas Iscariote, fils de Simon.
27 Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, “Unachotaka kufanya, kifanye haraka!”
Aussitôt que Judas l'eut pris, Satan entra en lui; et Jésus lui dit: " Ce que tu fais, fais-le vite. "
28 Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
Aucun de ceux qui étaient à table ne comprit pourquoi il lui disait cela.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
Quelques-uns pensaient que, Judas ayant la bourse, Jésus voulait lui dire: " Achète ce qu'il faut pour la fête, " ou: " Donne quelque chose aux pauvres. "
30 Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
Judas ayant pris le morceau de pain, se hâta de sortir. Il était nuit.
31 Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
Lorsque Judas fut sorti, Jésus dit: " Maintenant le Fils de l'homme a été glorifié, et Dieu a été glorifié en lui.
32 Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
Si Dieu a été glorifié en lui, Dieu aussi le glorifiera en lui-même, et il le glorifiera bientôt.
33 “Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
Mes petits enfants, je ne suis plus avec vous que pour un peu de temps. Vous me chercherez et comme j'ai dit aux Juifs qu'ils ne pouvaient venir où je vais, je vous le dis aussi maintenant.
34 Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
Je vous donne un commandement nouveau: que vous vous aimiez les uns les autres; que comme je vous ai aimés, vous vous aimiez aussi les uns les autres.
35 Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”
C'est à cela que tous connaîtront que vous êtes mes disciples, si vous avez de l'amour les uns pour les autres. "
36 Simoni Petro akamwuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon-Pierre lui dit: " Seigneur, où allez-vous? " Jésus répondit: " Où je vais, tu ne peux me suivre à présent; mais tu me suivras plus tard. —
37 Petro akamwambia “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!”
Seigneur, lui dit Pierre, pourquoi ne puis-je vous suivre à présent? Je donnerai ma vie pour vous. "
38 Yesu akajibu, “Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!”
Jésus lui répondit: " Tu donneras ta vie pour moi! En vérité, en vérité, je te le dis, le coq ne chantera pas, avant que tu ne m'aies renié trois fois. "

< Yohana 13 >