< Wahebrania 10 >

1 Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
Porque la ley, teniendo una sombra del bien que ha de venir, y no la imagen misma de las cosas, no puede con los mismos sacrificios de año en año, que ofrecen continuamente, hacer perfectos a los que se acercan.
2 Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
De lo contrario, ¿no habrían dejado de ofrecerse, porque los adoradores, una vez purificados, ya no tendrían conciencia de los pecados?
3 Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
Pero en esos sacrificios hay un recuerdo anual de los pecados.
4 Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
Porque es imposible que la sangre de los toros y de los machos cabríos quite los pecados.
5 Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: “Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
Por eso, cuando viene al mundo, dice, “No deseabas sacrificios ni ofrendas, pero preparaste un cuerpo para mí.
6 Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
No te agradaron los holocaustos completos ni los sacrificios por el pecado.
7 Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria.”
Entonces dije: “He aquí que he venido (en el rollo del libro está escrito de mí) para hacer tu voluntad, oh Dios”.
8 Kwanza alisema: “Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi.” Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
Antes de decir: “Sacrificios y ofrendas y holocaustos completos y sacrificios por el pecado no quisiste, ni te agradaron” (los que se ofrecen según la ley),
9 Kisha akasema: “Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako.” Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
entonces ha dicho: “He venido a hacer tu voluntad”. Quita lo primero para establecer lo segundo,
10 Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
por cuya voluntad hemos sido santificados mediante la ofrenda del cuerpo de Jesucristo hecha una vez para siempre.
11 Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
En efecto, todos los sacerdotes están de pie día tras día, sirviendo y ofreciendo a menudo los mismos sacrificios, que nunca pueden quitar los pecados,
12 Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
pero él, después de haber ofrecido un solo sacrificio por los pecados para siempre, se sentó a la derecha de Dios,
13 Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
esperando desde entonces hasta que sus enemigos sean puestos como escabel de sus pies.
14 Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
Porque con una sola ofrenda ha perfeccionado para siempre a los santificados.
15 Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
El Espíritu Santo también nos da testimonio, pues después de decir,
16 “Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao.”
“Este es el pacto que haré con ellos después de esos días”, dice el Señor, “Pondré mis leyes en su corazón, También los escribiré en su mente”. entonces dice,
17 Kisha akaongeza kusema: “Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu.”
“No me acordaré más de sus pecados e iniquidades”.
18 Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
Ahora bien, donde está la remisión de éstos, no hay más ofrenda por el pecado.
19 Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
Teniendo, pues, hermanos, la seguridad de entrar en el lugar santo por la sangre de Jesús,
20 Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
por el camino que él nos dedicó, un camino nuevo y vivo, a través del velo, es decir, de su carne,
21 Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
y teniendo un gran sacerdote sobre la casa de Dios,
22 Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
acerquémonos con un corazón verdadero en la plenitud de la fe, teniendo nuestros corazones purificados de una mala conciencia y teniendo nuestro cuerpo lavado con agua pura,
23 Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
mantengamos firme la confesión de nuestra esperanza sin vacilar, porque el que prometió es fiel.
24 Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
Consideremos cómo provocarnos unos a otros al amor y a las buenas obras,
25 Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
no dejando de reunirnos, como acostumbran algunos, sino exhortándonos unos a otros, y tanto más cuanto veis que el Día se acerca.
26 Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
Porque si pecamos voluntariamente después de haber recibido el conocimiento de la verdad, ya no queda un sacrificio por los pecados,
27 Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
sino una temible expectativa de juicio y una ferocidad de fuego que devorará a los adversarios.
28 Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
El hombre que hace caso omiso de la ley de Moisés muere sin compasión por la palabra de dos o tres testigos.
29 Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
¿De qué peor castigo creéis que será juzgado el que ha pisoteado al Hijo de Dios, y ha considerado impía la sangre de la alianza con la que fue santificado, y ha insultado al Espíritu de gracia?
30 Maana tunamfahamu yule aliyesema, “Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza,” na ambaye alisema pia, “Bwana atawahukumu watu wake.”
Porque conocemos al que dijo: “La venganza me pertenece. Yo pagaré”, dice el Señor. Otra vez: “El Señor juzgará a su pueblo”.
31 Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
Es una cosa temible caer en las manos del Dios vivo.
32 Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
Pero recordad los días anteriores, en los que, después de ser iluminados, soportasteis una gran lucha con sufrimientos:
33 Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
en parte, estando expuestos tanto a los reproches como a las opresiones, y en parte, haciéndoos partícipes de los que eran tratados así.
34 Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
Pues ambos os compadecisteis de mí en mis cadenas y aceptasteis con alegría el despojo de vuestros bienes, sabiendo que tenéis para vosotros una posesión mejor y duradera en los cielos.
35 Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
Por lo tanto, no desperdiciéis vuestra audacia, que tiene una gran recompensa.
36 Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
Porque necesitáis la resistencia para que, habiendo hecho la voluntad de Dios, recibáis la promesa.
37 Maana kama yasemavyo Maandiko: “Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
“Dentro de muy poco, el que venga, vendrá y no esperará.
38 Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye.”
Pero el justo vivirá por la fe. Si se encoge, mi alma no se complace en él”.
39 Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.
Pero no somos de los que retroceden a la destrucción, sino de los que tienen fe para la salvación del alma.

< Wahebrania 10 >