< Wahebrania 4 >

1 Mungu alituahidia kwamba tutaweza kupata pumziko hilo alilosema. Basi, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo.
Let us be afraid therefore, lest, a promise being left behind to enter into his rest, any of you should seem to have come short.
2 Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
For we also are having good news preached, just as also those men, but the word of hearing did not benefit those men, not having been mixed together with faith in those who heard.
3 Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
For those who believe enter into that rest, just as he said, So I swore in my wrath, They will not enter into my rest, although the works occurred from the foundation of the world.
4 Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”
For he spoke somewhere about the seventh this way, And God rested during the seventh day from all his works,
5 Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
and in this again, They will not enter into my rest.
6 Wale waliotangulia kuhubiriwa Habari Njema hawakupata pumziko hilo kwa sababu hawakuamini. Wapo, basi, wengine ambao wangejaliwa kulipata.
Since therefore it remains for some to enter into it, and those who formerly had good news did not enter because of disobedience,
7 Jambo hili ni wazi, kwani Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo”. Miaka mingi baadaye Mungu alisema juu ya hiyo siku kwa maneno ya Daudi katika Maandiko yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”
again he appoints a certain day, Today, saying in David after so long a time (as it is said), Today if ye will hear his voice, do not harden your hearts.
8 Kama Yoshua angaliwapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.
For if Joshua had given them rest, he would not have spoken about another day after these things.
9 Kwa hiyo, basi, bado lipo pumziko kwa watu wa Mungu kama kule kupumzika kwake Mungu siku ya saba.
There remains therefore a sabbath for the people of God.
10 Maana, kila anayepata pumziko aliloahidi Mungu atapumzika baada ya kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika baada ya yake.
For a man who has entered into his rest, he has also rested from his works, as God did from his own.
11 Basi, tujitahidi kupata pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwenu atakayeshindwa, kama walivyofanya wao kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.
Let us therefore be diligent to enter into that rest, so that not any man may fall by the same example of disobedience.
12 Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali zaidi kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na mafuta. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
For the word of God is living, and potent, and sharper, above every two-edged sword, and piercing as far as the division both of soul and spirit, of both joints and marrow, and discernible of the thoughts and intentions of the heart.
13 Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake. Kwake, sisi sote tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
And there is no creature concealed from his presence, but all things are naked and vulnerable to his eyes, before whom is the word to us.
14 Basi, tunapaswa kuzingatia kwa uthabiti imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka kwa Mungu mwenyewe—Yesu, Mwana wa Mungu.
Having therefore a great high priest who has passed through the heavens, Jesus the Son of God, let us take hold of the affirmation.
15 Huyu Kuhani Mkuu wetu si mmoja ambaye hawezi kutuunga mkono katika unyonge wetu, ila ni Kuhani Mkuu ambaye alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
For we do not have a high priest who is unable to sympathize with our weaknesses, but who was tempted in all things in the same way, without sin.
16 Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu, palipo na neema, ili tukajipatie huruma na neema ya kutusaidia wakati wa lazima.
Let us therefore come near with boldness to the throne of grace, so that we may take mercy, and may find grace for timely help.

< Wahebrania 4 >